Ina maana Katiba haijafuatwa?

Ina maana Katiba haijafuatwa?

Nyani Ngabu

Platinum Member
Joined
May 15, 2006
Posts
97,119
Reaction score
136,866
Mimi ni mtu ninayefuata falsafa ya ‘keep it simple’.

Sikuona sababu yoyote ile ya Rais Samia kulivunja baraza lote la mawaziri na kulisuka upya.

Mabadiliko madogo kama aliyoyafanya ni ya kawaida na niliyategemea.

Lakini tuliambiwa na watu mbalimbali kuwa eti baada ya Rais Magufuli kufariki, basi kwa mujibu wa katiba baraza nalo linavunjika na waziri mkuu anakoma kuwa waziri mkuu.

Nilipovisoma hivyo vifungu vya katiba walivyokuwa wanavitumia hao watu kusema kuwa baraza zima lazima livunjwe, sikushawishika hata kidogo.

Huu ni mwendelezo wa serikali ileile aliyoiacha Rais Magufuli.

Mambo ya kuvunja baraza zima ya nini? Just keep it simple na kazi ziendelee. Tweaks za hapa na pale, hizo ni sawa.

Sasa, mbona waziri mkuu anaendelea tu na nafasi yake? Hajateuliwa upya kama walivyokuwa wanadai hao wataalamu wa sheria. Hajaapa tena. Au ameapa upya?

Je, ina maana Mama Samia kaanza utawala wake kwa kuvunja katiba?
 
TLS walipotoka, kwa bahati mbaya kabisa wafuasi na chadema wakalibeba Kama ilivyo wakatoa waraka kupitia katibu mkuu kuwa mama Samia anatakiwa kulivunja baraza la mawaziri
Nakumbuka siku ile humu makamanda yalijitoa akili, Ila Sasa hivi yapo kimya hata hayazungumzii tena kuvunjwa Baraza.
 
O
TLS walipotoka, kwa bahati mbaya kabisa wafuasi na chadema wakalibeba Kama ilivyo wakatoa waraka kupitia katibu mkuu kuwa mama Samia anatakiwa kulivunja baraza la mawaziri
Nakumbuka siku ile humu makamanda yalijitoa akili, Ila Sasa hivi yapo kimya hata hayazungumzii tena kuvunjwa Baraza.
wamejikausha utadhani hawakutoa waraka!
 
Mimi ni mtu ninayefuata falsafa ya ‘keep it simple’.

Sikuona sababu yoyote ile ya Rais Samia kulivunja baraza lote la mawaziri na kulisuka upya.

Mabadiliko madogo kama aliyoyafanya ni ya kawaida na niliyategemea.

Lakini tuliambiwa na watu mbalimbali kuwa eti baada ya Rais Magufuli kufariki, basi kwa mujibu wa katiba baraza nalo linavunjika na waziri mkuu anakoma kuwa waziri mkuu.

Nilipovisoma hivyo vifungu vya katiba walivyokuwa wanavitumia hao watu kusema kuwa baraza zima lazima livunjwe, sikushawishika hata kidogo.

Huu ni mwendelezo wa serikali ileile aliyoiacha Rais Magufuli.

Mambo ya kuvunja baraza zima ya nini? Just keep it simple na kazi ziendelee. Tweaks za hapa na pale, hizo ni sawa.

Sasa, mbona waziri mkuu anaendelea tu na nafasi yake? Hajateuliwa upya kama walivyokuwa wanadai hao wataalamu wa sheria. Hajaapa tena. Au ameapa upya?

Je, ina maana Mama Samia kaanza utawala wake kwa kuvunja katiba?


Anaogopa kuvunja baraza la mtangulizi wake
 
TLS walipotoka, kwa bahati mbaya kabisa wafuasi na chadema wakalibeba Kama ilivyo wakatoa waraka kupitia katibu mkuu kuwa mama Samia anatakiwa kulivunja baraza la mawaziri
Nakumbuka siku ile humu makamanda yalijitoa akili, Ila Sasa hivi yapo kimya hata hayazungumzii tena kuvunjwa Baraza.
Katiba ndio ina mkanganyiko

Ibara ya 51(2), ina mtaka Rais mara baada ya kushika madaraka kumteua PM.

Sasa haijaeleza je kama Rais ameshika Madaraka baada ya Rais aliyepita kufariki.
Inakuwaje.

Katiba ndio ina mkanganyiko.
 
