Inawezekana kweli?

Inawezekana kweli?

Nimewahi kupitia unayopitia na ndio ilikuwa mara yangu ya kwanza kuijua JF kwasababu katika kugoogle namna ya kusahau mtu nikaletwa huku JF

Nilikuwa natamani kulia lakini machozi hayaji
Appetite ikapotea
Nikapiga hata simu nyumbani kuomba kughairisha mwaka manake nilijiona hata darasani hakieleweki

Nikaweka uzi humu wa kuomba msaada wa namna ya kumsahau ambapo kimsingi nilipata mawazo kadhaa ambayo yalinisaidia kiasi chake

Kimsingi kilichonisaidia kupotezea ni baada ya kuweka mbele mambo ya msingi zaidi katika maisha yangu,nikaanza kutumia muda wangu mwingi kusoma sana kwasababu ndio kilinipeleka kule

Nikaanza kufikiria mtu nayempenda zaidi katika hii dunia ambaye ni baba yangu,nikaanza kuwasiliana nae sanaaaaaa

Nikaanza kwenda kanisani siku za jumapili na jumamosi kufanya usafi

Jitahidi kuwa busy na mambo yako,hayo unayopitia sasa hayatakuwa hivyo milele....pole,pambana

Oh asante mamy!
 
Jambo sahihi ni kutulia na kujifanya huna haja na mapenzi, acha yachipue upya kwa mtu sahihi kwa wakati wake
 
Kama ilivo kwenye maisha kuna kupata na kukosa haijalishi ni kiasi gani hiko kitu ulikihitaji na ndivo yalivo mapenzi. Sio kila unalolitegemea litokee huja kama ulivopanga. Likija kinyume hutokea maumivu. Lakini kama kwenye maisha hutokea kupoteza either mzazi mmoja na kukubaliana na hio hali na maisha yakaendelea. kwann kwenye mapenzi ushindwe. Hivo cha kwanza ni wewe KUKUBALIANA na hio hali kua umeachwa na kua unaweza kuishi bila yeye. Wanasemaga pia MUDA NI TABIBU WA KWELI. Jipe muda tu itafika kipindi utasahau maumivu yote na maisha yataendelea.ni hayo tu
Wako kilaza
 
They say it takes half the time you dated to move on. Kama ulidate miaka 6 itakuchukua miaka 3 kumsahau huyo jamaa.


Anyways binafsi nishawahi kupitia mvunjiko moyo mara kadhaa ila mara ya mwisho ilikua balaa . Ila kumbuka mda ndio daktari wa ukweli. Mean time jaribu kufanya changes kadhaa ili uyaone maisha yako yanebadilika yani unahitaji maisha mapya ili uweze kusahau ya zamani. Hama mji unaoishi kama huwezi hama mtaa/ nyumba etc. Tafuta hobby mpya. Kama ulikua hufanyi mazoezi/ jogging anza, join gym nisehemu nzuri kukutana na watu wapya. Ila usianze drugs/ alcohol kwa wakati huu utapotea unless ni mtumiaji wa muda.

Yani became a new person, dress well, eat really good,work out, look good, smell good, start a new business, try to gain your self esteem back finally bila kujua one day utaamka asubuhi life will feel good again n utakua ushamove on.

All the best!
 
Leo nimepokea msg kutoka kwa mdada niliyemzingua yapata miaka 2 iliyopita kiukweli alizama na mimi nilimtamani tu baada ya kumuacha yule binti nkajua ashasahau na kusamehe lakini juzi ndo nkapokea Ujumbe toka kwake akielezea namna gani nilimuumiza kiukweli ilibidi nimuombee msamaha na kiukweli nimejisikia vibaya sana.. Pole sana dada yatakwisha tu
 
Kwanza jitahidi uitambue thamani yako,hakuna haja ya kujishusha sana kuyabembeleza mahusiano yaliyokwisha yatakutesa,
Jitahidi kutingwa na vitu vingine kama kazi na marafiki au kutembelea sehemu unazozipenda wewe sio mlizokua mnaenda wote.
Usiingie kwenye mahusiano mengine kwa pupa au kulipiza kisasi yatakuchanganya zaidi.

Kila lenye mwanzo halikosi mwisho,kama uliweza kuacha titi la mama yako sembuse mwanaume tu asiyekuthamini?Mbona wapo wengi sana au ya kwake ilikua ya dhahabu inakojoa vanilla na chocolate? Muwe mnayapitia na matokeo ya sensa ya taifa maana unavyolalamika utafikiri mlikua wawili tu kisiwani.

Maji yakimwagika unayapigia deki kama ni kwenye simenti au vigae lakini chini na we unayapiga chini.
 
Kama ilivo kwenye maisha kuna kupata na kukosa haijalishi ni kiasi gani hiko kitu ulikihitaji na ndivo yalivo mapenzi. Sio kila unalolitegemea litokee huja kama ulivopanga. Likija kinyume hutokea maumivu. Lakini kama kwenye maisha hutokea kupoteza either mzazi mmoja na kukubaliana na hio hali na maisha yakaendelea. kwann kwenye mapenzi ushindwe. Hivo cha kwanza ni wewe KUKUBALIANA na hio hali kua umeachwa na kua unaweza kuishi bila yeye. Wanasemaga pia MUDA NI TABIBU WA KWELI. Jipe muda tu itafika kipindi utasahau maumivu yote na maisha yataendelea.ni hayo tu
Wako kilaza

Naelewa kila kitu kaka sema huu uchungu wakati muda unazidi kwenda ndo unaonisumbua ila kama muda ni tabibu wa kweli, ipo siku itabaki story tu.
 
