Inaonekana kila wizi mkubwa wa mali ya umma upo mkono wa serikali

Byendangwero

JF-Expert Member
Oct 24, 2010
871
56
Katika hali halisi serikali ndiyo yenye dhamana ya kulinda mali ya umma.

Mali hiyo ya umma siyo ya viongozi wa serikali bali ni ya watanzania wote. Katika miaka ya hivi karibuni kumezuka mtindo wa wale walioko madarakani kujiamria wao wenyewe kujigawia mali ya umma kama kwamba ni ya kwao binafsi. Na hivyo tumeshuhudia wakati wa awamu ya pili viongozi waandamizi serikalini wakijiuzia nyumba za serikali kwa bei ya kutupwa.

Mbali ya hayo kumekuwepo matukio mengi ya wizi wa mali za umma k.m EPA, meremeta, Tangold, Rada n.k. Jambo la kushangaza badala ya serikali kuonyesha umakini katika kushughulikia masuala hayo imekua ikitumia nguvu nyingi kuzima ukweli husijitokeze! Wadadisi wa mambo wanasema hii inatokana na baadhi ya viongozi wa juu serikalini kuhusika moja kwa moja katika sakata hizo.

Swali la kujiuliza ni je kama mikono ya serikali ya kuhifadhi mali ya umma hivi sasa imefungwa, nani mwenye dhamana ya kuhifadhi mali hizo?
 
Katika hali halisi serikali ndiyo yenye dhamana ya kulinda mali ya umma.

Mali hiyo ya umma siyo ya viongozi wa serikali bali ni ya watanzania wote. Katika miaka ya hivi karibuni kumezuka mtindo wa wale walioko madarakani kujiamria wao wenyewe kujigawia mali ya umma kama kwamba ni ya kwao binafsi. Na hivyo tumeshuhudia wakati wa awamu ya pili viongozi waandamizi serikalini wakijiuzia nyumba za serikali kwa bei ya kutupwa.

Mbali ya hayo kumekuwepo matukio mengi ya wizi wa mali za umma k.m EPA, meremeta, Tangold, Rada n.k. Jambo la kushangaza badala ya serikali kuonyesha umakini katika kushughulikia masuala hayo imekua ikitumia nguvu nyingi kuzima ukweli husijitokeze! Wadadisi wa mambo wanasema hii inatokana na baadhi ya viongozi wa juu serikalini kuhusika moja kwa moja katika sakata hizo.

Swali la kujiuliza ni je kama mikono ya serikali ya kuhifadhi mali ya umma hivi sasa imefungwa, nani mwenye dhamana ya kuhifadhi mali hizo?
Kuiweka hii sawa ni viongozi wa awamu ya tatu (BWM) ndio waliojipa nyumba za serikali na sio awamu ya pili kama ulivyoandika kwani awamu ya pili ilikuwa ni ya mzee ruksa (Baba yake Hussein Mwinyi).
 
Back
Top Bottom