GE2025 INEC, NIDA wamkana Polepole

GE2025 INEC, NIDA wamkana Polepole

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025
Kauli ya aliyekuwa Balozi wa Tanzania nchini Cuba, Humphrey Polepole, kwamba mifumo ya Chama cha Mapinduzi (CCM) imeunganishwa na ile ya Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) na Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (Nida), imewaibua wakuu wa taasisi hizo na kukanusha madai hayo.

Wakuu hao wamebainisha kwamba hakuna mfumo wowote kwenye taasisi zao uliounganishwa na ya chama chochote cha siasa na kwamba jambo hilo si siri, na endapo lingekuwa hivyo lingekuwa tayari limejulikana.

Katika mazungumzo yake aliyoyafanya usiku wa kuamkia leo Agosti 22, 2025, Polepole amedai kwamba mifumo ambayo chama hichoimeijenga, inakiwezesha kupata ushindi hata kabla hawajakwenda kwenye uchaguzi.

INEC yakanusha

Akizungumzia tuhuma zilizoibuliwa na Polepole, Mwenyekiti wa INEC, Jaji Jacobs Mwambegele amesema hakuna mfumo wowote wa taasisi hiyo uliounganishwa na chama chochote cha siasa, hususani CCM.

“Hakuna. Sisi ni Tume huru na vitu kama mifumo kuunganisha si vitu vya siri, ukienda tu kitaalumu utajua, ni mfumo gani tuliounganisha na mtu mwingine,” amesema mwenyekiti huyo.

Jaji Mwambegele amesisitiza kwamba hata kama wangekuwa wameunganisha, hiyo inawahakikishiaje ushindi, kwani Tume hiyo inafanya kazi kwa mfumo wa dijitali? amehoji katika majibu yake.

“Kwa maana; je, kura zitapigwa kielekroniki? Kwa hiyo, hakuna kitu kama kuunganisha mifumo ya INEC na chama kingine, lakini nataka nimsikilize anavyozungumza huyo Polepole,” amesema Jaji Mwambegele.

Mwenyekiti huyo amesema mifumo yao haijaunganishwa na chama chochote cha siasa na hata Daftari la Kudumu la Wapigakura wameligawa kwa vyama vyote vya siasa, vinginevyo wangeweza kusema waunganishe katika mifumo yao ili waone.

“Lakini, daftari tumeligawa kwa vyama vyote vya siasa tangu Julai 27, 2025 kwa mfumo kidijitali na mfumo wa hardcopy (nakala ngumu),” amesema.

Jaji Mwambegele amesisitiza kwamba msimamo wa INEC, mjadala unaoendelea kuhusu kuunganisha mifumo, si wa kweli na wananchi hawapaswi kuamini hilo.

NIDA nayo yajitenga

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa Nida, James Kaji pia amesema hakuna jambo kama hilo la kuunganisha mifumo, huku akisisitiza Polepole aeleze vizuri kama aliwahi kufanya kazi na mamlaka hiyo huko nyuma.

“Hakuna kitu kama hicho. Ni vema akawaelezea vizuri labda yeye anajua na kama ameshafanya kazi Nida,” ameeleza Kaji alipoulizwa na Mwananchi kuhusu tuhuma zilizoibuliwa na Polepole kuhusu kuunganishwa kwa mifumo hiyo.

Chanzo: Mwananchi.
Hatudanganyiki
nidaNecCCM.jpg
 
Sasa ...nikwamba ...Kuna uhuni unafanyika...

Kuna watu walikwenda kujiandikisha kweli kwenye daftari...na kuna watu hata hawakupata muda wa kujiandikisha...

Kinachofanyika ni wale ambao hawajajiandikisha Kuna sehemu majina yao yapo katika daftari ...kwa kufanya copy and paste kutoka NIDA., na ndio maana Kuna sehemu watu walikuta majina ya marehemu..mtu hayupo Duniani miaka 4 ila jina linasomeka...

Sasa daftari linakuwa na idadi kubwa ya watu..ile mbeleni isaidie kuongeza kura ...yaani Kuna watu watakuwa nyumbani ila watapigishwa kura bila kujijua...na hapo ndio kura feki zinawekwa kwenye mabox ya kuhesabia...

Najua utauliza wakala wanakuwa wapi...Hilo siwezi kukueleza...maana mawakala huwa wanapata Cha mtema Kuni vituoni...hata simu hawaruhusiwi kuwa nazo ili wasirekodi vituko... Nimejitahidi kukupa mwanga
..
Unaona huo ni mchakato wa kuhitaji ulink na NIDA ili ufanyike ?.

