Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 34,239
- 44,476
Tunayakosa maoni yenu na mawazo yenu; nikiangalia maoni yanayotolewa mara kwa mara na wale ambao tumo humu siku nyingi ni wazi kuwa sehemu kubwa ya watumiaji hawajajiunga na ni watazamaji tu.
Kwa maneno mengine, yawezekana wanawakilisha kundi kubwa la Watanzania ambao wamechagua kuangalia toka mbali tu kile kinachofanyika; watu ambao wanaweza kuwa wanalalamika sana pembeni lakini wakipewa nafasi ya kutoa maoni huchagua ukimya kuliko kutoa maoni yao ambayo yanaweza kukosolewa, kupingwa, au kuungwa mkono au hata kusababisha malumbano.
Kwenye wanachama zaidi ya elfu 16, yawezekana siyo zaidi ya watu 100 wanaotoa maoni yao mara kwa mara na labda ni kikundi cha watu 50 tu kinachotoa mwelekeo wa maoni hapa. Hili siyo jambo zuri.
Najua kwa kutoa maoni yenu au kujiunga moja kwa moja wengine mnahatarisha hadhi na majina yenu na hata nafasi zenu. Na hasa labda wakati mwingine mnakwazika kwani baadhi yetu humu hatuchelewi kuwashambulia mara moja bila kuwapa nafasi ya kujizoesha au hofu ya kuwa unaweza kusema kitu kika kugive away.
Ushauri wangu ni kuwa yawapa mkivuke hicho kizingiti cha hofu (threshold of fear) na hatimaye nanyi mtoa mawazo yenu kuchangia. Binafsi nitakaa pembeni na mimi kuwa msomaji wiki hii (isipokuwa kama kuna ulazima kweli wa kuvunja ukimya huo) ili kuwapisha wanachama wapya nao watoe michango yao.
So.. inatosha kusoma.. jiunge... changia!!!
Kwa maneno mengine, yawezekana wanawakilisha kundi kubwa la Watanzania ambao wamechagua kuangalia toka mbali tu kile kinachofanyika; watu ambao wanaweza kuwa wanalalamika sana pembeni lakini wakipewa nafasi ya kutoa maoni huchagua ukimya kuliko kutoa maoni yao ambayo yanaweza kukosolewa, kupingwa, au kuungwa mkono au hata kusababisha malumbano.
Kwenye wanachama zaidi ya elfu 16, yawezekana siyo zaidi ya watu 100 wanaotoa maoni yao mara kwa mara na labda ni kikundi cha watu 50 tu kinachotoa mwelekeo wa maoni hapa. Hili siyo jambo zuri.
Najua kwa kutoa maoni yenu au kujiunga moja kwa moja wengine mnahatarisha hadhi na majina yenu na hata nafasi zenu. Na hasa labda wakati mwingine mnakwazika kwani baadhi yetu humu hatuchelewi kuwashambulia mara moja bila kuwapa nafasi ya kujizoesha au hofu ya kuwa unaweza kusema kitu kika kugive away.
Ushauri wangu ni kuwa yawapa mkivuke hicho kizingiti cha hofu (threshold of fear) na hatimaye nanyi mtoa mawazo yenu kuchangia. Binafsi nitakaa pembeni na mimi kuwa msomaji wiki hii (isipokuwa kama kuna ulazima kweli wa kuvunja ukimya huo) ili kuwapisha wanachama wapya nao watoe michango yao.
So.. inatosha kusoma.. jiunge... changia!!!