Inashangaza Mkuu wa Chuo cha Usafirishaji Tanzania (NIT) kuisemea Serikali

Mkuu wa Chuo Cha Usafirishaji kwa kauli aliyoitoa kwamba madereva warudi shuleni na hatimaye kusababisha mgomo katika sekta ya usafirishaji na matokeo ya mgomo huo kuleta hasara kubwa kwa taifa. Je; Mkuu huyo wa chuo anachukuliwa hatua gani baada ya serikali kusalimu amri kwa madereva?

Je; ni hasara kiasi gani iliyosababishwa na mgomo huo uliodumu kwa saa 9? Madhara ya mwananchi mmoja mmoja ni pamoja na kufukuzwa kazi kwa kuchelewa/ kutofika kibaruani jana; wagonjwa kushindwa kufika hospitali kwa wakati n.k.

Je; Ni nani atakayeendelea kubeba mzigo huu pamoja na ule mgomo wa wafanyabiashara? Je; Nchi hii inaongozwa au inajiongoza?
Hivi hakuna walioathiriwa na mgomo huo wanaoweza kufungua daawa mahakamani?!
 
Mbona hawaambii Polisi warudi CCP Kwa ajili wanaporwa silaha kila kukicha.

Hawawezi kuwaambia Polisi warudi CCP kwasababu CCP hawalipi ada itakula kwa serikali...tunataka Madereva warudi Darasani siyo kwasababu ya kuchukia ajali na kuwapenda watanzania ...hapana tulitaka kujipigia vihela tule tu laki tano
 
Huyo Mkuu wa Chuo ni kweli anatakiwa ashtakiwe kwa kuingilia majukumu ambayo si ya kwake. Licha ya hilo Kova nae nimeona akisema tochi hakuna, ametoa tamko hilo akiwa kama nani?

Yaani hii nchi isikie tuu kova nahisi kawa msemaji wa jeshi la polisi.
 
Kati ya wote aliyeniacha hoi ni kova tu....."Madereva oyee"Oyeeeee......alf akapiga kuanzia sasa hakuna toch....sasa sijui alifikiri kwanza kabla ya kuongea au alijilopokea tu.. .dah! Duniani humu....
nadhani alitoa hiyo amri akidhani yeye ni afande Mpinga au IGP
 
Kazi kweli kweli serikali inaongozwa na prof.kikwete,kutoka msoga.tutakukumbuka kwa kutuletea tezi dume tz.
 
Nilicheka sana baada ya waziri kumkana Mkuu Wa Chuo. Dili ya pesa za kuhonga wakati Wa uchaguzi imeyeyuka.EFD nayo ilibuma,CCM hawaamini macho na masikio yako jinsi watz wwalivyojanjaruka. Kama hawakumtuma wao wamshtaki mkuu Wa Chuo tuone.
 
Mkuu wa Chuo Cha Usafirishaji kwa kauli aliyoitoa kwamba madereva warudi shuleni na hatimaye kusababisha mgomo katika sekta ya usafirishaji na matokeo ya mgomo huo kuleta hasara kubwa kwa taifa. Je; Mkuu huyo wa chuo anachukuliwa hatua gani baada ya serikali kusalimu amri kwa madereva?

Je; ni hasara kiasi gani iliyosababishwa na mgomo huo uliodumu kwa saa 9? Madhara ya mwananchi mmoja mmoja ni pamoja na kufukuzwa kazi kwa kuchelewa/ kutofika kibaruani jana; wagonjwa kushindwa kufika hospitali kwa wakati n.k.

Je; Ni nani atakayeendelea kubeba mzigo huu pamoja na ule mgomo wa wafanyabiashara? Je; Nchi hii inaongozwa au inajiongoza?

nchi inajiongoza coz sasa hv kila kitu utasikia mgomo af viongoz vivuli ndio wanajitokeza na wanajitokeza baada ya madhara kutokea....
hatari sana kwa taifa letu!
Mungu ibariki Tanzania
 
Back
Top Bottom