Ikulu, Dar: Rais Magufuli azungumza na Wabunifu wa mitambo midogo ya kufua umeme kwa kutumia maji ya mito

Ni vyema likatolewa tangazo na Tanesco kama wananunua umeme kutoka kwa local producer.


Sipingani nawewe lakini kuna vitu inabidi tuvifikirie kiundani sana kabla ya kuvichukulia maamuzi..
Newtons, Faraday, Galileo nk walikuwepo kipindi hicho dunia ikiwa haina uelekeo na hakuna teknolojia hivyo wao kanuni zao ndio zikaleta msingi wa kila kitu leo kwa maana ya Meli, Ndege, Rockets, submarines nk, Kifupi kwa sasa hakuna kitu utatengeneza bila kupitia kwenye hiyo misingi. Kinachofanyika duniani kwa sasa ni researches na technology invention zikitumika kanuni ambazo tayari zipo, Mchina akaja kwa kasi na kitu kinaitwa reverse engineering kwa maana ya copy and paste ili naye aingie kwenye soko.

Kama tumeamua kutengeneza hivi vitu lazima pia tujue sababu ni ipi hasa, tutengeneze tuuze au tutengeneze tutumie?
Kama kutengeneza kuuza tunamuuzia nani na soko likoje la bidhaa hiyo maana sokoni tayari wapo wengine, Je tutaweza kushindana kwenye ubora, ufanisi, bei na umadhubuti wa bidhaa yetu?
Kama tutaamua kutengeneza na kutumia wenyewe, Je itatulipa kiuchumi kwa maana ileile ya ufanisi, ubora, gharama za uendeshaji, umadhubuti nk..
Binafsi naamini kuendelea kupoteza muda kwenye hizi local inventions ni kama kuamua kuishi 1800 wakati dunia iko 2019 labda kama tumeamua kuanza mwanzo kujifunza, maana naamini tuko watanzania wengi wenye uwezo wa kudesign na kuendesha hizo local invetions kama Magari ya kienyeji, bunduki, Umeme wa kienyeji, Pombe za kienyeji, Ndege za kienyeji, Meli za kienyeji nk. SERIKALI IKITOA RUHUSU UTAONA MPAKA BUNDUKI ZA KIENYEJI HUKO URAIA, UMEME TUTANGENEZA WENYEWE HUKO URAIANI maana si kweli kutengeneza hivi vitu kunahitaji kipaji au akili sana everybody can do it locally tuwe wakweli..

Serikali iache kukimbia majukumu yake; uwekezaji mkubwa unahitajika kwenye technology ili vijana wengi waweze kuwa na uwezo kwenye ubunifu wa kweli utakaoendana na kasi ya sasa ya dunia ili hizo teknolojia zitakazogunduliwa ziweze kuleta tija kwenye jamii yote kuanzia kwetu hapa na duniani kwa ujumla.
kwa mawazo haya nitakwazwa sana na mtu atakaekujibu kwa kutanguliza neno "mkuu"..
 
kwahiyo bora tuache tu sio!!
kutengeneza kitu chochote kwa matumizi binafsi kwa maana ya nyumbani kwako changamoto inaweza kuwa ndogo au isiwepo kabisa, Lakini kitu hicho hicho kwa matumizi ya wengi hapo ndipo changamoto zinapoanza na utaalamu ndipo utaanza kuhitajika.. Kuzalisha maji au kufua umeme kutoka kwenye chanzo sio tatizo na maarifa hayo yapo kwa wengi tatizo linaaza pale utapohitaji kupeleka kwenye matumizi ya wengi maana mengi lazima yazingatiwe ili huduma hiyo isiwe namadhara.
 
