Ikulu, Dar: Rais Magufuli azungumza na Wabunifu wa mitambo midogo ya kufua umeme kwa kutumia maji ya mito

Vyuo vyetu vikuu havifanyi kazi inayotakiwa, watu wanafanya tafiti mbalimbali zinabaki kwenye makabati, kwanini wasomi wasifanye tafiti kulingana na mahitaji yetu ya ndani?
Hawa wenye Phd wengi wameingia kwenye siasa badala yake kutumia ujuzi wao kwenye kuliendeleza taifa mbele wao wamekuwa watu wa maslahi binafsi.
Well said👍🏽👏🏽
 
Kwa kweli niliangalia kile kipindi TBC kuhusu hawa jamaa mawili wanaozalisha umeme wa maji huko njombe maeneo ya vijijini na kuugawa bure umeme kwa wananchi.Nilivutiwa sana na ubunifu wao na jitihada zao za kuzalisha umeme na kuwagawia wanavijiji wenzao bure kabisa. Ila kusema ukweli hata mimi binafsi nilishangaa na kukasirika kiasi fulani pale ambapo meneja wa Tanesco Mkoa wa Njombe alipohojiwa na mwandishi wa habari kama anafahamu chochote kuhusu hhawa wabunifu na wazalishaji na meneja kukuri kutofahamu chochote lakini mbaya zaidi ni pale aliposema kwamba wanawasubiri hao wazalishaji waende ofisini (Tanesco) ndio wajadiliane nao.

Nilishangaa sana na kuwaza wamba kama ndio aina ya viongozi tulionao kwenye mashirika yetu basi tuna safari ndefu sana. Na si hili suala la umeme tu kuna wabunifu wengi sana ambao kama ubunifu wao ungethaminiwa na serikali na kuuendeleza uengeleta manufaa makubwa sna kwenye jamii yetu lakini NO BODY CARES!
 
Rais Magufuli leo 13 Juni, 2019 anakutana na Wabunifu wa mitambo midogo ya kufua umeme kwa kutumia maji ya mito

Kuanzia saa 3:30 Ikulu Jijini Dar es salaam





UPDATE
Rais Magufuli:
Nilifikiri kuwa Mkurugenzi wa TANESCO pamoja na Katibu Mkuu wangekuwepo hapa kusikiliza shida zao. Hawa ni mafundi ndiyo maana hawazungumzi sana.


Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia, Dkt. Amos Nungu
Hadi sasa jumla ya wabunifu 60 wameshatambuliwa na kuingizwa katika Kanzidata ya Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia

Mkurugenzi wa TANESCO, Dkt. Tito Mwinuka.
TANESCO imejipanga kutoa shilingi Milioni 30 kwa ajili ya wabunifu wawili wa mitambo midogo ya kufua umeme ili waongeze uzalishaji wa umeme huo

Tutawaendeleza wabunifu hawa wawili wa mitambo midogo ya kufua umeme kwa kuwaongezea shilingi Milioni 20 kwa ajili ya kuendeleza kazi zao

TANESCO imejipanga kutoa shilingi Milioni 30 kwa ajili ya wabunifu wawili wa mitambo midogo ya kufua umeme ili waongeze uzalishaji wa umeme huo

Rais Magufuli
Tatizo la Watanzania tunajidharau na hatuthamini vya kwetu, hawa wabunifu wa mitambo wangegunduliwa mapema wangepunguza gharama za uzalishaji umeme kwa sababu tayari wana chanzo cha umeme.

Wangekuwa wameshasaidiwa wasingefika hapa. Transfoma zingekuwepo, Mkurugenzi wa TANESCO kwao ni Njombe na nina uhakika huwa anaenda likizo huko lakini hajafanya lolote. Meneja wa TANESCO mkoa (Njombe) nimemsikia akizungumza hawa waje wanione kasha waende Ewura…yeye hakutaka shida.

Hata wangezalisha umeme ukaleta madhara shida isingekuwa kwa watendaji wa TANESCO kwa hiyo Mkurugenzi wa Njombe naye hajaleta taarifa yoyote kuhusiana na wagunduzi hawa tangu mwaka 1980.

Natoa siku saba kwa TANESCO kwenda katika eneo la mradi huo wa kufua umeme uliopo Mkoani Njombe na kuona ni namna gani utafanya kazi vizuri zaidi

Natoa wito kwa viongozi wote kuangalia Televisheni ya Taifa (TBC) ili kila kitakachoonyeshwa kuhusu wizara husika kikashughulikiwe kwa haraka.

