wa stendi
JF-Expert Member
- Jul 7, 2016
- 24,688
- 26,796
Sababu sio hiyokwani hamjui kuna trafiki light mbele?
Sababu sio hiyokwani hamjui kuna trafiki light mbele?
Kuanzia stopover hadi mbezi hakuna vituo vya mwendokasi vinavyolingana na namna mabasi yalivyo.Kwanini hawa mwendokasi wasiwe na route ya moja kwa moja kutoka mbezi mpk Kivukoni wakaachana na kuwashusha pale korogwe huu iendeshaji wa mwendokasi unabidi ujitathimini kbs
Nitashukuru sanaSerikali ya sasa ni sikivu mno hilo swala litafanyiwa kazi.
Yaa ni kweli kabisa kule mwanzoni ile servise road kushoto ilikuwa inatumika daladala zinaingia kwa sasa nashangaa kunapoaki tax na soko hapo hapo ni bora wangefanya hapo kituo kidogo kama kile cha kimara mwisho daladala ziwe zinaingia zinaenda kutokea kule mbele risotiiiiTatizo nikituo cha Daladala pale Kimara Korogwe ndio sababu kubwa
Nafasi ndogo then kunanjia ile inayotoka Kule kilungure na hapohapo kunakivuko kikubwa cha waende kwa miguu na soko pembeni
Hiyo ni bottleneck effect. Bahati mbaya engineers wetu hawakuiona. Hata shekilango asubuhi ni balaa.
Chini ya mh Rais magu hili linawezekana kabisa kabisa na naamini hiloAwamu Hii Ya Tano
Itaondoa Foleni Hayo Maeneo
Ishu sio huko hata tatizo kubwa ni hapa nilipozungumzia ni marekebisho madogo tuuUpanuzi wa bara bara ya Kimara - Kibaha ukikamilika, adha hiyo itapungua.
sawa mtaalamSababu sio hiyo
Vp kutajengwa fly overAwamu Hii Ya Tano
Itaondoa Foleni Hayo Maeneo
Baada ya barabara ya juu Ubungo flyover kuanza kutumika na kumaliza kabisa kabisa ule usumbufu wa foleni barabara ya morogoro sasa imekuwa kero kuanzia kiande cha rombo hadi kimara korogwe
Yaani kutoka Rombo hadi ufike Korogwe tuu ni masaa zaidi 2. chanzo cha foleni hakijulikani na ma trafic wako korogwe kituoni wanavuta magari tuu lakini foleni haiishi.
Uchunguzi niliofanya kwa haraka haraka tangu barabara ya Korogwe kituoni pale kushoto (ya kuelekea maji chumvi )ikamilike kiwekw lmi na kuanza kutumika ndio inachangia maana magari ni mengi sana yanaingilia pale na kutokea
Ombi/ushauri wangu:
Kama kuna uwezekano kuanzia kituo cha mewndo kasi bucher kushoto kama inaelekea kimara kuwekwe alama ya kuongozea magari ambayo yanaingia tu maji chumvi na pale pale mwanzo wa barabara ya kuwekwe alama ya katazo la kuingia barabara kuu ila servise road ile ya zamani kushoto mwa kituo cha daladala korogwe itengenezwe magari yanayotoka majichumvi kuingia barabara kuu yaingilie hapo yakatokezee kule mbele (risot)hii inaweza saidia kupunguza foleni maana imekuwa kero sana kwa abiria wanaishi mbezi.
Karibuni kwa ushauri zaidi.
... tatizo linachangiwa pakubwa na wingi wa zebra crossings kutoka na kuingia vituo vya mwendokasi; kila baada ya mita chache zebra! Zebra za kituo cha Korogwe zinasababisha foleni hadi Rombo (jioni) na foleni hadi Stop Over (asubuhi) ni tatizo kubwa! Maeneo ya kati ya Ubungo na Magomeni ni foleni ndefu pande zote za barabara kutokana na wingi wa zebra za kutoka na kuingia vituo vya mwendo kasi (mwanzo na mwisho wa kituo!).
Kutoka na kuingia vituoni ilitakiwa iwe ama kupitia tunnels au madaraja kama ilivyo pale Kimara ili kuruhusu magari ya kawaida kutosimama kila baada ya mwendo mfupi. Hali iliyopo sasa hivi kuendesha gari Morogoro Rd. ni adha kubwa sana.
... na ile kona isiyo na sababu pale mara baada ya Kituo cha Kimara; sijiu kwani waliweka mkunjo/kona pale hali inayofanya ipite gari moja tu at a time! Pangekuwa pamenyooka gari zingepita mbili na kwa speed hivyo kuondoa foleni ambayo wakati mwingine inafika hadi Korogwe.Tatizo barabara kutoka ubungo hadi kimara ni nyembamba na haijapanuliniwa tofauti na kuanzia kimara stop over na kuendelea ambapo barabara ni pana ... pia kituo cha mwendokas kimara korogwe kinachangia pia
Itapunguz a maana mengi yatakuwa hayapo speed sana kuna zebra paleSasa hapo resort yataingiaje barabarani? bado ni yale yale tu..
Mi nafikir wajenge kituo cha daladala na bajaji pale korogwe na sio kusimama barabarani..