GE2025 INEC, NIDA wamkana Polepole

GE2025 INEC, NIDA wamkana Polepole

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025
Kama kuna mtu kamuelewa polepole anisaidie kueleweshwa vipi kura zinapatikana kwa kuunganisha hiyo mifumo wakati kura zinapigwa kwa makaratasi.
Kura za Urais ubunge na udiwani huunganishwa kwa nchi nzima. Lakini mifumo ndiyo husaidia kujua mambo ya idadi ya wapiga kura na Demografia Yao.

Mbona Lowassa alipogombea watu wake waliokuwa wanamsaidia kuratibu uhesabuji wa kura walikamatwa na kuambiwa kuwa waliingilia mfumo wa Tume?
 
Hawa wanaona Watanzania bado ni majuha kama zamani. Siku hizi watu wanaelewa kila kitu. Pia wajue tu hatukuhitaji Polepole aongee ndio tujue michezo hii. Tulishashtuka kitambo.. Mama yao aendelee tu kutulazimishia uongozi, ila ajue hakuna marefu yasiyo na ncha.. tupo hapa.
 
Kumbe INEC na NIDA wakuu hawakulala,

Walifuatilia press ya Pole Pole usiku ule?

Sasa kwanini huwa wanazima mitandao ikiwa ni wafuatiliaji wazuri wa press zake?

Nchi ngumu hii!
 
Assume we ni mtu A, unashindana na mtu B kuhitaji kura za watu 20 ambazo mtapigiwa kwa karatasi, mtu B anavitambulisho vya watu wote 20.

Unaweza nambia nikwanamna gani Vitambulisho vitamsaidia mtu B kukuibia kura ulizopigiwa na miongoni mwa wale watu 20 ?
Kwenye majumuisho ya kura kura feki na vituo feki ndipo zinapo ingizwa kutumia huo mfumo wao
 
Subirini siku mkiitwa mbele ya sheria na kufanyiwa cross examination based on facts ndio mtajua hamjui, na mjue kusema tulikuwa tunafuata maelekezo haitawasaidia na sio defense under the law
 
Kauli ya aliyekuwa Balozi wa Tanzania nchini Cuba, Humphrey Polepole, kwamba mifumo ya Chama cha Mapinduzi (CCM) imeunganishwa na ile ya Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) na Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (Nida), imewaibua wakuu wa taasisi hizo na kukanusha madai hayo.

Wakuu hao wamebainisha kwamba hakuna mfumo wowote kwenye taasisi zao uliounganishwa na ya chama chochote cha siasa na kwamba jambo hilo si siri, na endapo lingekuwa hivyo lingekuwa tayari limejulikana.

Katika mazungumzo yake aliyoyafanya usiku wa kuamkia leo Agosti 22, 2025, Polepole amedai kwamba mifumo ambayo chama hichoimeijenga, inakiwezesha kupata ushindi hata kabla hawajakwenda kwenye uchaguzi.

INEC yakanusha

Akizungumzia tuhuma zilizoibuliwa na Polepole, Mwenyekiti wa INEC, Jaji Jacobs Mwambegele amesema hakuna mfumo wowote wa taasisi hiyo uliounganishwa na chama chochote cha siasa, hususani CCM.

“Hakuna. Sisi ni Tume huru na vitu kama mifumo kuunganisha si vitu vya siri, ukienda tu kitaalumu utajua, ni mfumo gani tuliounganisha na mtu mwingine,” amesema mwenyekiti huyo.

Jaji Mwambegele amesisitiza kwamba hata kama wangekuwa wameunganisha, hiyo inawahakikishiaje ushindi, kwani Tume hiyo inafanya kazi kwa mfumo wa dijitali? amehoji katika majibu yake.

“Kwa maana; je, kura zitapigwa kielekroniki? Kwa hiyo, hakuna kitu kama kuunganisha mifumo ya INEC na chama kingine, lakini nataka nimsikilize anavyozungumza huyo Polepole,” amesema Jaji Mwambegele.

Mwenyekiti huyo amesema mifumo yao haijaunganishwa na chama chochote cha siasa na hata Daftari la Kudumu la Wapigakura wameligawa kwa vyama vyote vya siasa, vinginevyo wangeweza kusema waunganishe katika mifumo yao ili waone.

“Lakini, daftari tumeligawa kwa vyama vyote vya siasa tangu Julai 27, 2025 kwa mfumo kidijitali na mfumo wa hardcopy (nakala ngumu),” amesema.

Jaji Mwambegele amesisitiza kwamba msimamo wa INEC, mjadala unaoendelea kuhusu kuunganisha mifumo, si wa kweli na wananchi hawapaswi kuamini hilo.

NIDA nayo yajitenga

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa Nida, James Kaji pia amesema hakuna jambo kama hilo la kuunganisha mifumo, huku akisisitiza Polepole aeleze vizuri kama aliwahi kufanya kazi na mamlaka hiyo huko nyuma.

“Hakuna kitu kama hicho. Ni vema akawaelezea vizuri labda yeye anajua na kama ameshafanya kazi Nida,” ameeleza Kaji alipoulizwa na Mwananchi kuhusu tuhuma zilizoibuliwa na Polepole kuhusu kuunganishwa kwa mifumo hiyo.

Chanzo: Mwananchi.
Hupati uteuzi acha kujisumbua wewe hakuna mwenye Akili Timamu atakaa akuelewe licha ya kujifaragua kuandika mandishi mengi yasiyo na point hata moja, ni wajinga pekee watakaa kukusikiliza
 
Ni muda wa polepole kuja kudadavua vizuri maana bado wameweka pamba masikioni
ccm wanahaha kujibu jibu chawa wanakomaa kusaka Uteuzi kupitia humo humo lakini wenye Akili Timamu wapo na polepole hawatetereki
 
Sasa kwanini tumeccm inataka mawakala wasipewe matokeo na cm wasiende nazo vituoni? Huo sio uchaguzi
Tanzania hakuna uchaguzi kuna Maigizo tu kwani ccm walishapiga kura mapema wanasubiria kutangazwa tu
 
Huyo Mwambegele kachaguliwa na nani kukaa hapo? Kifupi hana jipya.

Juzi nilihudhuria mkutano na Tume huru na Waandishi wa Habari aliambiwa ukweli kuwa Tume haikubaliwi na haitakiwi na Wananchi...huyu Jaji aliwaka utadhani mwehu.
TUME HURU YA UCHAGUZI ❎❎❎

TUME CHAFU YA UCHAGUZI ✅✅✅
 
Nilikuwa nabisha wakenya wakisema watanzania tuna IQ ndogo.

Hili la polepole limefanya niamini kweli watanzania tunashida ya kufkiria.

Mtu kwakuwa aliongea ni mtu anae muamini basi yeye anachukuwa tu km lilivyo nae kuliamini.

Sasa Akili ya kwaida tu ujiulize, access ya NIDA inakusaidia vipi kupata kura kupitia mfumo ?
Wewe ndiyo una IQ ndogo zaidi kwa kuamini kukariri Maovu ujinga wote wa ccm na kukataa ccm isikosolewe, hakuna kitu kibaya kama kujiona upo sawa kwa kila kitu na hupaswi ukosolewe milele
 
Ukweli umejulikans hata watapetape vipi hakuna wa kuwaamini labda wale mazezeta wao
 
Back
Top Bottom