Wengine hili janga la derby ya leo tuliliona linakuja kitambo

SAYVILLE

JF-Expert Member
Mar 25, 2010
5,151
7,918
Wakati wengine wanaangalia tu matokeo ya uwanjani na timu inavyocheza, wengine tumekuwa tunaangalia mazoezi ya Simba na kuanza kuona mapungufu ya kitimu kuanzia huko.

Nakumbuka kuleta uzi nikikumbushia umuhimu wa "Rondo" katika kutengeneza wachezaji wenye uwezo wa kumiliki mpira. Hilo ni zoezi moja tu ila wachezaji wa Simba wanaonyesha mapungufu yao kuanzia mazoezini. Yanga wako serious sana kuanzia mazoezini hadi katika mechi zao. Simba kuna mizaha mingi na mambo ya hovyo hovyo yanaendekezwa katika ngazi zote.

Mapungufu na matatizo yaliyoonekana leo kwa Simba na ubora ulioonyeshwa leo na Yanga ni matokeo ya kile kilichokuwa kinafanyika kwenye uwanja wa mazoezi kwa muda sasa. Nilijua mazingira yanatengenezwa kwa Simba kuja kufungwa goli nyingi na mtani wake na si kwa sababu ya hujuma bali kuzidiwa mchezo.
 
Hilo RONDO akina SAIDO, KANOUTE na KIBU nao wanatakia wawepo maana hawa jamaa ni "ma-one man army",,, yaani wazee kwa ku_dribble na mara nyingi wanaishia kupoteza mipira...

In short utatu wa PACOME, AZIZ na ZENGELI umewaacha mbali sana CHAMA, SAIDO na KIBU na ndo NGUVU ya YANGA na udhaifu wa SIMBA ulipo...
 
Tulale Sasa imetosha
Na Bado mpaka mseme!

GAMONDI ana roho mbaya sana yaani kwa akili zake timamu eti kaamua kabisa kuua Mbu (Simba) kwa gobole!
Mara nasikia kaagiza makombora mengine ya nyuklia eti ya Jana 5G hakuridhika ye alitaka kufanya udhalilishaji mkubwa zaidi kwa Yanga kuua Makolo wiki nzima ( 7G - 0)
 

Attachments

  • VID-20231105-WA0025.mp4
    3.4 MB
.
20231106_140633.jpg
 
Wakati wengine wanaangalia tu matokeo ya uwanjani na timu inavyocheza, wengine tumekuwa tunaangalia mazoezi ya Simba na kuanza kuona mapungufu ya kitimu kuanzia huko.

Nakumbuka kuleta uzi nikikumbushia umuhimu wa "Rondo" katika kutengeneza wachezaji wenye uwezo wa kumiliki mpira. Hilo ni zoezi moja tu ila wachezaji wa Simba wanaonyesha mapungufu yao kuanzia mazoezini. Yanga wako serious sana kuanzia mazoezini hadi katika mechi zao. Simba kuna mizaha mingi na mambo ya hovyo hovyo yanaendekezwa katika ngazi zote.

Mapungufu na matatizo yaliyoonekana leo kwa Simba na ubora ulioonyeshwa leo na Yanga ni matokeo ya kile kilichokuwa kinafanyika kwenye uwanja wa mazoezi kwa muda sasa. Nilijua mazingira yanatengenezwa kwa Simba kuja kufungwa goli nyingi na mtani wake na si kwa sababu ya hujuma bali kuzidiwa mchezo.
🗣️ sema baba! Wewe sema tu!! Usiogope!!
 
Dah we jamaa ulivo mnazi kishamba hujawahi kuona baya la simba, kama uliona mapungufu mbona hukuwahi kuja na uzi hata wa tahadhari hapa?

Atusaidie Uzi mmoja tu wa hayo mapungufu. Zaidi ya CAPO na GENTA Hakuna mwanasimba mwingine aliyewahi kukosoa usajili, uchezaji na Wachezaji wa Simba.
Fuatilia nyuzi zangu nyingi tu na post zangu katika nyuzi zingine, nimekosoa benchi la ufundi, viongozi na baadhi ya wachezaji hadi nimekuwa naambiwa nina chuki binafsi dhidi yao. Nyuzi zangu za mwisho mwisho nilikuwa nakumbushia kuwa nimekaa pembeni kwenye masuala haya ya mpira kwa sababu nilikuwa naona janga linalokuja. Hao mnaotaja wanakujaga kucopy na kupaste kile ambacho nakuwa nimeshakiandika.
 
Back
Top Bottom