Kwanza jitahidi uitambue thamani yako,hakuna haja ya kujishusha sana kuyabembeleza mahusiano yaliyokwisha yatakutesa,
Jitahidi kutingwa na vitu vingine kama kazi na marafiki au kutembelea sehemu unazozipenda wewe sio mlizokua mnaenda wote.
Usiingie kwenye mahusiano mengine kwa pupa au kulipiza kisasi yatakuchanganya zaidi.
Kila lenye mwanzo halikosi mwisho,kama uliweza kuacha titi la mama yako sembuse mwanaume tu asiyekuthamini?Mbona wapo wengi sana au ya kwake ilikua ya dhahabu inakojoa vanilla na chocolate? Muwe mnayapitia na matokeo ya sensa ya taifa maana unavyolalamika utafikiri mlikua wawili tu kisiwani.
Maji yakimwagika unayapigia deki kama ni kwenye simenti au vigae lakini chini na we unayapiga chini.

Hahaha yani mtu ukimchukulia kama kila kitu (rafiki, kaka, mpenzi) alafu ukampoteza inauma sana! Ngoja nami niyapige chini hayo maji maana yamemwagika mchangani
 
Hahaha yani mtu ukimchukulia kama kila kitu (rafiki, kaka, mpenzi) alafu ukampoteza inauma sana! Ngoja nami niyapige chini hayo maji maana yamemwagika mchangani
Huwezi jua,dhahabu ili ing'ae inapitishwa kwenye moto labda Mungu amekuandalia mzuri zaidi na ndoa juu.
 
They say it takes half the time you dated to move on. Kama ulidate miaka 6 itakuchukua miaka 3 kumsahau huyo jamaa.


Anyways binafsi nishawahi kupitia mvunjiko moyo mara kadhaa ila mara ya mwisho ilikua balaa . Ila kumbuka mda ndio daktari wa ukweli. Mean time jaribu kufanya changes kadhaa ili uyaone maisha yako yanebadilika yani unahitaji maisha mapya ili uweze kusahau ya zamani. Hama mji unaoishi kama huwezi hama mtaa/ nyumba etc. Tafuta hobby mpya. Kama ulikua hufanyi mazoezi/ jogging anza, join gym nisehemu nzuri kukutana na watu wapya. Ila usianze drugs/ alcohol kwa wakati huu utapotea unless ni mtumiaji wa muda.

Yani became a new person, dress well, eat really good,work out, look good, smell good, start a new business, try to gain your self esteem back finally bila kujua one day utaamka asubuhi life will feel good again n utakua ushamove on.

All the best!

Pole na hongera kwa kuipita hiyo phase! Si mchezo mi natamani niamke it’s 2022 already! Iwe imebaki story! Na sio rahisi kumove on kama watu wanavoshauri ila kama ndo fate yangu sina namna
 
Leo nimepokea msg kutoka kwa mdada niliyemzingua yapata miaka 2 iliyopita kiukweli alizama na mimi nilimtamani tu baada ya kumuacha yule binti nkajua ashasahau na kusamehe lakini juzi ndo nkapokea Ujumbe toka kwake akielezea namna gani nilimuumiza kiukweli ilibidi nimuombee msamaha na kiukweli nimejisikia vibaya sana.. Pole sana dada yatakwisha tu

Miaka miwili jamani! Kweli hii issue sio mchezo! Asante
 
Jambo sahihi ni kutulia na kujifanya huna haja na mapenzi, acha yachipue upya kwa mtu sahihi kwa wakati wake

Issue sio kuwa na haja ya mapenzi, ni uchungu tu niliobaki nao wala si kingine!
Asante kwa ushauri pia
 
Kumsahau unae mfahamu na mliezoeana Sana,nisawa nakumkumbuka usie mjua Wala kuwa naukaribu nae....Mim ilintokea iyo huu nimwaka6 Sasa nakla mtu anamaisha yake lakn paka leo nmeshndwa kusahau kabsa nainansumbua kchwani pamoja nakutoka mkoa ule...labda Kama uyo wako hakuna makubwa mliowah kufanya na hamkuachana kwamatat o makubwa utaweza fankiwa.chamsngi jarbu kupambania maisha yako tu.... Naujfunze kupenda kwatahadhali...mfano me sasaiv habar yamapenz yadhati staki tena kuiskia Nisha jifunza binadamu niwakatili......mapenzi yakweli nadhati yapo kwababa na mamayako tu hao ndio hawatokuacha ata upatwe nanini.......jitaidi kujiweka bze tu muda wore....it's punguza ila sio kusahau kabsa huo niuongo labda kama age yako ipo kwenye foolish age....apa ndio huwa inakuwa Kama moja yahatua yaukuaji ila Kama tayar umekomaa kiakl huwez kumsahau mazima.lazma moyoni mwako kutakua namambo mawili....kinyongo cha kisasi,au dua mbaya yeye kuhalbikiwa mambo yake paka aje ku conface kwako kwaunyama alio tenda
 
Back
Top Bottom