MALCOM LUMUMBA
JF-Expert Member
- Jul 26, 2012
- 21,750
- 71,628
Nimelizungumzia hili kwenye uzi wangu namba #13 kwamba Katiba inasema Mawaziri wote nchini hufanya kazi kwa matakwa ya Raisi (At the Pleasure of the President). Hivyo baraza hili linafanya kazi kutokana na kiapo cha walichoapa mbele ya Raisi Magufuli, hivyo yeye akiwa hayupo basi ni lazima waape tena kwa Raisi mpya ambaye watafanya kazi kufuata matakwa yake (At her pleasure).Kwa hiyo mkuu hapo unaonaje.
Katiba imefuatwa au haijafuatwa?
Nakubali mimi sina ufahamu kwenye maswala ya kisheria.
Kisheria, hili ni tukio la aina yake kuwahi tokea tangu kuzaliwa kwa Jamhuri: Hivyo Katiba iko kimya juu ya utaratibu ambao ungepaswa kufuatwa kuhusu mustakabali wa Baraza la Mawaziri. TLS walichofanya ni kutoa maoni yao kisomi wakitimiza majukumu yao kisheria ya kuishauri serikali (Hivyo sioni kosa lolote lile) kwasababu sheria iko kimya. Lakini wengine wanaweza kusema Baraza litaendelea kuwepo, kitu ambacho kipo kwenye maamuzi na mamlaka ya Raisi mpya (Within the discretionary power of the new President): Hivyo hata hili kundi nalo linaweza kuwa sahihi kwasababu sheria iko kimya juu ya huu utaratibu. Wengine wanaweza kuiga kanuni na utaratibu wa nchi za nje, hili nalo ni sawa lakini (It's not binding).
Japo, kitu ambacho nina uhakika ni kwamba Baraza la Mawaziri ni lazima liape kiapo kipya cha utii kwa Raisi mpya, kwasababu watafanya kazi kufuatana matakwa yake: Angeamua kuwarudisha wote nyumbani na kusema naanza upya nalo ni sawa kwasababu Tanzania tuna Uraisi wa Kifalme (Imperial Presidency).
Kitu ambacho mimi nakereka ni hichi kitabia cha BUSH-LAWYERS na WANAHARAKATI kujifanya wao ndiyo watafasiri wa Katiba na kuanza kupinga kila kitu bila kuleta hoja zenye mantiki kisheria. Hawajaridhika waende Mahakama Kuu wafungue kesi ya Kikatiba kuomba tafasiri, maana kile ndiyo chombo cha mamlaka ya mwisho kuhusu kutafasiri katiba na siyo hizi blah, blah, blah za hapa mitandaoni.