Ikulu mpya na maswali

Ikulu mpya na maswali

HIMARS

JF-Expert Member
Joined
Jan 23, 2012
Posts
72,960
Reaction score
102,733
Je, kuna ulazima wa yafuatayo au ni kupoteza pesa za walipa kodi?
  1. Kujenga Njia ya Kuruka Ndege Ikulu.
  2. Ujenzi wa Viwanja vya Golf.
  3. Ujenzi wa Complex ya watu 2000-3000
NB: Kama wanatimiliza Ndoto ya Nyerere kwanini Complex isiitwe Nyerere Complex au iitwe aliyeanzisha Ujenzi Magufuli Complex. Kwanini iitwe Samia Complex?

Je, Watanzania tuna kodi kiasi hicho kujenga Ikulu ya namna hiyo? Kuna ulazima gani?

Je, nani mnufaika wa hayo yote?

Kwanini hizo pesa zisiende kwenye elimu ya awali na msingi maana huko ndo chanzo cha madudu ya huku juu?
 
Je kuna ulazima wa yafuatayo au ni kupoteza pesa za walipa kodi?

Kujenga Njia ya Kuruka Ndege Ikulu

Ujenzi wa Viwanja vya Golf

Ujenzi wa Complex ya watu 2000-3000


NB: Kama wanatimiliza Ndoto ya Nyerere kwanini Complex isiitwe Nyerere Complex au iitwe aliyeanzisha Ujenzi Magufuli Complex
Kwanini iitwe Samia Complex?


Je Watanzania tuna kodi kiasi hicho kujenga Ikulu ya namna hiyo?

Kuna ulazima gani?

Je nani mnufaika wa hayo yote?

Kwanini hizo pesa zisiende kwenye elimu ya awali na msingi maana huko ndo chanzo cha madudu ya huku juu?
Tatizo Afrika sio pesa, pesa ipo ila vipaumbele. Hapo wakikwambia zinahitajika pesa kwa ajili ya mashine za kusaifisha damu kwa wagonjwa wa figo ziwekwe kila hospitali ili gharama zishuke waweze kuafford watakujibu budget haitoshi.
Complex ya watu 2000 ikulu ya kazi gani?
 
Tatizo Afrika sio pesa, pesa ipo ila vipaumnele. Hapo wakikwambia zinahitajika pesa kwa ajili ya kusaifisha damu kwa waginjwa wa figo ziwekwe kila hospitali ili gharama zishuke waweze kuafford watakujibu budget haitoshi.
Complex ya watu 2000 ikulu ya kazi gani?
Jana Samia kaongea kuwa Ikulu bado kuna mambo yanafanyika ikiwa ni pamoja na ujenzi wa njia ya kurukia Ndege
 
Tatizo Afrika sio pesa, pesa ipo ila vipaumnele. Hapo wakikwambia zinahitajika pesa kwa ajili ya kusaifisha damu kwa waginjwa wa figo ziwekwe kila hospitali ili gharama zishuke waweze kuafford watakujibu budget haitoshi.
Complex ya watu 2000 ikulu ya kazi gani?
Kifurushi cha bima ya watoto yenyewe wameshindwa. Kisha mmama mtu mzima wanayemuita rais anashangilia kujengwa kiwanja kwa golf sababu anajua wajukuu zake watatibiwa ulaya.
 
Jana Samia kaongea kuwa Ikulu bado kuna mambo yanafanyika ikiwa ni pamoja na ujenzi wa njia ya kurukia Ndege
Hatari sana what for? Wangeweka tu kiwanja cha helicopter ingekuwa poa tu. Afrika tuna shida mahala viongozi wanataka kufanya mambo kama donor country tena unakuta donor country hata hawafanyi hivyo. Just imagine ni pesa kiasi gani itatumika kuitunza hiyo complex kwa kila mwezi?
 
Hatari sana what for? Wangeweka tu kiwanja cha helicopter ingekuwa poa tu. Afrika tuna shida mahala viongozi wanataka kufanya mambo kama donor country tena unakuta donor country hata hawafanyi hivyo. Just imagine ni pesa kiasi gani itatumika kuitunza hiyo complex kwa kila mwezi?
Pia sikuona sababu ya Ikulu kuwa na eneo kubwa vile, operations costs ni kubwa sana
 
Je, kuna ulazima wa yafuatayo au ni kupoteza pesa za walipa kodi?

  1. Kujenga Njia ya Kuruka Ndege Ikulu.
  2. Ujenzi wa Viwanja vya Golf.
  3. Ujenzi wa Complex ya watu 2000-3000
NB: Kama wanatimiliza Ndoto ya Nyerere kwanini Complex isiitwe Nyerere Complex au iitwe aliyeanzisha Ujenzi Magufuli Complex. Kwanini iitwe Samia Complex?

Je, Watanzania tuna kodi kiasi hicho kujenga Ikulu ya namna hiyo? Kuna ulazima gani?

Je, nani mnufaika wa hayo yote?