Natoa shilingi Milioni Tano kwa wabunifu wawili wa mitambo midogo ya kufua umeme ili kuwaongezea mtaji katika shughuli zao.

Zaidi, soma;

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli tarehe 13 Juni, 2019 amekutana na wabunifu wawili wa kuzalisha umeme kwa kutumia maji ya mito kutoka Mkoani Njombe na kuagiza wataalamu wa wizara na taasisi zinazojihusisha na sayansi, teknolojia na uvumbuzi kuwafuatilia na wabunifu na wavumbuzi mbalimbali ili kuwaunga mkono katika kuboresha kazi zao.

Wabunifu waliokutana na Mhe. Rais Magufuli Ikulu Jijini Dar es Salaam ni John Akani Fute na Jairos Ngairo ambao wamebuni miradi ya kuzalisha umeme kwa kutumia maji yanayotiririka mtoni, kusukuma maji kwa kutumia pampu zisizotumia umeme na kusaga nafaka kwa kutumia machine zinazoendeshwa na maji ya mto. Bwana Fute amebuni mradi unaozalisha kilowati 28 na Bw. Ngairo anazalisha kilowati 15 za umeme.

Mkutano huo umewahusisha Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati Dkt. Hamis Mwinyimvua, Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dkt. Leonard Akwilapo, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara Bw. Ludovick Nduhiye pamoja na viongozi na wataalamu wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), Tume ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) na Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC).

Mhe. Rais Magufuli amewapongeza wabunifu hao kwa kuzalisha umeme wa gharama nafuu unaowanufaisha wananchi na ameagiza TANESCO na COSTECH kuwaunga mkono ambapo TANESCO itatoa shilingi Milioni 30 na COSTECH shilingi Milioni 20 kwa wabunifu hao, na pia timu ya wataalamu itaondoka kesho kwenda Njombe ilipo miradi hiyo kwa ajili ya kutoa ushauri wa kitaalamu na kuiboresha.

Mhe. Rais Magufuli ameelezea kutofurahishwa na vitendo vya wataalamu kuwakatisha tamaa na kuwatisha wabunifu wa vitu mbalimbali vinavyowasaidia wananchi kama ambavyo Bw. John Fute (Pwagu) na Bw. Jairos Ngairo wamekuwa wakifanyiwa na badala yake ametaka wabunifu hao waungwe mkono kwa ushauri wa kitaalamu na kuwawezesha kuongeza tija.

Mhe. Rais Magufuli ameipongeza TBC kwa kufuatilia kazi za ubunifu na uvumbuzi kupitia makala yake ya Hadubini (Habari kwa Kina) ikiwemo makala ya ubunifu wa mradi huo wa umeme iliyoandaliwa na waandishi wa Habari Bi. Tatu Abdallah na Bi. Zaituni Mkwama na ameagiza Wizara na Taasisi za Serikali kufuatilia taarifa zinazotangazwa na vyombo vya habari na kuchukua hatua katika maeneo yanayozihusu.

Ameiagiza Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kufuatilia jengo la ghorofa 3 linalodaiwa kutelekezwa na raia mmoja wa kigeni huko Kunduchi Jijini Dar es Salaam ambalo limebaki mikononi mwa mlinzi ambaye anatishwa na wajanja wanaotaka kujimilikisha kwa nguvu. Taarifa hii pia ilitangazwa na TBC kupitia makala ya Hadubini.

“Nakupongeza sana Mkurugenzi Mkuu wa TBC, Dkt. Ayub Rioba na wafanyakazi wa TBC kwa kazi nzuri mnayoifanya, angalau nyinyi mnathubutu kujituma hadi vijijini kufuatilia mambo haya muhimu kwa jamii, nataka wizara na taasisi ambazo zina wataalamu na wasomi ziigeni mfano huu” amesema Mhe. Rais Magufuli.

Wakizungumza katika mkutano huo, Bw. Fute na Bw. Ngairo wamemshukuru Mhe. Rais Magufuli kwa kuwapa shilingi Milioni 5 ikiwa ni kutambua ubunifu wao na wameahidi kwenda kuboresha zaidi kwa kushirikiana na wataalamu wa Serikali.

Vyombo vya uslama pamoja na baadhi ya wasaidizi wake ndiyo wanaomwaribia. Awasiliane na sisi wananchi moja kwa moja. Vikao kama hivi viendelee bila kukoma, hata ikibidi kila wiki!





