Ms Judith
JF-Expert Member
- Dec 24, 2010
- 2,563
- 918
Kila kifo Gongo la Mboto fidia Sh.8.5m
Na Muhibu Said
3rd March 2011
Kila aliyekufa kutokana na milipuko ya mabomu ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), Serikali italipa fidia ya Sh. milioni 8.5.
Taarifa hiyo ilitolewa jana na Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Meck Sadiki, ambaye ilizitaka familia 29 zilizofiwa na ndugu kutokana na mabomu hayo kuteua msimamizi wa mirathi ya marehemu, kwani iko tayari sasa kuilipa kila familia Sh. milioni 8.5 kama kifuta machozi.
Agizo hilo lilitolewa na Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Saidi Meck Sadiki, alipozungumza na waandishi wa habari katika kituo cha kupokelea misaada kwa waathirika cha Kamati ya Maafa ya Mkoa jana.
Alisema kwa sasa kinachotakiwa kufanywa na familia za marehemu, ni kufungua mirathi mahakamani ili kumteua haraka msimamizi wa mirathi, ambaye ndiye atakayelipwa fedha hizo kwa niaba ya warithi.
Sadiki alisema utaratibu huo ndio unaostahili kufuatwa, kwani utasaidia kuepusha migogoro inayoweza kujitokeza ndani ya familia iwapo fedha hizo zitatolewa kiholela.
Alisema hadi kufikia jana, watu waliothibitika kufariki dunia kutokana tukio hilo, ni 29 akiwamo aliyefia nyumbani Kinyerezi wiki iliyopita na mwingine aliyefia katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) juzi.
source: :: IPPMEDIA
Na Muhibu Said
3rd March 2011
Kila aliyekufa kutokana na milipuko ya mabomu ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), Serikali italipa fidia ya Sh. milioni 8.5.
Taarifa hiyo ilitolewa jana na Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Meck Sadiki, ambaye ilizitaka familia 29 zilizofiwa na ndugu kutokana na mabomu hayo kuteua msimamizi wa mirathi ya marehemu, kwani iko tayari sasa kuilipa kila familia Sh. milioni 8.5 kama kifuta machozi.
Agizo hilo lilitolewa na Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Saidi Meck Sadiki, alipozungumza na waandishi wa habari katika kituo cha kupokelea misaada kwa waathirika cha Kamati ya Maafa ya Mkoa jana.
Alisema kwa sasa kinachotakiwa kufanywa na familia za marehemu, ni kufungua mirathi mahakamani ili kumteua haraka msimamizi wa mirathi, ambaye ndiye atakayelipwa fedha hizo kwa niaba ya warithi.
Sadiki alisema utaratibu huo ndio unaostahili kufuatwa, kwani utasaidia kuepusha migogoro inayoweza kujitokeza ndani ya familia iwapo fedha hizo zitatolewa kiholela.
Alisema hadi kufikia jana, watu waliothibitika kufariki dunia kutokana tukio hilo, ni 29 akiwamo aliyefia nyumbani Kinyerezi wiki iliyopita na mwingine aliyefia katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) juzi.
source: :: IPPMEDIA