Kwanini hizo pesa zisiende kwenye elimu ya awali na msingi maana huko ndo chanzo cha madudu ya huku juu?
Ukiona mtu yoyote katia neno kwanini pesa hizo zisiende kwenye elimu ujue mwisho wake wa kufikiri umeishia hapo. Ngoja nikujibu kwa urahisi tu, Ikulu ya nchi ni hazina ya nchi na itabaki hata vizazi vinayokuja ni muhimu kuwa na sehemu bora ya kufanya shughuli za serikali wala sio kupoteza pesa kwa mawazo yako maana ni kama kusema budget ya nchi 100% iende kwenye shule tu huu ni ujinga kila kitu kinapangwa kwa budget na elimu ina budget yake. Ukisema kodi kwani uliambiwa kodi yako inaongezake kulipia ujenzi? acheni gubu hata wewe unaweza kumuita mtoto wako Magufuli. Stand Magufuli, Mji wa serikali Magufuli na mpaka ikulu Magufuli imekuwa nini tena, Nyerere jina lake liko kila sehemu mimi naona tubadilishe nchi jina tu kutoka Repuclic of Tanzania to Republic of Nyerere au Magufuli
 
Ukiona mtu yoyote katia neno kwanini pesa hizo zisiende kwenye elimu ujue mwisho wake wa kufikiri umeishia hapo. Ngoja nikujibu kwa urahisi tu, Ikulu ya nchi ni hazina ya nchi na itabaki hata vizazi vinayokuja ni muhimu kuwa na sehemu bora ya kufanya shughuli za serikali wala sio kupoteza pesa kwa mawazo yako maana ni kama kusema budget ya nchi 100% iende kwenye shule tu huu ni ujinga kila kitu kinapangwa kwa budget na elimu ina budget yake. Ukisema kodi kwani uliambiwa kodi yako inaongezake kulipia ujenzi? acheni gubu hata wewe unaweza kumuita mtoto wako Magufuli. Stand Magufuli, Mji wa serikali Magufuli na mpaka ikulu Magufuli imekuwa nini tena, Nyerere jina lake liko kila sehemu mimi naona tubadilishe nchi jina tu kutoka Repuclic of Tanzania to Republic of Nyerere au Magufuli
Acha mawazo mfu,nyie ndio mnaojifanya hamjui shida za hii nchi mnapenda anasa kuliko kutatua changamoto za wananchi masikini.makolokolo yote hayo kwa lengo lipi hasa,eti hazina,kwani ili kitu kiwe hazina kinatakiwa kuwa na izo kolokolo zote utumie B kwenye izo kolokolo wakati una wananchi ambao hawana maji Safi na salama uo ni mfano tu.Tubadilikeeeee
 
Acha mawazo mfu,nyie ndio mnaojifanya hamjui shida za hii nchi mnapenda anasa kuliko kutatua changamoto za wananchi masikini.makolokolo yote hayo kwa lengo lipi hasa,eti hazina,kwani ili kitu kiwe hazina kinatakiwa kuwa na izo kolokolo zote utumie B kwenye izo kolokolo wakati una wananchi ambao hawana maji Safi na salama uo ni mfano tu.Tubadilikeeeee
Huyo jamaa hana akili.

Elimu ndo Msingi wa maendeleo ya nchi yoyote duniani.
Bila Elimu bora wananchi hawataendelea
 
Acha mawazo mfu,nyie ndio mnaojifanya hamjui shida za hii nchi mnapenda anasa kuliko kutatua changamoto za wananchi masikini.makolokolo yote hayo kwa lengo lipi hasa,eti hazina,kwani ili kitu kiwe hazina kinatakiwa kuwa na izo kolokolo zote utumie B kwenye izo kolokolo wakati una wananchi ambao hawana maji Safi na salama uo ni mfano tu.Tubadilikeeeee
Toka lini tulikuwa na maji safi na salama? kabla ya ikulu kujengwa au? pambana na maisha tafuta pesa hakuna wa kukusaidia hata hayo maji safi na salama ya kulipia hakuna bure hujalipa unakatiwa tu. ondekeni na fikra za kimasikini ufanyiwe na serikali hakuna kitu hicho, tafuta pesa hakuna mtu maskini tafuta utapata utakunywa maji safi tu. acheni nongwa kama kipaumbele chako maji safi wengine sio kipaumbele chetu hicho, usilazimishe ujamaa humu
 
Huyo jamaa hana akili.

Elimu ndo Msingi wa maendeleo ya nchi yoyote duniani.
Bila Elimu bora wananchi hawataendelea
Kwani kuna mahali serikali imesema imekosa hela ya kuendeshea elimu? Ni sahihi kuwa na eneo kubwa la Ikulu maana pale Dar kuna mpaka wanyamapori sasa kwa Ikulu ya Chamwino kuwa na eneo kubwa itakuwa rahisi hata kuanzisha hiyo game ranch kwa ajili ya wageni wetu! Eneo lina ukubwa wa ekari elfu 8 sasa wakigawa hata ekari elfu 6 au 7 kwa ajili ya game ranching itapendeza sana!
 
Je, kuna ulazima wa yafuatayo au ni kupoteza pesa za walipa kodi?
  1. Kujenga Njia ya Kuruka Ndege Ikulu.
  2. Ujenzi wa Viwanja vya Golf.
  3. Ujenzi wa Complex ya watu 2000-3000
NB: Kama wanatimiliza Ndoto ya Nyerere kwanini Complex isiitwe Nyerere Complex au iitwe aliyeanzisha Ujenzi Magufuli Complex. Kwanini iitwe Samia Complex?

Je, Watanzania tuna kodi kiasi hicho kujenga Ikulu ya namna hiyo? Kuna ulazima gani?

Je, nani mnufaika wa hayo yote?

Kwanini hizo pesa zisiende kwenye elimu ya awali na msingi maana huko ndo chanzo cha madudu ya huku juu?
Watu mnawivu mno khaaaaa.
Kuna mambo hayana maana kabisa kuyaazishia mjadala
 
Back
Top Bottom