Gerson Msigwa

Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU

Dar es Salaam

13 Juni, 2019
View attachment 1126395View attachment 1126396

Kusema kweli nimefurahishwa sana na rais kwenye hili. Ndiyo inavyotakiwa kuendesha hii nchi. Maghufuli avionye tu vyombo vya usalama visitumie fursa kunyanyasa wananchi na visasi. Maana huyu rais anahitaji support kubwa kabisa!
 
" Rais amewataka viongozi kuwa na utaratibu wa kuangalia runinga ya taifa na kufuatilia kitu chochote kitakachokuwa kinatolewa kinachohusu wizara zao ili waweze kuvifanya kazi".

We have a communication problem people!
 
Hii safi
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli tarehe 13 Juni, 2019 amekutana na wabunifu wawili wa kuzalisha umeme kwa kutumia maji ya mito kutoka Mkoani Njombe na kuagiza wataalamu wa wizara na taasisi zinazojihusisha na sayansi, teknolojia na uvumbuzi kuwafuatilia na wabunifu na wavumbuzi mbalimbali ili kuwaunga mkono katika kuboresha kazi zao.
Wabunifu waliokutana na Mhe. Rais Magufuli Ikulu Jijini Dar es Salaam ni John Akani Fute na Jairos Ngairo ambao wamebuni miradi ya kuzalisha umeme kwa kutumia maji yanayotiririka mtoni, kusukuma maji kwa kutumia pampu zisizotumia umeme na kusaga nafaka kwa kutumia machine zinazoendeshwa na maji ya mto. Bwana Fute amebuni mradi unaozalisha kilowati 28 na Bw. Ngairo anazalisha kilowati 15 za umeme.
Mkutano huo umewahusisha Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati Dkt. Hamis Mwinyimvua, Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dkt. Leonard Akwilapo, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara Bw. Ludovick Nduhiye pamoja na viongozi na wataalamu wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), Tume ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) na Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC).
Mhe. Rais Magufuli amewapongeza wabunifu hao kwa kuzalisha umeme wa gharama nafuu unaowanufaisha wananchi na ameagiza TANESCO na COSTECH kuwaunga mkono ambapo TANESCO itatoa shilingi Milioni 30 na COSTECH shilingi Milioni 20 kwa wabunifu hao, na pia timu ya wataalamu itaondoka kesho kwenda Njombe ilipo miradi hiyo kwa ajili ya kutoa ushauri wa kitaalamu na kuiboresha.
Mhe. Rais Magufuli ameelezea kutofurahishwa na vitendo vya wataalamu kuwakatisha tamaa na kuwatisha wabunifu wa vitu mbalimbali vinavyowasaidia wananchi kama ambavyo Bw. John Fute (Pwagu) na Bw. Jairos Ngairo wamekuwa wakifanyiwa na badala yake ametaka wabunifu hao waungwe mkono kwa ushauri wa kitaalamu na kuwawezesha kuongeza tija.
Mhe. Rais Magufuli ameipongeza TBC kwa kufuatilia kazi za ubunifu na uvumbuzi kupitia makala yake ya Hadubini (Habari kwa Kina) ikiwemo makala ya ubunifu wa mradi huo wa umeme iliyoandaliwa na waandishi wa Habari Bi. Tatu Abdallah na Bi. Zaituni Mkwama na ameagiza Wizara na Taasisi za Serikali KufuatiliaView attachment 1126406
 
Pumbavu kabisa! Eti mapumbavu yanaulizia CV! Yani hiyo habari kidogo initoe machozi ya gadhabu! Miafrika tunakwamishana wenyewe! Rais ajifunze sasa kujaza hao wenye phd si solution kwenye hii nchi! Yani hadi mjerumani ndiyo amekuja kumthamini darasa la saba!

Na hilo jamaa lenye miwani, linalo ile mentality ya kutaka litumikiwe badala lenyewe ndo liwatumikie wananchi, lenyewe kukaa ofisini na kubweka maamuzi tu! ningekuwa rais ningelitimulia mbali. Pambaaf kabisa😡
 
“Tanesco hakikisheni mnaondoka na hawa waliozalisha umeme kwenda kuangalia hiyo mitambo na kuweka kinga maana mlitakiwa muwape ushirikiano kuanzia mwanzo lakini hamkufanya hivyo, na wasiondoke na basi kama walivyokuja mchukue magari yenu yenye nembo ya Tanesco,” amesema


"Na wapulizwe kiyoyozi mpaka mwisho wa safari" :D alisisitiza
 
Wabunifu hao wamekabidhiwa shilingi milioni 7.5 kila mmoja kutoka kwa rais Magufuli huku Tanesco wakiahidi kutoa shilingi milioni 15 kwa kila mmoja, nayo Tume ya Sayansi na Teknolojia Tanzania (COSTECH) imeahidi kutoa shilingi milioni 10 kwa kila mmoja kama kianzio cha kuwasaidia wabunifu hao kujiendeleza.