Maelezo yako it means lengo kuu nikupata Idadi kubwa ya waliojiandikisha kupiga kura.

Hivyo kura feki zitaletwa kulingana na idadi ya waliojiandikisha kwenye kupiga kura eneo husika.

Bilashaka unamaana kuna link kati ya mfumo wa iNEC na NIDA na sio daftari kitu ambacho nikawaida coz hakuna namna utaverify NIN kama huna access ya NIDA

NIDA haikupi currently address wala status ya mtu so kutumia NIDA mnaweza andikisha watu MOSHI, KLM ambao wanaishi TABATA, DSM, mnaweza andika marehemu au wagonjwa wasioweza kabisa kupiga kura.

Mifumo ya uongozi wa chini ndio inaweza kuwasaidia kuandaa kura feki kwa usahihi kiasi.

Imani hii sio inaweza sababisha taharuki kubwa miaka yote hivyo inafaa kupuzwa.

Mifumo tarajiwa ya kutrack na kuhifadhi taarifa za makazi kwa kila mtanzania, Ikiwa pamoja na status yake na anapokaa inaweza isiaminiwe na watanzia kwani kwa hoja yako it means huu mfumo utakuwa na mchango mkubwa sana katika hili zaidi ya mfumo wowote ule

Watanzania wakielewa kama ulivyoeleza wewe na wakaamini itakuwa inajengwa chuki na taharuki itayosababisha vita kubwa mno. coz jambo pekee litakuwa linasolve hili itabidi kila aliejiandikisha awe anaulizwa kama kweli alishiriki kupia kura richa yakujiandikisha "ulijiandikisha ndio, je ulipiga kura au hukupiga" ?.

Otherwise unielezee ni kwanamna gani Serikali unayoimani ikiwa madarakani itaniondolea hii hofu iliosababishwa na Imani ya kuto amini michakato.

#KUWA NA IMANI NA SERIKALI YAKO,
 
Kwa taasisi zenye accountability nilitegemea nione hawa wakuu waseme wana karibisha uchunguzi huru wa wadau ili kuji ridhisha lakini wanatoka tu kama madume ya nyani na kusema kuwa sio kweli
Tanzania ni nchi ngumu kuliko uijuavyo mkuu.
Ngumu ngumu Tena ngumu sana.
Amini maneno yangu
 
Kauli ya aliyekuwa Balozi wa Tanzania nchini Cuba, Humphrey Polepole, kwamba mifumo ya Chama cha Mapinduzi (CCM) imeunganishwa na ile ya Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) na Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (Nida), imewaibua wakuu wa taasisi hizo na kukanusha madai hayo.

Wakuu hao wamebainisha kwamba hakuna mfumo wowote kwenye taasisi zao uliounganishwa na ya chama chochote cha siasa na kwamba jambo hilo si siri, na endapo lingekuwa hivyo lingekuwa tayari limejulikana.

Katika mazungumzo yake aliyoyafanya usiku wa kuamkia leo Agosti 22, 2025, Polepole amedai kwamba mifumo ambayo chama hichoimeijenga, inakiwezesha kupata ushindi hata kabla hawajakwenda kwenye uchaguzi.

INEC yakanusha

Akizungumzia tuhuma zilizoibuliwa na Polepole, Mwenyekiti wa INEC, Jaji Jacobs Mwambegele amesema hakuna mfumo wowote wa taasisi hiyo uliounganishwa na chama chochote cha siasa, hususani CCM.

“Hakuna. Sisi ni Tume huru na vitu kama mifumo kuunganisha si vitu vya siri, ukienda tu kitaalumu utajua, ni mfumo gani tuliounganisha na mtu mwingine,” amesema mwenyekiti huyo.

Jaji Mwambegele amesisitiza kwamba hata kama wangekuwa wameunganisha, hiyo inawahakikishiaje ushindi, kwani Tume hiyo inafanya kazi kwa mfumo wa dijitali? amehoji katika majibu yake.

“Kwa maana; je, kura zitapigwa kielekroniki? Kwa hiyo, hakuna kitu kama kuunganisha mifumo ya INEC na chama kingine, lakini nataka nimsikilize anavyozungumza huyo Polepole,” amesema Jaji Mwambegele.

Mwenyekiti huyo amesema mifumo yao haijaunganishwa na chama chochote cha siasa na hata Daftari la Kudumu la Wapigakura wameligawa kwa vyama vyote vya siasa, vinginevyo wangeweza kusema waunganishe katika mifumo yao ili waone.

