Mimi mwanadamu ni nini hata nijidai?Kwani mimi nilieumbwa kwa mwili wa nyama na pumzi ya msaada ni nani hata nilewe madaraka?
Mimi ni msafiri,Mpita njia na mpangaji katika Ulimwengu huu uliojaaa dhiki na taabu.
Nina nini mimi?Eti nina jeshi na pesa?Hapana...Hivyo vyote havitanizuia kufa na kuoza na kuliwa na funza.
Nina magari na nyumba za kifahari kushinda wenzangu?Hapana...Hata moja sitazikwa nayo,Yote na ufahari wake nitaziacha nyuma.
Sasa mimi ni nani eti??Mimi si kitu,mimi si lolote...Nijapopita katikati ya majeshi yanayonitii na watu wanaoniogopa...bado mimi si lolote!!Mimi ni fukara na masikini wa mwili na roho.. kiburi na majivuno ya ubinadamu yananidanganya.
Mimi ni mavumbi,katika mavumbi nimetoka,na mavumbini nitarudi....Nitaoza kwa kuliwa na funza...Kilo kilicho changu katika mwili huu wa nyama ktapukutika...Utabaki unywele tu katika shimo la kaburi ili kutimiza hesabu mbele za yeye aliye mkuu kuliko wote.
Thamani yangu si lolote...Nisijivune,Nisijigambe,Nisinyanyase,Nisihusudu vilivyo vya ulimwengu na kuyaacha maisha yasiyo na kikomo.Eee Mungu unirehemu...Kwa kuwa mimi ni mdhambi.