Ila wanawake mna dhambi wakati mwingine

Ila wanawake mna dhambi wakati mwingine

Hapo tatizo lipo kwa me, kwanini usiwe muwazi tu kwa huyo mlimbwende wako? Unapretend unajiweza wacha wakukamue hadi utoke jasho
Shida demu wake ni kisu kiaina na jamaa anakosa sauti kabisa.. huwa inatokea aisee
 
Nimeishuhudia jana hii jana kwa rafiki yangu wa karibu,

Upo na gari yako (IST) umetoka job ukampitia Girlfriend wako mkale bata na kutoa machungu ya kazi za wiki nzima. Girlfriend wako ni type flani hivi za wanawake wa kimjinimjini, anaamua pia kwenye mtoko huo aungane na best yake wanafanya kazi pamoja.

Paaaaaaap, kidume unawapitia gari; Girlfriend wako anakaa siti ya mbele na best yake anakaa siti ya nyuma. Unafika Magomeni bahati mbaya kuna foleni ya magari, unasubir dakika kama 20 hiv unaona foleni haijaruhusiwa. Unapandwa na hasira unaamua kuzima gari, punde kama dakika tano tena unaona foleni inaruhusiwa, unaamua kuwasha gari lakini linagoma kuwaka.

Solution inakuwa ni kusukuma gari na kuliweka pembeni, kwakuwa wewe unakifua kama kabati unaona ukimpata mtu mmoja anatosha kabisa kukusaidia mkasukuma gari mkaliweka pembeni.

Wakati huo huo GF wako na best yake, wameona kabisa kwamba unahitaji msaada na wangeweza kabisa kutoka na kukusaidia kusukuma gari na kulipaki pembeni, ila wanaamua tu kuua soo na kutoa simu zao na kusurfsurf.

Huku nyuma kidume unampata teja mmoja unamtoa jero anaamua kukusaidia. Mnaanza kusukuma gari na kumsukuma na GF wako na best yake. Unafanikiwa kulipak pembeni hapo hapo unafanya mpango fundi mara moja halafu anaweka mambo sawa unaendelea na safari yako ya kula bata.

Kwa kuwa demu wako ni wa kimjinimjini unaamua kwenda nae lachaz pale, baada ya kuvuja jasho ya kusukuma gari unaanza pia kuvuja jasho kwenye upande wa wallet maana unagundua shot wanazopiga ni za kiwango cha first class.

Baada ya masaa manne unagundua kwamba bajeti iliyopo kwenye wallet haiwez kuhimili hii ligi ya kiwango cha La Liga cha huyu GF wako na best yake.

Kidume unaanza kusumbua washkaji saa sita usiku wakutumuie walau laki moja ili mechi iishe salama...

Kweli nyinyi wanawake nadhani kuna jehanamu yenu maalumu inawasubiri
Tatizo la kumiliki demu ambae siyo level yako matokeo ndo hayo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mnaelewaga kwamba mdau hana au ndo basi baadae muaze kumgeuza mada ya kulalia
😀😀😀, huyo mwanaume naye alishindwaje kuwa muwazi kwa GF wake kwamba mfuko wake kwa leo ni kiasi fulani, ili wajiongeze na huyo shosti ake ktk matumizi , sasa sijui alitaka sifa ili aonekane yuko vizuri,Pole yake ila siku nyingine akili itamkaa sawa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mzee hili la kusema ukweli wengi hawana kifua.
Haswa pale mwanamke anapokuwa mzuri.. Ukijidai kusema ukweli ndo tiket ya kuachwa saa nyingine.. So option nzur ni ku chill mpaka umle vya kutosha
 
Afu muache dharau,mtu kukusaidia kusukuma gari na kumpa jero ushamwita teja,hapo wa kulaumiwa siyo ke ni me,kwanini usimwambie huna pesa ya kutosha mpaka unaanza kukopa kwa mambo ya kisengerema.
 
Mtaan kuna watot wazur zaidi ya Irene uwoya tena wabichi gharama yao ndogo sana,kwann mnajitwika kwenye mashetan kama hayo
 
Nshawahi kushusha mademu kwenye gari. Nlipata hitilafu wakadai wanatangulia kwenye tukio. Lilipopona nikawajoin wakati tunarudi wakataka kupanda. Nkawaambie watafute bajaji au boda nkawatema sa 6 usiku.

Usiniulize walifikaje makwao

Sent using Jamii Forums mobile app
 
😀😀😀, huyo mwanaume naye alishindwaje kuwa muwazi kwa GF wake kwamba mfuko wake kwa leo ni kiasi fulani, ili wajiongeze na huyo shosti ake ktk matumizi , sasa sijui alitaka sifa ili aonekane yuko vizuri,Pole yake ila siku nyingine akili itamkaa sawa.
Kupenda kuonekana matawi ya juu kumbe hohe hahe. Kama ni girlfriend iweje ushindwe kumwambia status ya mfuko wako, halafu analeta rafiki yake unakubali vipi? Huyo jamaa ni danga
 
Kupenda kuonekana matawi ya juu kumbe hohe hahe. Kama ni girlfriend iweje ushindwe kumwambia status ya mfuko wako, halafu analeta rafiki yake unakubali vipi? Huyo jamaa ni danga
Ndyo wakaamua kumkomesha jamaa, wakafyonza vinywaji vingii ili ajute , ila hawana huruma khaa. Mtu anasukuma Gari ,eti hata hawajashuka ,

Sent using Jamii Forums mobile app
 
sheria namba moja. USIMWACHIE MWANAMKE ACHAGUE MAHALI PA KUKUTANA
sheria namba mbili . UKIONA ULIYEMWALIKA KAJA NA LUNDO LA WATU TENGENEZA DHARURA YA GHAFLA SANA NA ONDOKA HILO NI KUNDI LA WACHIMBAJI WADOGO WADOGO WATAKUACHIA MASHIMO.
 
Back
Top Bottom