“Lakini, daftari tumeligawa kwa vyama vyote vya siasa tangu Julai 27, 2025 kwa mfumo kidijitali na mfumo wa hardcopy (nakala ngumu),” amesema.

Jaji Mwambegele amesisitiza kwamba msimamo wa INEC, mjadala unaoendelea kuhusu kuunganisha mifumo, si wa kweli na wananchi hawapaswi kuamini hilo.

NIDA nayo yajitenga

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa Nida, James Kaji pia amesema hakuna jambo kama hilo la kuunganisha mifumo, huku akisisitiza Polepole aeleze vizuri kama aliwahi kufanya kazi na mamlaka hiyo huko nyuma.

“Hakuna kitu kama hicho. Ni vema akawaelezea vizuri labda yeye anajua na kama ameshafanya kazi Nida,” ameeleza Kaji alipoulizwa na Mwananchi kuhusu tuhuma zilizoibuliwa na Polepole kuhusu kuunganishwa kwa mifumo hiyo.

Chanzo: Mwananchi.
Kwahiyo watu walitarajia wakubali madai ya polepole! Hayo majibu ni lazima yalitarajiwa tu.
 
Ni aliyetengeneza mfumo ndio amejitokeza kukanusha.

kwa kimombo tunaita guilty consciousness inasumbua Mzee oh sorry kijana kipili nani sijui. Asituchoshe
 
Unaona huo ni mchakato wa kuhitaji ulink na NIDA ili ufanyike ?.

Maelezo yako it means lengo kuu nikupata Idadi kubwa ya waliojiandikisha kupiga kura.

Hivyo kura feki zitaletwa kulingana na idadi ya waliojiandikisha kwenye kupiga kura eneo husika.

Bilashaka unamaana kuna link kati ya mfumo wa iNEC na NIDA na sio daftari kitu ambacho nikawaida coz hakuna namna utaverify NIN kama huna access ya NIDA

NIDA haikupi currently address wala status ya mtu so kutumia NIDA mnaweza andikisha watu MOSHI, KLM ambao wanaishi TABATA, DSM, mnaweza andika marehemu au wagonjwa wasioweza kabisa kupiga kura.

Mifumo ya uongozi wa chini ndio inaweza kuwasaidia kuandaa kura feki kwa usahihi kiasi.

Imani hii sio inaweza sababisha taharuki kubwa miaka yote hivyo inafaa kupuzwa.

Mifumo tarajiwa ya kutrack na kuhifadhi taarifa za makazi kwa kila mtanzania, Ikiwa pamoja na status yake na anapokaa inaweza isiaminiwe na watanzia kwani kwa hoja yako it means huu mfumo utakuwa na mchango mkubwa sana katika hili zaidi ya mfumo wowote ule

Watanzania wakielewa kama ulivyoeleza wewe na wakaamini itakuwa inajengwa chuki na taharuki itayosababisha vita kubwa mno. coz jambo pekee litakuwa linasolve hili itabidi kila aliejiandikisha awe anaulizwa kama kweli alishiriki kupia kura richa yakujiandikisha "ulijiandikisha ndio, je ulipiga kura au hukupiga" ?.

Otherwise unielezee ni kwanamna gani Serikali unayoimani ikiwa madarakani itaniondolea hii hofu iliosababishwa na Imani ya kuto amini michakato.

#KUWA NA IMANI NA SERIKALI YAKO,
Rejea maneno ya Polepole: ^mfumo ulikuwa na nia njema, ila ukiwa mikononi mwa watu wabaya ni hatari mno.^
 
Hiyo engo alioingia ndo imezibitisha kuwa ni kweli pole polepole kasema kweli * hatakama kama wangekuwaa wameunganisha*
 
Nilikuwa nabisha wakenya wakisema watanzania tuna IQ ndogo.

Hili la polepole limefanya niamini kweli watanzania tunashida ya kufkiria.

Mtu kwakuwa aliongea ni mtu anae muamini basi yeye anachukuwa tu km lilivyo nae kuliamini.

Sasa Akili ya kwaida tu ujiulize, access ya NIDA inakusaidia vipi kupata kura kupitia mfumo ?
NIDA inasidia kupata wapiga kura vivuli.
Je kura zao zinaingiaje kwenye kituo?
Kuna njia kadhaa za kuingiza kura hizo.
Kwahiyo Kama hujui kitu usijione mwerevu sana
 
Kauli ya aliyekuwa Balozi wa Tanzania nchini Cuba, Humphrey Polepole, kwamba mifumo ya Chama cha Mapinduzi (CCM) imeunganishwa na ile ya Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) na Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (Nida), imewaibua wakuu wa taasisi hizo na kukanusha madai hayo.

