BRO LEE
JF-Expert Member
- Dec 25, 2011
- 826
- 600
Kuna jambo ambalo huwa linanisikitisha sana ninapohudhuria baadhi ya misiba, jambo hilo hunifanya hata nitokwe na machozi hata kama wahusika wa msiba si wa2 wa karibu. Jambo hilo nimekutana nalo tena leo hii si msibani bali katika dadadala.
Kuna mama m1 alikuwa analia kuwa kwikwi na kwa uchungu mkubwa, ikabidi abiria wa karibu amwulize kulikoni, ndipo alipofunguka kwamba amepewa taarifa kwamba mumewe amefariki!, ikabidi abiria waanze kumpa pole na kutupa lawama kwa aliye mtaarifu kwa njia ya simu. Mama huyu alipokuwa anafarijiwa ndipo alipoaanza kulia zaidi na kusema mumewe kamwachia watoto wa4 na wa kwanza yupo darasa la nne atawatunza vipi.
Suala la wanawake wanapofiwa kulia kwa uchungu kwa kuwaza mzigo wa familia ulioachwa na marehemu ndo huniumiza, mara nyingine utamsikia mama anasema kwanini umeniachia huu mzigo, bora ningetangulia mm, nilikwambia tufanye... ukabisha sasa watoto nitawapeleka wapi n.k.
Napenda kufahamu kutoka kwako je mazingira haya ya kuliliwa ukifa kwa minajili ya matatizo utakayoacha nyuma unayaona/kumlilia marehemu mumeo kwa mzigo wa familia anayoacha unayaona? Kwa wewe ambaye mme akiondoka duniani leo bado utakuwa hutatetereki kwa maswala ya kiuchumi unashauri nini?
Nini kifanyike katika familia ili mmoja anapotangulia mbele ya haki anayebaki amkose/am-miss kwa yale mambo ambayo ni passion zaidi? mf. mke alie akisema mme wangu umeondoka tabasamu lako nitalipata wapi, upole wako nitaupata wapi? n.k
Kuna mama m1 alikuwa analia kuwa kwikwi na kwa uchungu mkubwa, ikabidi abiria wa karibu amwulize kulikoni, ndipo alipofunguka kwamba amepewa taarifa kwamba mumewe amefariki!, ikabidi abiria waanze kumpa pole na kutupa lawama kwa aliye mtaarifu kwa njia ya simu. Mama huyu alipokuwa anafarijiwa ndipo alipoaanza kulia zaidi na kusema mumewe kamwachia watoto wa4 na wa kwanza yupo darasa la nne atawatunza vipi.
Suala la wanawake wanapofiwa kulia kwa uchungu kwa kuwaza mzigo wa familia ulioachwa na marehemu ndo huniumiza, mara nyingine utamsikia mama anasema kwanini umeniachia huu mzigo, bora ningetangulia mm, nilikwambia tufanye... ukabisha sasa watoto nitawapeleka wapi n.k.
Napenda kufahamu kutoka kwako je mazingira haya ya kuliliwa ukifa kwa minajili ya matatizo utakayoacha nyuma unayaona/kumlilia marehemu mumeo kwa mzigo wa familia anayoacha unayaona? Kwa wewe ambaye mme akiondoka duniani leo bado utakuwa hutatetereki kwa maswala ya kiuchumi unashauri nini?
Nini kifanyike katika familia ili mmoja anapotangulia mbele ya haki anayebaki amkose/am-miss kwa yale mambo ambayo ni passion zaidi? mf. mke alie akisema mme wangu umeondoka tabasamu lako nitalipata wapi, upole wako nitaupata wapi? n.k