Kuna mambo Rais wetu huwa anafanya hata kama vyuma vimekaza na pamoja na kuwalea vibaraka Fulani Fulani huwezi kukosa kumpenda na kumpongeza. Nasema sijui kama ni michezo ya kisiasa au muumini wa kweli wa Uzalendo na kuamini katika falsafa ya kutatua matatizo yako mwenyewe ndio msingi mkuu wa maendeleo ya binadamu. Kama ni muumini wa kweli wa falsafa hii basi tumsamehe kwa mengine lakini kwa ujumla wake Rais tunae. Ukweli ni kwamba hata uende ukapate digrii Harvard, Yale, Oxford au Cambridge kama unashindwa pata uvumbuzi wa matatizo yako msingi kama binadamu basi umepoteza muda wako na wa jamii yako kwenda mbali sana kupata elimu ambayo ungeweza kuipata hata kama ungeendelea kuishi kwenye Bariadi au Maswa. Kwenye hili alilofanya leo na maneno aliyoyasema pale kwenye mkutano huu na wabunifu kanigusa JPM.
 
Magufuli huwa anapenda sana kukurupuka. Hapa alipaswa kuwatuma kwanza wataalamu wote wahusika wakakae na hao wagunduzi ilii wamletee concrete findings and opinions.

Hapa nao watu wanajikanyaga kanyaga tu kwa kushtukizwa bila hoja zenye msingi na msimamo.
Na Magufuli alivyo usishangae Akaondoka na Mtu hapa!
jinga sana wewe na siasa zako mavi na kukosoa kila kitu....
Hii inakufanya ujione una akili kuliko JPM...
Toka miaka ya 80 hao wataalam hawajawahi kusikia kuna wafua umeme asilia?
This is his approach kuwafanya viongozi na wataalam wajione wajinga na wasikilize kila mtu na ubunifu wake wasisubiri yeye awaite ikulu na kuwa storm na maswali.. Kosa liko wapi hapo??..
Uko kwenye kizazi cha wajinga wanaojifanya wanajua..
Ati kakurupuka.. nyanmbaff
 
Sileti dharua kwa yeyeto.Napinga layman kujipendekeza ni mtaaalam wa energy systems. Usistajabu mapendekezo ya mashine inayozalisha umeme milele daima bila gharama yeyote-perpetual motion machine.
Acha dharau za kishamba, Kwani Faraday uliyemsoma na laws zake alikuwa na elimu gani? Hayo majenereta si yeye ndiye aliyeyagundua bila hata ya kujua surface integral ni nini?
 
Ubunifu wa ku supersede technology ya kufua umeme iliyopo kwenye soko?
Heee, unasemaje mkuu. Wamebuni teknologia mpya kabisa, mbali ya hii iliyopo sasa?

Anyway, nawapongeza sana kwa juhudi zao na hasa moyo wa kujituma walionao. Katika siku hizi, na changamoto zote zinazotukabili sote, lakini wao wakaendelea na juhudi zao, wanastahili pongezi sana.

Kuhusu aina ya ugunduzi waliofanya, huenda siku moja wakapata mda wa kueleza kwa kina ili sote tujue.

Ingefaa, Taasisi kama COSTEC wakawa na utaratibu wa kufanya makongamano, hata kama ni mara moja kwa mwaka ikawa ndio sehemu nzuri ya kuwapa wagunduzi mbalimbali kuzungumzia kazi zao. Hatua hii ingewatia moyo, hasa vijana kuendeleza vipaji walivyonavyo.
 
Lakini tuseme tu ukweli, maswali na hoja za Maghufuli ni kama za humu JF kabisa. Huyu jamaa ni member humu bila shaka hata kidogo. Yani maswali aliyokuwa akiwapiga hao mafala, ni kama maswali ambayo hata mimi ningeyauliza. Nimegundua huyu rais ni smart sana. Mnyonge myongeni...

Ila Ben Saanane angeridishwa na waliompiga risasi Lissu kuchukuliwa hatua, mambo yangekuwa mswanu sana yani.
 
