Ilikuwa nife jioni hii ya leo!!!

Ilikuwa nife jioni hii ya leo!!!

Pole yangu ni kwa huyo mtoto na sio wewe baba mtukutu!! Unaomba ushauri kwa wajenzi ulitarajia wakuambie nini kama sio "kula kona?!" Nawe ukafanya hivyo bila kukumbuka kwamba upo na mtoto mdogo ndani!! Did you really expect polisi wangekuachia hata baada ya kukuona unawakimbia kwa kasi kubwa hivyo?! Kama ulitarajia wangekuachia, kulikuwa na umuhimu gani basi wa polisi kuwa na road patrol kwa kutumia magari... wanafahamu, wahalifu watawakimbia tu kwahiyo na wao wapo standby kumtoa nduki yeyote!

Umesema upo barabarani kwa muda mrefu! Hebu rejea umefanya matukio kama hilo au yanayofanana na hilo mangapi! Ikiwa ni tukio lako la kwanza, nitajilazimisha kukuelewa lakini kama umeshawahi kufanya kitu kama hicho huko nyuma, basi ningekushauri usiwe unatembea na mtoto unless kama una sababu za msingi za kufanya hivyo. Hapo ulihatarisha sana maisha ya mtoto bila sababu za msingi. Ukaingia mitaani... huko nako kuna watoto; aaaaargh!!
 
Naukubali upumbavu wangu.....na sijalalamika popote kuwa nimeonelewa bali nimeleta mkasa ili iwe funzo kwa wengine haswa nikizingatia kuwa ni wengi wenye kufanya hivi hadi wenye pikipiki.

Wanausalama walikuwa sawa kabisa na walijiridhisha kuwa sina kibaya chochote na wakaniachia.
Yaah tumejifunza boss huwa kuna makosa makubwa zaidi ya hayo mie gari yangu nilichelewesha kulipia vibali vyote na nikasafiri nayo btn Mbeya na Dar kama mara tatu hivi mwaka huu lakini sikuwahi kufikiria kuwakimbia wazee wa kazi, hawa jamaa ni washkaji zetu ukizungumza nao kwamba nitarekebisha mbona wanaelewa!!
 
Pole yangu ni kwa huyo mtoto na sio wewe baba mtukutu!! Unaomba ushauri kwa wajenzi ulitarajia wakuambie nini kama sio "kula kona?!" Nawe ukafanya hivyo bila kukumbuka kwamba upo na mtoto mdogo ndani!! Did you really expect polisi wangekuachia hata baada ya kukuona unawakimbia kwa kasi kubwa hivyo?! Kama ulitarajia wangekuachia, kulikuwa na umuhimu gani basi wa polisi kuwa na road patrol kwa kutumia magari... wanafahamu, wahalifu watawakimbia tu kwahiyo na wao wapo standby kumtoa nduki yeyote!

Umesema upo barabarani kwa muda mrefu! Hebu rejea umefanya matukio kama hilo au yanayofanana na hilo mangapi! Ikiwa ni tukio lako la kwanza, nitajilazimisha kukuelewa lakini kama umeshawahi kufanya kitu kama hicho huko nyuma, basi ningekushauri usiwe unatembea na mtoto unless kama una sababu za msingi za kufanya hivyo. Hapo ulihatarisha sana maisha ya mtoto bila sababu za msingi. Ukaingia mitaani... huko nako kuna watoto; aaaaargh!!
Kutokea tukio kama hili ni mara ya kwanza kabisa.....kumbuka mkuu ndege mjanja hunaswa na tundu bovu.
 
Yaah tumejifunza boss huwa kuna makosa makubwa zaidi ya hayo mie gari yangu nilichelewesha kulipia vibali vyote na nikasafiri nayo btn Mbeya na Dar kama mara tatu hivi mwaka huu lakini sikuwahi kufikiria kuwakimbia wazee wa kazi, hawa jamaa ni washkaji zetu ukizungumza nao kwamba nitarekebisha mbona wanaelewa!!
Umeniongezea kitu kichwani.....mimi huwa nafanya hivyo nikiwa na gari ya kazi pekee lakini leo yamenikuta.
 
Pole mkuu zaidi namwonea mtoto wako huruma kwa kushuhudia mtu anaemwamini zaidi duniani akipigwa na kusemewa hovyo.
 
Usirudie tena kuwakimbia askari kwani kufanya hivyo unaweza kusababisha mengine kabisa (kama yaliyokukuta). Ungeweza hata kugonga mtu/watu, mnyama au ajali ya kipuuzi ukapata hasara kubwa. Simama umalizane nao tu. Wengi wa askari wetu (kama walivyo Watanzania wengi) usipowaprovoke wako poa sana tu, hata ungekua na makosa mia wanaweza kukuachia. Labda uwaonyeshe dharau, kiburi, ubabe, nk.