Wakuu hao wamebainisha kwamba hakuna mfumo wowote kwenye taasisi zao uliounganishwa na ya chama chochote cha siasa na kwamba jambo hilo si siri, na endapo lingekuwa hivyo lingekuwa tayari limejulikana.

Katika mazungumzo yake aliyoyafanya usiku wa kuamkia leo Agosti 22, 2025, Polepole amedai kwamba mifumo ambayo chama hichoimeijenga, inakiwezesha kupata ushindi hata kabla hawajakwenda kwenye uchaguzi.

INEC yakanusha

Akizungumzia tuhuma zilizoibuliwa na Polepole, Mwenyekiti wa INEC, Jaji Jacobs Mwambegele amesema hakuna mfumo wowote wa taasisi hiyo uliounganishwa na chama chochote cha siasa, hususani CCM.

“Hakuna. Sisi ni Tume huru na vitu kama mifumo kuunganisha si vitu vya siri, ukienda tu kitaalumu utajua, ni mfumo gani tuliounganisha na mtu mwingine,” amesema mwenyekiti huyo.

Jaji Mwambegele amesisitiza kwamba hata kama wangekuwa wameunganisha, hiyo inawahakikishiaje ushindi, kwani Tume hiyo inafanya kazi kwa mfumo wa dijitali? amehoji katika majibu yake.

“Kwa maana; je, kura zitapigwa kielekroniki? Kwa hiyo, hakuna kitu kama kuunganisha mifumo ya INEC na chama kingine, lakini nataka nimsikilize anavyozungumza huyo Polepole,” amesema Jaji Mwambegele.

Mwenyekiti huyo amesema mifumo yao haijaunganishwa na chama chochote cha siasa na hata Daftari la Kudumu la Wapigakura wameligawa kwa vyama vyote vya siasa, vinginevyo wangeweza kusema waunganishe katika mifumo yao ili waone.

“Lakini, daftari tumeligawa kwa vyama vyote vya siasa tangu Julai 27, 2025 kwa mfumo kidijitali na mfumo wa hardcopy (nakala ngumu),” amesema.

Jaji Mwambegele amesisitiza kwamba msimamo wa INEC, mjadala unaoendelea kuhusu kuunganisha mifumo, si wa kweli na wananchi hawapaswi kuamini hilo.

NIDA nayo yajitenga

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa Nida, James Kaji pia amesema hakuna jambo kama hilo la kuunganisha mifumo, huku akisisitiza Polepole aeleze vizuri kama aliwahi kufanya kazi na mamlaka hiyo huko nyuma.

“Hakuna kitu kama hicho. Ni vema akawaelezea vizuri labda yeye anajua na kama ameshafanya kazi Nida,” ameeleza Kaji alipoulizwa na Mwananchi kuhusu tuhuma zilizoibuliwa na Polepole kuhusu kuunganishwa kwa mifumo hiyo.

Chanzo: Mwananchi.
Kama ingekuwa kweli wangekiri hadharani?
 
Kama kuna mtu kamuelewa polepole anisaidie kueleweshwa vipi kura zinapatikana kwa kuunganisha hiyo mifumo wakati kura zinapigwa kwa makaratasi.
Mchezo unaanzia wakati wa kuandikisha pale. Majina yanaingia kwenye orodha.
Hata wasipotokea kituoni mchezo unakuja kumalizika wakati wa kujumlisha kura za vituo mbali mbali
 
Unaona huo ni mchakato wa kuhitaji ulink na NIDA ili ufanyike ?.

Maelezo yako it means lengo kuu nikupata Idadi kubwa ya waliojiandikisha kupiga kura.

Hivyo kura feki zitaletwa kulingana na idadi ya waliojiandikisha kwenye kupiga kura eneo husika.

Bilashaka unamaana kuna link kati ya mfumo wa iNEC na NIDA na sio daftari kitu ambacho nikawaida coz hakuna namna utaverify NIN kama huna access ya NIDA

NIDA haikupi currently address wala status ya mtu so kutumia NIDA mnaweza andikisha watu MOSHI, KLM ambao wanaishi TABATA, DSM, mnaweza andika marehemu au wagonjwa wasioweza kabisa kupiga kura.