Kama tumeamua kutengeneza hivi vitu lazima pia tujue sababu ni ipi hasa, tutengeneze tuuze au tutengeneze tutumie?
Kama kutengeneza kuuza tunamuuzia nani na soko likoje la bidhaa hiyo maana sokoni tayari wapo wengine, Je tutaweza kushindana kwenye ubora, ufanisi, bei na umadhubuti wa bidhaa yetu?
Kama tutaamua kutengeneza na kutumia wenyewe, Je itatulipa kiuchumi kwa maana ileile ya ufanisi, ubora, gharama za uendeshaji, umadhubuti nk..
Binafsi naamini kuendelea kupoteza muda kwenye hizi local inventions ni kama kuamua kuishi 1800 wakati dunia iko 2019 labda kama tumeamua kuanza mwanzo kujifunza, maana naamini tuko watanzania wengi wenye uwezo wa kudesign na kuendesha hizo local invetions kama Magari ya kienyeji, bunduki, Umeme wa kienyeji, Pombe za kienyeji, Ndege za kienyeji, Meli za kienyeji nk. SERIKALI IKITOA RUHUSU UTAONA MPAKA BUNDUKI ZA KIENYEJI HUKO URAIA, UMEME TUTANGENEZA WENYEWE HUKO URAIANI maana si kweli kutengeneza hivi vitu kunahitaji kipaji au akili sana everybody can do it locally tuwe wakweli..

Serikali iache kukimbia majukumu yake; uwekezaji mkubwa unahitajika kwenye technology ili vijana wengi waweze kuwa na uwezo kwenye ubunifu wa kweli utakaoendana na kasi ya sasa ya dunia ili hizo teknolojia zitakazogunduliwa ziweze kuleta tija kwenye jamii yote kuanzia kwetu hapa na duniani kwa ujumla.
[/QUOTE]
Sijui kama nimekuelewa sawa sawa uliyoandika hapa, au pengine sikupati vizuri.

Sitaandika kwa kirefu kujibu hoja yako hii kwani ninahisi hata kuandika kitabu kizima juu ya jambo hili. Nitoe tu mifano michache itatosha.
1. Taiwan sasa hivi wanayo 'chemical industry' nzuri sana kiasi kwamba viwanda vyao wanatengeneza 'active pharmaceutical ingredients' zinazotumika kutengeneza madawa sehemu mbalimbali duniani na viwanda vikubwa vinavyotengeneza madawa. Hawa hawakutegemea watumie tu njia za wengine, lakini walitumia uvumbuzi wao ulioshirikisha yaliyokuwepo tayari ili kujenga viwanda vyao hivi.

2. China sasa hivi wanauza ma-mashine ya kila aina duniani kote, na hasa hapa kwetu Afrika. Wametumia ubunifu wao wa kuiga hayo yaliyokwishagunduliwa na sasa hivi wanaelekea kuwa vinara sehemu nyingi.

Hali ni hiyo hiyo Korea Kusini na kwingineko.

Mimi ningekuwa Magufuli, wakati huu ningewakusanya wastaafu wote wenye taaluma maalum mbalimbali.

Mathalani. Pale Mlimani na Mhimbili wamefundisha sana watu wa Kemia na Mambo ya kutengeneza Madawa. Kuna watu wametumika katika vyuo hivyo maisha yao yote na sasa wengi wao wameupeleka utaalam wao wote majumbani mwao. Pamoja na kwamba tunao vijana wengi ambao wamo kazini sasa hivi, ningewashirikisha pamoja na wastaafu hao wenye uzoefu waweze kufanya mambo ambayo taifa hili halijawahi kuyafanya.
Ningewaweka kambi maalum na kuwapa jukumu la kutengeneza mazingira ya kuwa na viwanda vyetu vyenye uwezo kamili wa kutengeneza kila aina ya dawa inayopatikana duniani.

Hii sio ndoto hata kidogo. Watu wetu tulionao sasa hivi tungeamua kuwatumia ipasavyo nchi yetu ingebadilika haraka sana katika kila nyanja ambayo tungependa kuiendeleza.

Nilisema sitaandika kwa kirefu. Acha niishie hapa.
 
Ila Ben Saanane angeridishwa na waliompiga risasi Lissu kuchukuliwa hatua, mambo yangekuwa mswanu sana yani.
Ni vigumu kuelewa kwa nini ililazimu haya yafanyike, kwani yamewaondoa wengi waliotaka kuona haya mengine mazuri yakipewa nguvu zaidi. Wengine roho zilipinda moja kwa moja baada ya matukio hayo yaliyokuwa si ya lazima yafanyike.
 
