Inamaanisha nini?

hahahahah... usichukulie kuwa kwa vile yeye kakutwa ok na wewe uko ok... ushasikia kuhusu discordant couples?
Leo mbona umenishupalia hivi mama! LOL! Ninalo!
Ila kupima? Hapana mama! Naomba msamaha wako.
Hizo couples nshazisikia. Maadam yeye yuko OK, potelea mbali kama mimi nimekanyaga. At least Matesha atalelewa na mama wakati mimi nimesharest in peace! Kupima hapana mama, hivi nilishakuomba samahani? Nisamehe mama ushauri!
 
Samahani ya nini tena CHRIS?....
HAYA ngoja nikuache.... kama hujakubali basi tena .....lakini mada inaendelea...
 
Mwache alie
Nakubali machozi ni therapeutic kwani yanamfanya mtu arelease tension lakini siyo kumwacha alie kama kumkomoa waweza kumshauri atulie. Ila best kwa reaction ya huyo bwana siyo siri kuna jambo linaendelea. Mpe pole!
 
Yaani Babu hakuna siku niliyocheka kama leo!! kumbe mwoga namna hii? Ngoja nikakusemee kwa Grandma
 


haaa huyo mama nae alikuwa na moyo, 12yrs unalirudia limtu mweh....hivi ni msamaha wa aina gani huo? hapana.
 
Newton's first law of motion inasemaje wakulu?

Huyo shistito aliamua tu 'kuchafua hali ya hewa' kwa kuuliza kitu kama hicho halafu eti majibu yawe 'ndiyo au hapana'

mimi naamini, kama angemuuliza wakati muafaka, sehemu muafaka, na kuliframe swali lake, asingekumbana na hayo....kuna mmoja hapa amesema wanaume tunafanya reasoning zaidi kwenye haya mambo...ndio kusema tupo more rational...ikijumuisha kupima athari za majibu na pia motives za muuliza swali

sasa hapa inaonekana swali liliulizwa huku shosti akionekana wazi kwamba anamhisi mumewe kutembea naye ndo akaruka kimanga,

Ushauri wa kwenda kupima..tunarudi kule kwen topic ya WoS kwamba lazima apime kwa akili hasara na faida iwapo atagunulika ameambukizwa!

ushauri wangu kwa shosti ni kwamba bora akubali yaishe, aendelee na maisha yake, manake akisema anamcontrol, huyo ni yule anayemhisi/kumjua......na ambao hawajui anawajua?
 

Aksante kaizer
 
Hapo huyo jamaa tayari kammega huyo dada, hapo ni busara ndogo tu inahitajika kujua hilo.
 
Aksante Ama nitafanya kama ulivyonishauri. Hivi inawezekana jamaa (shem) anamega ?? Maana mbona kareact kihivyo??

Mwanajamii1,

Inaezekana jama hafanyi hivyo,ila unaweza kuta huyo jamaa anakuawaga tu na mood swings.Unaezakuta hata jamaa hajawahi kufikiria kufanya hivyo+mood swings anajikuta anakasirika

Pia,inaezekana jamaa huwa anamdharau sana huyo dada kutokana na tabia zake chafu ,so inapotokea mke wake kuonyesha dalili za kumhisi vibaya basi kaona amedharauliwa
 
Aksante Ben inawezekana ni wasiwasi tu but hii reaction ndo imeshangaza na mpaka sasa Mr hajajisikia kusema lolote juu ya hili ah amekaa kimya kama maji ya mtungini
 
Namshauri ajishushe aombe msamaha na amuulize in other ways- kwa upendo not in kimitego! kisa cha yeye kureact kwa upendo; na huko ndio atapata majibu ikiwa jamaa ataendelea kufront poor defences; Hapo naungana na wote wanaoshauri ajiandae kuchukua hatua ngumu; mojawapo ni kwenda kupima bila kumshirikisha mwenzie na ikiwezekana kumlazimisha kupima ikiwa yeye atakuwa salama!
 
Ninadhani ndoa hiyo ina migogoro ya muda mrefu kiasi kwamba mume amekuwa sensitive sana na maswali ya jinsi hiyo. So ili kujilinda, inabidi aporomoshe matusi ili maswali yasiendelee.

Kuna polite way ya kuuliza maswali sensitive, inaonekana muulizaji hakutumia polite language. Mhusika akiulizwa swali kishari shari anaweza kujibu ama kwa mkato au akaporomosha matusi. Kwenye mahusiano/ndoa unapouliza maswali ya kishari/kipolisi au kama ya kitimoto, always huwa hayaishii pazuri. Mara nyingi huwa inaongeza tension hasa kama mahusiano/ndoa hiyo ina historia ya kutuhumiana/kutoaaminiana.

Nina refer majibu ya mhusika, "mimi si malaya/mhuni wa kutembea na KILA CHANGU". So inaonyesha alishatuhumiwa/fumaniwa/shikwa akitoka nje ya ndoa.

Kwa hiyo kuuliza maswali sensitive sometimes kunahitaji hekima ya kutosha, kuangalia mazingira na trend ya mahusiano/ndoa. Suppose watu wametoka kugombana asubuhi hiyo ama jana yake usiku mke alimnyima mume wake, au mume alichelewa kurudi nyumbani unategemea jamaa akikumbana na swali kama hilo hataacha kutoa matusi? Maana wengi wetu kabla ya kujibu maswali ya jinsi hiyo lazima huwa tunajiuliza, kwanini kaniuliza? Ndipo kwa haraka mtu anaweza kuunganisha dots ambazo zinaweza kuwa sahihi ama siyo sahihi, matokeo yake ni kuporomosha matusi ama majibu ya mkato.

Ni ngumu kumhukumu huyo mwanaume kama anammega huyo dada au la, kwa kuwa tu ameporomosha matusi. Kwa maoni yangu, ninahisi kuna mengine ya ziada ambayo wachangiaji na MJ1 hatuyajui. More details plz!
 

...hovyo kabisa, ndio hawa wanaotufanya sote tuonekane tuna IQ ndogo 😀
 

...swadaktaaa...

tena kuna wale wengine ukijibu ndio au hapana unazidi kujichimbia kaburi...
 
It beats me!
Hivi kwenye ndoa huu ndio utaratibu wa kuonyesha kutoridhika, wa kukwepesha usiyotaka? Kwani ukijibu kistaarabu bila kutoa/kuporomosha matusi hutasikika?

Nadhani taasisi ya ndoa kwa siku hizi leaves much to be desired!Nadhani there is something fundamentally wrong somewhere kama wanandoa - baba na mama wenye dhamana ya kulea na kukuza kizazi kijacho wana tabia za namna hii.

Hivi heshima bado itakuwepo? Nashindwa kuelewa inakuwaje endapo mke naye atatumia defence mechanism ya matusi - ndoa zingesimama?
Samahani kuuliza maswali mengi badala ya majibu.
 

Ah dada hawa wenzetu ni wafanye wao, ukifanya wewe ndoa imekushinda. Najaribu tu kufikiria mimi ambaye mume wangu kila siku ni kunihisi vibaya yaani ukitoka -umekwenda kuwaona mabwana zako, ukijifungia ndani unawasiliana nao kwenye simu lakini bado nikiulizwa wamjua flani najibu politely siku nikijibu kwa mitusi kama alivyojibiwa shoga angu sijui itakuwaje ! Mi wananichosha jamani, mnanichosha kweli
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…