Hapa umedanganya kabisa, Rais amewakabidhi kila mmoja Milioni 2.5 (ametoa 5M kwa wote wawili na akasema wagawane
 
Da, Mwinuka amepata taabu sana!


Najaribu kufikiria hali aliyokuwa nayo meneja wa Tanesco mkoa wa Njombe baada ya kusema alikuwa anawasubiri ofisini kwake badala ya yeye kwenda site.

Nahisi kama alikuwa anafuatilia session ile Ikulu atakuwa alijifunga mipira miguuni mithili ya wale wanaotumia pombe aina ya wanzuki
 
Yani jamaa hadi nyaya amechoma matairi kuzipata, halafu kuna wajinga wako maofisini kwenye viyoyozi wanatafuna kodi zetu!🤢 Halafu wanabana pua “walete CV”, huku mjerumani yeye anasaidia! Umasikini wetu umechangiwa na ujinga wetu na si kitu kingine chochote!

Halafu Maghufuli lazima ni member humu. Amenifurahisha sana kwenye kuelezea “an educated person” watu wana mavyeti lakini ni wajinga waliopewa nafasi ya kutuongoza!

Maendeleo ya waafrika yataletwa na sisi waafrika wenyewe. This is something I have learned in my entire life. Hakuna anayetupenda, si mzungu, si mchina, si muindi, wote wanatuchukia.
 
Kwa kweli niliangalia kile kipindi TBC kuhusu hawa jamaa mawili wanaozalisha umeme wa maji huko njombe maeneo ya vijijini na kuugawa bure umeme kwa wananchi.Nilivutiwa sana na ubunifu wao na jitihada zao za kuzalisha umeme na kuwagawia wanavijiji wenzao bure kabisa. Ila kusema ukweli hata mimi binafsi nilishangaa na kukasirika kiasi fulani pale ambapo meneja wa Tanesco Mkoa wa Njombe alipohojiwa na mwandishi wa habari kama anafahamu chochote kuhusu hhawa wabunifu na wazalishaji na meneja kukuri kutofahamu chochote lakini mbaya zaidi ni pale aliposema kwamba wanawasubiri hao wazalishaji waende ofisini (Tanesco) ndio wajadiliane nao.

Nilishangaa sana na kuwaza wamba kama ndio aina ya viongozi tulionao kwenye mashirika yetu basi tuna safari ndefu sana. Na si hili suala la umeme tu kuna wabunifu wengi sana ambao kama ubunifu wao ungethaminiwa na serikali na kuuendeleza uengeleta manufaa makubwa sna kwenye jamii yetu lakini NO BODY CARES!
Viongozi wote kwenye mashirika ya umma hawafai hata kidogo! Ni kufumulia uongozi mbali na kuweka watu ambao ni “proactive”, wasiokaa maofisini, walioelimika, na wenye uchungu na hii nchi.
 
Pumbavu kabisa! Eti mapumbavu yanaulizia CV! Yani hiyo habari kidogo initoe machozi ya gadhabu! Miafrika tunakwamishana wenyewe! Rais ajifunze sasa kujaza hao wenye phd si solution kwenye hii nchi! Yani hadi mjerumani ndiyo amekuja kumthamini darasa la saba!

Na hilo jamaa lenye miwani, linalo ile mentality ya kutaka litumikiwe badala lenyewe ndo liwatumikie wananchi, lenyewe kukaa ofisini na kubweka maamuzi tu! ningekuwa rais ningelitimulia mbali. Pambaaf kabisa😡
Ujue waafrica tunamtafuta mchawi wa maendeleo lkn kumbe yupo kwenye fikra zetu.
Ndiomana kuna wakati nafikiria kama tunaweza kumpata tena kiongozi mwenye falsafa kama ya huyu mzee, atakapo maliza muda wake.
 
Kuita na kuongea na watuwa fanimbalimali bila kutatua kero zao,kuweka mipango ya kuwatumia ipasavyo ,kuandaa mahitaji yao na soko ni kazi bure .
 
Kwa kitendo cha kugawa bure ndio Mungu aliwabariki na sasa wamelipwa Mungu ana njia zake.
Big up JPM najua hii pia sababu Rais kuwa serious na issue hii ila hawa tanesco Njombe ni MAZUZU sana
 
Back
Top Bottom