TLS walipotoka kisheria. Kimsingi halazamiki kuvunja Cabinet/kuteua PM. Ni discretion yake.
Hii tweak aliyoifanya, nadhani ni kuweka heshima na utii kwa Surbodinates wake.. 'hey im your boss now, i can fire you anytime i wish!'.
in Tanzania Ministers work at the Pleasure of the President to whom they swore an oath. When the incumbent dies, resigns or becomes incapable of fulfilling his duties, then they are automatically released from their oath. Some like TLS would argue that with Imperial President gone, the cabinet automatically dissolves. Now at the Pleasure of the President, Ministers would again have to swear an oath of fidelity and allegiance.

This is a new experience for the republic and the law is silent on procedures, so everything is left at the discretion of the President. So Tanganyika Law Society was right in light of their opinion, based on Constitutional Principles and Practice from another jurisdiction. Take an example in Republic like America, especially after the death of F.D.Roosevelt: President Truman had a discretion to appoint a new Government ASAP, or continue with the current Government left by his predecessor. He told Secretaries/Ministers to remain in their posts, meanwhile he was figuring out other options.

Remember, one of the basic feature of CURT 1977 is Imperial Presidency with all Ministers working at the Pleasure of the President.
 
TLs cha mtoto kuna watu walitafutia kiki kwa kuita press na leo wameita nyingine!
 
Katiba ndio ina mkanganyiko

Ibara ya 51(2), ina mtaka Rais mara baada ya kushika madaraka kumteua PM.

Sasa haijaeleza je kama Rais ameshika Madaraka baada ya Rais aliyepita kufariki.
Inakuwaje.

Katiba ndio ina mkanganyiko.
Katika haina mkanganyiko, nadhani wewe ndiyo unapata shida kuilewa. Halafu mwenye mamlaka ya kutafasiri vifungu vya sheria hapa nchini ni Mahakama Kuu na siyo kila mwananchi (Laymen). Ukisoma sayansi ya Sheria ya Katiba na Utawala (Constitutional & Administrative Law) utafahamu kwamba kuna jinsi ya kusoma na kutafasiri Katiba, kazi ambayo siyo kila mtu anaweza kufanya. Makamana huangalia vitu kama;
  • The Rule of Congruence,
  • The Rule of Consistency,
  • The Rule of Context,
  • Intention of the Parliament,
  • The Principle of Lex Specialis,
Hili tukioa ambalo wewe unalizungumzia hapa limetokea kwenye Context ipi, na sheria zake zikoje ??? Maana hiyo Ibara ya 51(2) ya Katiba inazungumzia Muktadha wa kutoka kwenye Uchaguzi Mkuu. Sasa tungeanza kujiuliza swali la msingi kabisa: Je, hichi kifungu (Ibara ya 51(2) kinatumika hata ambapo Raisi kajiuzulu, Kafariki, Katolewa na Bunge au Ameshindwa kutimiza majukumu yake. (Nadhani hili ndilo swali la msingi kabisa)

Sasa nadhani mnavyosema kwamba katika ina mkanganyiko nadhani mnakuwa na shida pahala: Hujaridhika na kilichofanyika nenda Mahakama Kuu kafungue kesi ya kikatiba kuomba tafasiri ya vifungu vya Katiba. Nadhani ifike mahali kazi ya sheria tuwaachie waliosomea, na kama tunataka kuwapinga basi tusilete maneno matupu bali sababu za kitaalamu ambazo zinaeleweka.
 
Katika haina mkanganyiko, nadhani wewe ndiyo unapata shida kuilewe. Halafu mwenye mamlaka ya kutafasiri vifungu vya sheria hapa nchini ni Mahakama Kuu na siyo kila mwananchi (Laymen). Ukisoma sayansi ya Sheria ya Katiba na Utawala (Constitutional & Administrative Law) utafahamu kwamba kuna jinsi ya kusoma na kutafasiri Katiba, kazi ambayo siyo kila mtu anaweza kufanya. Makamana huangalia vitu kama;
  • The Rule of Congruence,
  • The Rule of Consistency,
  • The Rule of Consistency,
  • Intention of the Parliament,
  • The Principle of Lex Specialis,
Sasa nadhani mnavyosema kwamba katika ina mkanganyiko nadhani mnakuwa na shida pahala: Hujaridhika na kilichofanyika nenda Mahakama Kuu kafungue kesi ya kikatiba kuomba tafasiri ya vifungu vya Katiba. Nadhani ifike mahali kazi ya sheria tuwaachie waliosomea, na kama tunataka kuwapinga basi tusilete maneno matupu bali sababu za kitaalamu ambazo zinaeleweka.
Kwa hiyo mkuu hapo unaonaje.

Katiba imefuatwa au haijafuatwa?

Nakubali mimi sina ufahamu kwenye maswala ya kisheria.
 
Hii kitu ingekuwa simple kama PM angejiuzulu, sasa PM kakomaa na mama anaonekana mwenye huruma ndio maana kaamua kuacha mambo yaendelee.
 
Back
Top Bottom