Ikulu, Dar: Rais Samia akutana na Freeman Mbowe

figganigga

JF-Expert Member
Oct 17, 2010
25,492
54,890
866F62F8-9E58-4FE3-A4D4-3B9A30471A9B.jpeg

Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan leo amekutana na kuzungumza na Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema Freeman Mbowe Ikulu Mkoani Dar Es Salaam.

Rais Samia amesisitiza kuwa kuna umuhimu wa kushirikiana ili kuijenga Tanzania kwa kuaminiana na kuheshimiana kwa misingi ya haki.

Mhe. Mbowe amemshukuru Rais Samia kwa kuonesha kwake kujali huku akikubali kuwa msingi mkubwa wa kujenga taila la Tanzania ni kusimama katika haki.

Vile vile, amesema wamekubaliana kufanya siasa za kistaarabu na kiungwana na kuwa yuko tayari kushirikiana na Serikali katika kuleta maendeleo ili nao pia waweze kutekeleza majukumu yao ipasavyo.


====

Picha Mbalimbali zikimuonesha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, akisalimiana na kuzungumza na Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Freeman Mbowe alipowasili Ikulu Jijini Dar Es salaam leo tarehe 04 March 2022

IMG_20220304_221704_270.jpg
IMG_20220304_221833_774.jpg
IMG_20220304_221830_135.jpg
IMG_20220304_222549_166.jpg
 
Tunategemea chadema itaendelea na mapambano ya kudai Haki na uhuru wa vyama vingi hili likishindikana basi tena tujiunge wote na ccm tu hakuna namna. Kwahiyo mwenyekiti pamoja na yote mliyozungumza na Rais samia leo baada ya kutoka gerezani hilo naomba uliweke akilini.
 
Tunategemea chadema itaendelea na mapambano ya kudai Haki na uhuru wa vyama vingi hili likishindikana basi tena tujiunge wote na ccm tu hakuna namna. Kwahiyo mwenyekiti pamoja na yote mliyozungumza na Rais samia leo baada ya kutoka gerezani hilo naomba uliweke akilini.
Usiogope!
 
Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan akutana na kuzungumza na Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema Freeman Mbowe Ikulu Mkoani Dar Es Salaam.

Rais Samia amesisitiza kuwa kuna umuhimu wa kushirikiana ili kuijenga Tanzania kwa kuaminiana na kuheshimiana kwa misingi ya haki.

Mhe. Mbowe amemshukuru Rais Samia kwa kuonesha kwake kujali huku akikubali kuwa msingi mkubwa wa kujenga taila la Tanzania ni kusimama katika haki.

Vile vile, amesema wamekubaliana kufanya siasa za kistaarabu na kiungwana na kuwa yuko tayari kushirikiana na Serikali katika kuleta maendeleo ili nao pia waweze kutekeleza majukumu yao ipasavyo.

Picha Mbalimbali zikimuonesha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, akisalimiana na kuzungumza na Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Freeman Mbowe alipowasili Ikulu Jijini Dar Es salaam leo tarehe 04 March 2022
View attachment 2139037View attachment 2139038View attachment 2139039View attachment 2139058
Naiona Tanzania Mpya hii hapa...
Mwendazake alituelekeza mkondo wa kuzimu!
Sasa tushikamane sote tudai uhuru kamili tusonge mbele na ujenzi wa taifa letu!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom