Ijue siri ya kucheza mpira wa umiliki mpira, yaani boli kutembea

SAYVILLE

JF-Expert Member
Mar 25, 2010
5,129
7,898
Kumekuwa na kelele nyingi sana kuhusu Simba kucheza mpira usiovutia, au wengine wanaita papatu papatu. Kuna wengine wamekuwa wanasifia uchezaji wa Yanga hivi sasa. Ngoja niwagusie mbinu mojawapo ninayoijua mimi ya kuwajenga wachezaji kuweza kucheza mpira wa umiliki yaani possession football.

Kuna zoezi fulani ambalo wachezaji wanakaa kwenye duara wanapasiana, halafu mchezaji mmoja au zaidi wanakuwa wanapambana kuugusa mpira. Ukiugusa, yule aliyepoteza anaingia kati. Najua wote mnaujua huu mchezo. Zoezi hili linaitwa "Rondo".

Kwa muda mrefu nimekuwa nafuatilia jinsi timu za Tanzania zinavyofanya hili zoezi. Ni zoezi ambalo nadhani kwa wachezaji na timu za Tanzania halijaeleweka faida zake, ni kama zoezi ambalo wengi wanafanya kama la kujifurahisha tu kusubiri mazoezi mengine ila lina faida kubwa katika kumjengea mchezaji uwezo wa kutoa pasi za uhakika kwa haraka na uwezo wa kufikiri.

Moja ya kitu nilichogundua kwa Simba ni kuwa hili zoezi wanalifanya sana ila wachezaji hawako vizuri kabisa, wachezaji hawawezi kumiliki mpira bila kuupoteza kwa muda mfupi sana. Huwezi kuona video ya mazoezi ya Simba uwanjani usione wakifanya Rondos. Yanga huwa nikiangalia mazoezi ni nadra sana kuona wakionyesha rondos zao ambalo ni jambo la kushangaza ila nakumbuka kila nikiziona niligundua wachezaji wake wako vizuri sana kwenye hili zoezi. Siri inaanzia hapa.

Hii hapa ni video ya mazoezi ya Simba ya leo tu wakifanya rondo. Ukiingia kwenye channel ya Simba ukatafuta video yoyote wanayofanya mazoezi, utaliona hili ninalolisema. Wachezaji wanakosa umakini wa kukaa na mpira na kutoa pasi bila kupoteza. Sisemi wachezaji wa Simba hawana uwezo, ila nadhani kuna hali fulani ya kurelax na matokeo yake bongo zao zinafubaa inafika kwenye mechi wanakosa ile usharp wa akili unaohitajika.


View: https://www.youtube.com/watch?v=7Dq9cA3oc_c

Linganisha na Rondos za timu zinazojulikana kwa kucheza possession football kama Barcelona au Manchester City.

Hizi hapa Rondos za Barcelona (unaweza kuzipata nyingi Youtube)


View: https://www.youtube.com/watch?v=oofexHQGCbM


View: https://www.youtube.com/watch?v=UUV5gbknTG0


Hii hapa rondo ya Manchester City


View: https://www.youtube.com/watch?v=--cyAUmN85w


Mtu akipata rondo yoyote ya Yanga ya hata kipindi cha Nabi aiweke mtaona ninachokisema ni nini.
 
Wachezaji ndio tatizo, shabalala akipata mpira lazima aupooze ama akimbie nao au atoe pasi lakini lazima aupooze mpira, Mzamiru akipata mpira lazima azunguke halafu apige pasi ndefu ambazo Mara nyingi zinapotea, Inonga naye akikokota mpira anawaza kupiga pasi ndefu hata Kama zitapotea hajali, Saidoo akipata mpira anawaza kukokota na kupiga mashuti , tabia huyo anayo Kibu Dennis akipata mpira anawaza kukimbia huku anaangalia chini kwa Aina ya wachezaji Hawa ni vigumu kucheza pasi ndio maana walipoingia Phiri, Kanoute, Konde boy mpira ulibadilika.
 
Nimejaribu kuangalia Mechi ya marudiano Simba na Dynamo mchezo WA Simba Day.

Nimeumia sana Kuona Simba wanashindwa kufikisha hata pasi 5 za uhakika.

1. Nitoe somo kwa MLETA mada kuwa Ili timu icheze inahitaji kuwa na kiungo mzuri mno , mwenye uwezo Mkubwa WA kupiga pass. 6,8,10
Bangala na Aucho.
HAPA NDIO KWENYE Roho ya Timu.

2. Ili mcheze kwa kuonana Huwa tunaita Triangle Lazima wachezaji wajue Kutengeneza pembeni Tatu wawapo uwanjani
Rejea Barca ya pep na man city.

Nitarudi kesho kutoa Darasa
 
Unataka kusema nini unapoingiza matatizo yenu binafsi na maswala ya Yanga? Uzi wako u stick kwa Simba na mapungufu yenu. Habari ya Yanga kufanya mazoezi ya Rondo au kutokufanya hayakuhusu kwasababu sio video zinazowekwa mtandaoni zitaonesha kila kitu. La pili Yanga kwanzia kipindi cha Nabi, wachezaji walikuwa wanauwezo wa kumiliki mpira, na kupiga pasi kwa usahihi. Kaja kocha mpya napo wachezaji wameongezewa vitu vitu zaidi saivi wamekuwa kama wana sumaku miguuni, wanajiamini na wana utulivu mkubwa. Sasa usitake kujua ni aina gani ya mazoezi wanayofanya.
 
Unataka kusema nini unapoingiza matatizo yenu binafsi na maswala ya Yanga? Uzi wako u stick kwa Simba na mapungufu yenu. Habari ya Yanga kufanya mazoezi ya Rondo au kutokufanya hayakuhusu kwasababu sio video zinazowekwa mtandaoni zitaonesha kila kitu. La pili Yanga kwanzia kipindi cha Nabi, wachezaji walikuwa wanauwezo wa kumiliki mpira, na kupiga pasi kwa usahihi. Kaja kocha mpya napo wachezaji wameongezewa vitu vitu zaidi saivi wamekuwa kama wana sumaku miguuni, wanajiamini na wana utulivu mkubwa. Sasa usitake kujua ni aina gani ya mazoezi wanayofanya.
Nafikiri mleta mada ameelezea analolijua ni hekima isiyohitaji elimu kuheshimu mawazo ya mtu, nafikiri tujikite kwa mada iliopo mezani
 
Wachezaji ndio tatizo, shabalala akipata mpira lazima aupooze ama akimbie nao au atoe pasi lakini lazima aupooze mpira, Mzamiru akipata mpira lazima azunguke halafu apige pasi ndefu ambazo Mara nyingi zinapotea, Inonga naye akikokota mpira anawaza kupiga pasi ndefu hata Kama zitapotea hajali, Saidoo akipata mpira anawaza kukokota na kupiga mashuti , tabia huyo anayo Kibu Dennis akipata mpira anawaza kukimbia huku anaangalia chini kwa Aina ya wachezaji Hawa ni vigumu kucheza pasi ndio maana walipoingia Phiri, Kanoute, Konde boy mpira ulibadilika.
Exactly, issue ipo kwa wachezaji. Wanahitaji utimamu na utulivu wa akili na kuboresha footwork yao. Ushauri wangu watumie mazoezi ya rondo kwa umakini zaidi.

Rondo ni moja ya mazoezi yanayopendwa sana na Pep Guardiola katika kuwajenga wachezaji wake.
 
Back
Top Bottom