kiss ov love
JF-Expert Member
- Jan 21, 2025
- 9,363
- 16,092
Sijui ni lini na mimi ntakuwa na furaha maishani, Furaha yangu ilitoweka pasipo kujua baada ya kumpoteza mama yangu miaka mingi iliyopita nikiwa bado mdogo sana.
Maisha niliyopitia kutoka kwa ndugu, mama wa kambo pamoja na baba asiyejali yananipa hasira sana, sijui hata nimlaumu nani kuzaliwa kwenye hii familia, huu ukoo na huyu mzazi ambaye hakutaka kabisa kusimamia nafasi yake na kutimiza majukumu yake ya malezi ipasavyo kwetu sisi watoto wake.
Natamani kama kungekuwa kuna Dunia nyingine ambayo haitakuwa na binadamu niende nikaishi huko nipotelee nisionekane na mtu yoyote kila mtu asahau kuhusu mimi.
R.I.P mom ulikuwa mpambanaji ukahakikisha kaka amesoma na amemaliza chuo kupitia ujasiriamali wako mdogo mdogo uliokuwa ukifanya, matokeo yake huyu kaka uliyempambania leo hii hakumbuki wadogo zake ametuacha tuteseke peke yetu, hata leo hii simu zake hazipatikani amekuwa addicted na pombe hadi anashindwa kufanya kazi yake kwa ufanisi.
Pengine ungekuwepo mom nisingepita nilikopita ungenifundisha vingi vizuri na imani pia ungenipambania, wala usingeniacha niteseke kama alivyofanya baba. Nasikitika sana kwanini umeondoka nikiwa bado mdogo, bado nakuhitaji mama yangu😭😭
Kwanini Mungu ameruhusu hili litokee kwangu, kuna muda huwa najiuliza hivi Mungu huwa anaona mateso na matatizo yetu tunayopitia sisi wanadamu, huwa namlaumu sana Mungu kuniondolea mama yangu kipenzi nikiwa mdogo, namlaumu pia kuruhusu mateso yawe sehemu ya maisha yangu, kunipa baba asiyejali watoto wake.
Ninahisi kumchukia baba yangu, hata akinipigia simu sifurahii kabisa, hata kwenda kumsalimia hadi anikumbushe au tu hiyo siku nijisikie mwenyewe. Lakini nimemsamehe kwa yote aliyoyafanya maishani mwangu japo moyoni mwangu naumia sana kila nikiyafikiria maisha yangu yaliyopita.
Natamani hata wakati ule mama yangu angebaki ningetanguliaga mimi, najitahidi kuwa na furaha lakini nikikaa mwenyewe furaha yote inatoweka.
Nawezaje kuondokana na haya maumivu yaliombatana na chuki kwa ndugu zangu?
Maisha niliyopitia kutoka kwa ndugu, mama wa kambo pamoja na baba asiyejali yananipa hasira sana, sijui hata nimlaumu nani kuzaliwa kwenye hii familia, huu ukoo na huyu mzazi ambaye hakutaka kabisa kusimamia nafasi yake na kutimiza majukumu yake ya malezi ipasavyo kwetu sisi watoto wake.
Natamani kama kungekuwa kuna Dunia nyingine ambayo haitakuwa na binadamu niende nikaishi huko nipotelee nisionekane na mtu yoyote kila mtu asahau kuhusu mimi.
R.I.P mom ulikuwa mpambanaji ukahakikisha kaka amesoma na amemaliza chuo kupitia ujasiriamali wako mdogo mdogo uliokuwa ukifanya, matokeo yake huyu kaka uliyempambania leo hii hakumbuki wadogo zake ametuacha tuteseke peke yetu, hata leo hii simu zake hazipatikani amekuwa addicted na pombe hadi anashindwa kufanya kazi yake kwa ufanisi.
Pengine ungekuwepo mom nisingepita nilikopita ungenifundisha vingi vizuri na imani pia ungenipambania, wala usingeniacha niteseke kama alivyofanya baba. Nasikitika sana kwanini umeondoka nikiwa bado mdogo, bado nakuhitaji mama yangu😭😭
Kwanini Mungu ameruhusu hili litokee kwangu, kuna muda huwa najiuliza hivi Mungu huwa anaona mateso na matatizo yetu tunayopitia sisi wanadamu, huwa namlaumu sana Mungu kuniondolea mama yangu kipenzi nikiwa mdogo, namlaumu pia kuruhusu mateso yawe sehemu ya maisha yangu, kunipa baba asiyejali watoto wake.
Ninahisi kumchukia baba yangu, hata akinipigia simu sifurahii kabisa, hata kwenda kumsalimia hadi anikumbushe au tu hiyo siku nijisikie mwenyewe. Lakini nimemsamehe kwa yote aliyoyafanya maishani mwangu japo moyoni mwangu naumia sana kila nikiyafikiria maisha yangu yaliyopita.
Natamani hata wakati ule mama yangu angebaki ningetanguliaga mimi, najitahidi kuwa na furaha lakini nikikaa mwenyewe furaha yote inatoweka.
Nawezaje kuondokana na haya maumivu yaliombatana na chuki kwa ndugu zangu?