blackberry m
JF-Expert Member
- Apr 16, 2012
- 563
- 415
MWANAUME mmoja kutoka katika familia maskini inayoishi mjini Bhawanipatna katika jimbo la Orissa nchini, amelazimika kuubeba mwili wa mkewe begani, baada ya hospitali kushindwa kutoa gari la kubebea mwili huo.
Dana Majhi alikutwa na masahibu hayo, baada ya aliyekuwa mke wake, Amang kufariki dunia katika hospitali ya wilaya, kutokana na kuugua kwa muda mrefu ugonjwa wa Kifua Kikuu.
Mara baada ya mkewe kufariki, Majhi (42) alianza taratibu zote za kusafirisha mwili wa mke wake, kwa kuulizia gari maalum lililotolewa na Serikali kwa ajili ya shughuli hizo.
Cha ajabu, uongozi wa hospitali hiyo ulimjibu kuwa gari hilo halipo hivyo kumlaimu Majhi kuuandaa mwili wa mkewe na kuanza kuubeba, kuelekea kijiji kwake ambako kuna umbali wa kilometa 60 kutoka hospitalini hapo.
Mara baada ya Majhi kukamilisha kuuandaa mwili wa mke wake, aliianza safari ya kuelekea kijijini kwake Melghar, huku akiwa ameubeba mwili huo begani pamoja na kusindikizwa na mwanae wa kike mwenye umri wa miaka 12, Chaula. Hata hivyo, uongozi wa hospitali hiyo, ulikana kumnyima gari la kubebea maiti mwanaume huyo maskini.
Akizungumza kuhusu hilo, Ofisa mmoja wa hospitali hiyo, B Brahma alisema mwanamke huyo alifikishwa hospitalini hapo Jumanne mchana na kufariki siku hiyo hiyo, na mume wake kuubeba mwili wa mkewe pasina kuutaarifu uongozi wa hospitali hiyo.
“Mwanamke huyo aliyekuwa akisumbuliwa na Kifua Kikuu (TB), alifikishwa hapa Jumanne mchana, na kufariki dunia siku hiyo hiyo. Cha ajabu, mumewe aliamua kuubeba mwili wa mkewe, pasipo kutoa taaria kwa uongozi wa hospitali,” alisema Brahma.
Dana Majhi alikutwa na masahibu hayo, baada ya aliyekuwa mke wake, Amang kufariki dunia katika hospitali ya wilaya, kutokana na kuugua kwa muda mrefu ugonjwa wa Kifua Kikuu.
Mara baada ya mkewe kufariki, Majhi (42) alianza taratibu zote za kusafirisha mwili wa mke wake, kwa kuulizia gari maalum lililotolewa na Serikali kwa ajili ya shughuli hizo.
Cha ajabu, uongozi wa hospitali hiyo ulimjibu kuwa gari hilo halipo hivyo kumlaimu Majhi kuuandaa mwili wa mkewe na kuanza kuubeba, kuelekea kijiji kwake ambako kuna umbali wa kilometa 60 kutoka hospitalini hapo.
Mara baada ya Majhi kukamilisha kuuandaa mwili wa mke wake, aliianza safari ya kuelekea kijijini kwake Melghar, huku akiwa ameubeba mwili huo begani pamoja na kusindikizwa na mwanae wa kike mwenye umri wa miaka 12, Chaula. Hata hivyo, uongozi wa hospitali hiyo, ulikana kumnyima gari la kubebea maiti mwanaume huyo maskini.
Akizungumza kuhusu hilo, Ofisa mmoja wa hospitali hiyo, B Brahma alisema mwanamke huyo alifikishwa hospitalini hapo Jumanne mchana na kufariki siku hiyo hiyo, na mume wake kuubeba mwili wa mkewe pasina kuutaarifu uongozi wa hospitali hiyo.
“Mwanamke huyo aliyekuwa akisumbuliwa na Kifua Kikuu (TB), alifikishwa hapa Jumanne mchana, na kufariki dunia siku hiyo hiyo. Cha ajabu, mumewe aliamua kuubeba mwili wa mkewe, pasipo kutoa taaria kwa uongozi wa hospitali,” alisema Brahma.