Rais Magufuli leo 13 Juni, 2019 anakutana na Wabunifu wa mitambo midogo ya kufua umeme kwa kutumia maji ya mito

Kuanzia saa 3:30 Ikulu Jijini Dar es salaam





UPDATE
Rais Magufuli:
Nilifikiri kuwa Mkurugenzi wa TANESCO pamoja na Katibu Mkuu wangekuwepo hapa kusikiliza shida zao. Hawa ni mafundi ndiyo maana hawazungumzi sana.


Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia, Dkt. Amos Nungu
Hadi sasa jumla ya wabunifu 60 wameshatambuliwa na kuingizwa katika Kanzidata ya Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia

Mkurugenzi wa TANESCO, Dkt. Tito Mwinuka.
TANESCO imejipanga kutoa shilingi Milioni 30 kwa ajili ya wabunifu wawili wa mitambo midogo ya kufua umeme ili waongeze uzalishaji wa umeme huo

Tutawaendeleza wabunifu hawa wawili wa mitambo midogo ya kufua umeme kwa kuwaongezea shilingi Milioni 20 kwa ajili ya kuendeleza kazi zao

TANESCO imejipanga kutoa shilingi Milioni 30 kwa ajili ya wabunifu wawili wa mitambo midogo ya kufua umeme ili waongeze uzalishaji wa umeme huo

Rais Magufuli
Tatizo la Watanzania tunajidharau na hatuthamini vya kwetu, hawa wabunifu wa mitambo wangegunduliwa mapema wangepunguza gharama za uzalishaji umeme kwa sababu tayari wana chanzo cha umeme.

Wangekuwa wameshasaidiwa wasingefika hapa. Transfoma zingekuwepo, Mkurugenzi wa TANESCO kwao ni Njombe na nina uhakika huwa anaenda likizo huko lakini hajafanya lolote. Meneja wa TANESCO mkoa (Njombe) nimemsikia akizungumza hawa waje wanione kasha waende Ewura…yeye hakutaka shida.

Hata wangezalisha umeme ukaleta madhara shida isingekuwa kwa watendaji wa TANESCO kwa hiyo Mkurugenzi wa Njombe naye hajaleta taarifa yoyote kuhusiana na wagunduzi hawa tangu mwaka 1980.

Natoa siku saba kwa TANESCO kwenda katika eneo la mradi huo wa kufua umeme uliopo Mkoani Njombe na kuona ni namna gani utafanya kazi vizuri zaidi

Natoa wito kwa viongozi wote kuangalia Televisheni ya Taifa (TBC) ili kila kitakachoonyeshwa kuhusu wizara husika kikashughulikiwe kwa haraka.

Natoa shilingi Milioni Tano kwa wabunifu wawili wa mitambo midogo ya kufua umeme ili kuwaongezea mtaji katika shughuli zao.

Zaidi, soma;

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli tarehe 13 Juni, 2019 amekutana na wabunifu wawili wa kuzalisha umeme kwa kutumia maji ya mito kutoka Mkoani Njombe na kuagiza wataalamu wa wizara na taasisi zinazojihusisha na sayansi, teknolojia na uvumbuzi kuwafuatilia na wabunifu na wavumbuzi mbalimbali ili kuwaunga mkono katika kuboresha kazi zao.

Wabunifu waliokutana na Mhe. Rais Magufuli Ikulu Jijini Dar es Salaam ni John Akani Fute na Jairos Ngairo ambao wamebuni miradi ya kuzalisha umeme kwa kutumia maji yanayotiririka mtoni, kusukuma maji kwa kutumia pampu zisizotumia umeme na kusaga nafaka kwa kutumia machine zinazoendeshwa na maji ya mto. Bwana Fute amebuni mradi unaozalisha kilowati 28 na Bw. Ngairo anazalisha kilowati 15 za umeme.

Mkutano huo umewahusisha Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati Dkt. Hamis Mwinyimvua, Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dkt. Leonard Akwilapo, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara Bw. Ludovick Nduhiye pamoja na viongozi na wataalamu wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), Tume ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) na Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC).