Nimekua nikitumia gari bovu sana labda kuliko yote Moshi mjini miaka ya 2000 hadi nikafahamiana na askari ila sijawahi hata siku moja kuwakimbia askari. Wengi wako friendly kama utajishusha, kuwaheshimu na mara chache kuwatoa (posho ya kubrashia viatu)
 
ungeua watoto hao wasiokuwa na hatia yoyote kwa ufala wako
Ufala pia unakwenda na ahadi ikifika au jambo likipangwa.....na yote kwa yote hakuna anaependa kifo na hata uwe makini vipi likipangwa kukukuta basi huna mbadala, umeshawahi kusikia msemo wa mganga hajigangi? Siku ya kufa nyani miti huteleza? Hakuna ajuae kesho? Kifo hakina dawa? Ndege mjanja hunaswa na tundu bovu? Ni nani ambae hakupata matatizo au kuishi tangu enzi ya nabii Nuhu mpaka leo sababu hakuwa fala? Mwenzako akipata mtihani mshukuru Mungu kwa sababu haukuupata wewe.
 
Uzi wako umetoa elim kwa watu wenye rabia za kuwakimbia askari.
Nilishawahi kuona huo mchezo bagamoyo kipindi cha nyuma kidogo enzi za TZR au black mamba(wale wa dar es salaam watanielewa)
Jamaa kapigwa mkono na traffic akawakimbia,kilichotokea ikaingia deffender barabarani ikaanza kuranda nae jamaa akaws anawazunfusha mtaani tu bagamoyo.
Wakat wanazungushana kumbe askar wanawasiliana na wenzao ,baada ya muda jamaa akajikuta amekuwa blocked.
Kilichotokea hapo ni historia
 
Duuuh.. poleeee, ila nimechekaaaa... poleee bana... usichukie lkn.. nimecheka sana... atleast umepata akili kidogo, polisi ni nani.. haaaaa
Una haki ya kucheka maana halijakukuta.....ila nashukuru nalala nyumbani badala ya korokoroni japo nimeshaanza kuhisi homa kwa mbali.
 
Pole sana mkuu, kweli JF kiboko, pamoja na kuchezea kipigo cha mbwa mwizi bado umejikongoja kupost....
Ah! Hapa tunatakiana kheri hivyo iwe funzo kwa wengine ndiyo lengo langu, makofi nimepokea mfululizo japo nashukuru sikupigwa mateke wala virungu kama wenzangu.
 
Kama movie vile....
Taarifa zingeshakuja kwenye media tumekamata majambazi wakiwa na gari dogo..... Lkn hayo ndo matokeo ya kukaidi amri ya polisi japo hatujui kitu gan wanataka.
Iwe d
Fundisho kwetu
Kabisa kabisa mkuu, na kuanzia leo nimejua umuhimu wa polisi na upendo kwetu raia jinsi wanavyopambana usiku kucha.
 
  • Thanks
Reactions: Ok9
Hakuna haja ya kuwakimbia labda uwe na kosa kubwa.
pole.
Mama nazipokea busara zako mimi kama mwanao au hata ndugu yako, hekima ni jambo jema na ubarikiwe.
 
Simulizi yako inatoa FUNZO sana. .kama huna kosa, isiwakimbie askari.Pole kwa masaibu
Valid, nashukuru nipo nanyi tena maana hata wao pamoja na ukali wote na kipigo lakini baadae walinipa darasa na nikawashukuru sana.
 
Pumbavu wewe,.. Haya kunywa bia moja ulale... Umefanya ujinga mkubwa sana.
Matusi, kejeli na dharau havinifikirishi.....nafikiria tu yaliyonisibu na kumshukuru Mungu, kuhusu bia sijawahi kunywa tangu kuzaliwa kwangu.
 
Ulistahili virungu hata sikupi pole mana umejitakia
Nimeshavipata vya kumwaga hivyo ridhika kuwa unachoona nastahili nimekipata, hata hivyo imetokea kama ajali na sikuwa na sababu yeyote ya kufanya hayo haswa kwa kuwa si mgeni wa njia ile.
 
Pole sana. Siku nyingine usithubutu sbb kipind hiki wanafanya kazi kwa sifa sana. Waliambiwa wakikuta mtu porini wauwe. Na mkuu wa kaya akapigilia msumari,
siku hiz hawachagui pa kupiga, wanafanya kwa sifa
Akhsante sana ndugu yangu kwa kunipa pole.
 
Ulifanya jambo la kijinga sana na ulistahili hayo makofi!
Tuangalie pia wangapi hukimbia askari barabarani na tusione ni kama jambo jipya, pia uthubutu wangu wa kuandika hapa usichukuliwe kwa kulaumu tu bali pia iwe funzo kwa wengine.
 
Back
Top Bottom