Mifumo ya uongozi wa chini ndio inaweza kuwasaidia kuandaa kura feki kwa usahihi kiasi.

Imani hii sio inaweza sababisha taharuki kubwa miaka yote hivyo inafaa kupuzwa.

Mifumo tarajiwa ya kutrack na kuhifadhi taarifa za makazi kwa kila mtanzania, Ikiwa pamoja na status yake na anapokaa inaweza isiaminiwe na watanzia kwani kwa hoja yako it means huu mfumo utakuwa na mchango mkubwa sana katika hili zaidi ya mfumo wowote ule

Watanzania wakielewa kama ulivyoeleza wewe na wakaamini itakuwa inajengwa chuki na taharuki itayosababisha vita kubwa mno. coz jambo pekee litakuwa linasolve hili itabidi kila aliejiandikisha awe anaulizwa kama kweli alishiriki kupia kura richa yakujiandikisha "ulijiandikisha ndio, je ulipiga kura au hukupiga" ?.

Otherwise unielezee ni kwanamna gani Serikali unayoimani ikiwa madarakani itaniondolea hii hofu iliosababishwa na Imani ya kuto amini michakato.

#KUWA NA IMANI NA SERIKALI YAKO,
Mkuu..nakuhakikishia daftari la wapiga kura..Lina majina mengi sana ya marehemu, wengine hata hawapo ndani ya nchi, wengine Wagonjwa ambao hata Kwenda kuboresha taarifa zao hawawezi...
Lakini kwakuwa daftari Lina chukua direct majina kutoka NIDA na kuyabandika...unaweza kukuta wewe jina lako lipo Bukoba na hukujiandikisha....
Hivi unaamini wapiga kura millioni 37 wamejiandikisha ?
 
Waruhusu wakaguzi huru waikague hiyo mifumo inayodaiwa kudukuliwa tumalize ubishi hizi tantalila zao kama wapiga debe hatuzihitaji kwa sasa.
 
Waruhusu wakaguzi huru waikague hiyo mifumo inayodaiwa kudukuliwa tumalize ubishi hizi tantalila zao kama wapiga debe hatuzihitaji kwa sasa.
Watavuliwa Nguo Ikikaguliwa
Yaani CCM,INEC,NIDA Wameshikwa Pabaya
 
Unaona huo ni mchakato wa kuhitaji ulink na NIDA ili ufanyike ?.

Maelezo yako it means lengo kuu nikupata Idadi kubwa ya waliojiandikisha kupiga kura.

Hivyo kura feki zitaletwa kulingana na idadi ya waliojiandikisha kwenye kupiga kura eneo husika.

Bilashaka unamaana kuna link kati ya mfumo wa iNEC na NIDA na sio daftari kitu ambacho nikawaida coz hakuna namna utaverify NIN kama huna access ya NIDA

NIDA haikupi currently address wala status ya mtu so kutumia NIDA mnaweza andikisha watu MOSHI, KLM ambao wanaishi TABATA, DSM, mnaweza andika marehemu au wagonjwa wasioweza kabisa kupiga kura.

Mifumo ya uongozi wa chini ndio inaweza kuwasaidia kuandaa kura feki kwa usahihi kiasi.

Imani hii sio inaweza sababisha taharuki kubwa miaka yote hivyo inafaa kupuzwa.

Mifumo tarajiwa ya kutrack na kuhifadhi taarifa za makazi kwa kila mtanzania, Ikiwa pamoja na status yake na anapokaa inaweza isiaminiwe na watanzia kwani kwa hoja yako it means huu mfumo utakuwa na mchango mkubwa sana katika hili zaidi ya mfumo wowote ule

Watanzania wakielewa kama ulivyoeleza wewe na wakaamini itakuwa inajengwa chuki na taharuki itayosababisha vita kubwa mno. coz jambo pekee litakuwa linasolve hili itabidi kila aliejiandikisha awe anaulizwa kama kweli alishiriki kupia kura richa yakujiandikisha "ulijiandikisha ndio, je ulipiga kura au hukupiga" ?.

Otherwise unielezee ni kwanamna gani Serikali unayoimani ikiwa madarakani itaniondolea hii hofu iliosababishwa na Imani ya kuto amini michakato.

#KUWA NA IMANI NA SERIKALI YAKO,
2010 ulikuwa na umri gani mkuu?
Ulisikia malalamiko ya Dr. Slaa kwenye matokeo ya Urais.
Matokeo yanayotangazwa na tume yalikuwa tofauti na kwenye karatasi walizohesabia vituoni
 
Back
Top Bottom