Mhe. Rais Magufuli amewapongeza wabunifu hao kwa kuzalisha umeme wa gharama nafuu unaowanufaisha wananchi na ameagiza TANESCO na COSTECH kuwaunga mkono ambapo TANESCO itatoa shilingi Milioni 30 na COSTECH shilingi Milioni 20 kwa wabunifu hao, na pia timu ya wataalamu itaondoka kesho kwenda Njombe ilipo miradi hiyo kwa ajili ya kutoa ushauri wa kitaalamu na kuiboresha.

Mhe. Rais Magufuli ameelezea kutofurahishwa na vitendo vya wataalamu kuwakatisha tamaa na kuwatisha wabunifu wa vitu mbalimbali vinavyowasaidia wananchi kama ambavyo Bw. John Fute (Pwagu) na Bw. Jairos Ngairo wamekuwa wakifanyiwa na badala yake ametaka wabunifu hao waungwe mkono kwa ushauri wa kitaalamu na kuwawezesha kuongeza tija.

Mhe. Rais Magufuli ameipongeza TBC kwa kufuatilia kazi za ubunifu na uvumbuzi kupitia makala yake ya Hadubini (Habari kwa Kina) ikiwemo makala ya ubunifu wa mradi huo wa umeme iliyoandaliwa na waandishi wa Habari Bi. Tatu Abdallah na Bi. Zaituni Mkwama na ameagiza Wizara na Taasisi za Serikali kufuatilia taarifa zinazotangazwa na vyombo vya habari na kuchukua hatua katika maeneo yanayozihusu.

Ameiagiza Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kufuatilia jengo la ghorofa 3 linalodaiwa kutelekezwa na raia mmoja wa kigeni huko Kunduchi Jijini Dar es Salaam ambalo limebaki mikononi mwa mlinzi ambaye anatishwa na wajanja wanaotaka kujimilikisha kwa nguvu. Taarifa hii pia ilitangazwa na TBC kupitia makala ya Hadubini.

“Nakupongeza sana Mkurugenzi Mkuu wa TBC, Dkt. Ayub Rioba na wafanyakazi wa TBC kwa kazi nzuri mnayoifanya, angalau nyinyi mnathubutu kujituma hadi vijijini kufuatilia mambo haya muhimu kwa jamii, nataka wizara na taasisi ambazo zina wataalamu na wasomi ziigeni mfano huu” amesema Mhe. Rais Magufuli.

Wakizungumza katika mkutano huo, Bw. Fute na Bw. Ngairo wamemshukuru Mhe. Rais Magufuli kwa kuwapa shilingi Milioni 5 ikiwa ni kutambua ubunifu wao na wameahidi kwenda kuboresha zaidi kwa kushirikiana na wataalamu wa Serikali.





Gerson Msigwa

Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU

Dar es Salaam

13 Juni, 2019
View attachment 1126395View attachment 1126396


Hawa wataalamu walikuwa wametelekezwa makusudi kwa sababu walihofiwa wangeweza kuvuruga dili! Umeme wa maji anaoutaka JPM ulikuwa hautakiwi nchi hii, watu walikuwa wanapendelea zaidi umeme wa Gas. Na ili uweze kujua Gas iko wapi, inabidi uwe na data za matetemeko. Waves propagation za earthquakes zina-obey laws of light propagation, kwamba huwa zinakuwa reflected na kuwa refracted pia. Kwa hiyo zinapokuwa zinapita kwenye medium fulani na zikawa refracted, then wataalamu watajua kuwa zimekuwa refracted na media ipi na kama ni oil au gas, bas watajua kwa kupima ile refractive index ya kile kilicho-refract waves hizo. In short this is how you can determine what an earthquake wave propagated through.
Kwa hiyo kama huna hizo earthquake data, inabidi utengeneze an artificial earthquake. Now connect the dots kwa nini watu hawataki kusikia umeme wa gas kwa kipindi hiki na wanataka wa maji, na kwa nini huko nyuma umeme wa gas ulikuwa unatakiwa na wa maji hautakiwi!

How Big Could a Man-Made Earthquake Get?

 
Hao wame copy. Umeme wangu mimi unazalishwa na magari yanayopita barabarani ni wa aina ya pekee duniani ni mimi tu ninao.
Cha pili nimegundua air cond. Ya Ndani ya nguo hasa sehemu za joto km Dsm.hawanijui wana nibagua
 
Back
Top Bottom