Bilionea Asigwa
JF-Expert Member
- Sep 21, 2011
- 16,587
- 28,749
Safi sana, tukienda hivi tutafika mbali sana aiseeeMkuu kwenye majeshi hakuna mihemko kule..unakumbuka Waziri Kitwanga alipoliagiza jeshi kufanya operesheni ya kusafisha majambazi kwa kuvamia mapori ya Mbagala..Siku iliyofuata Kamati ya Ulinzi na Usalama ikamuambia hakunaga amri kama hizo kwenye mambo kama hayo kuna taratibu zake..Lile agizo lilifia palepale. Kwenye Majeshi huwezi kupanda cheo bila ya kurudi kozi na kuburuzwa upya..
Hapana mkuu zawadi haipaswi kua na masharti...kwani askari huyo alihitaji cheo kwa sasa?Ila Mangu anamtakia mema askari , aende akasome ili zawadi iwe na tija huko mbeleni asije kutokea wa kumnyanyasa
Wanaandika tu bila kufahamu nafasi ya rais katika majeshi, Rais anauwezo wa kumpandisha cheo askari au kumshusha kwa mamlaka aliyopewa na mkuu wake asipinge. Hii ya mangu sina hakika kama kweli kasema hayo.Kwan yule jamaa aliyewadhibiti majambazi pale Ubungo kipindi kile, alienda mafunzon ndiyo akapandishwa cheo? SMH!
Kwa ufahamu wangu mdogoMdau nadhani hili swala ww umelitafsili kwa angle yako kadiri ulivyolielewa ww . Mangu hakuna kitu alichokosoa, Kifupi ni kwamba Serekali huwa inawasiliana kwa maandishi.......ili Mangu aweze kutekeleza maelekezo ya Mh Rais lazima apewe barua ya kumtaka afanye alichoagizwa...... na yy wakati anatekeleza aliyoagizwa ni Iazima afate utaratibu wa kupandisha askari vyeo...... at the end of the day.... yule askari atapandishwa cheo kwa mujibu wa maelekezo lakini kwa kuzingatia utaratibu.
Anasubiri agizo la kiofisi ndio achukue hatua.Raia mna matatizo sana.kwa kifupi magufuli ni amir jeshi mkuu,neno lake ni amri,huyo mangu amejitoa ufahamu tu kwa vile anajua nae hana muda mrefu kuachia hicho cheo cha uIgp.
Safi sana, tukienda hivi tutafika mbali sana aiseee
Kwa mtazamo wangu Mangu kafanya kilichowashinda wengi na hii yaweza kuwa chache ya mwamko mpya wa kutenda kulingana na taratibu tulizojiwekea wenyeweAnasubiri agizo la kiofisi ndio achukue hatua.
Heri ahesabu siku zake ila hiki kisa?Wangapi wanatukana askari?Waza tu kawaida?Au kwa kuwa mke wa waziri?Tunapoelekea zitatoka amri au maagizo yasiyo na ujazo na yakaathiri nji mdogomdogo.Angali tu bei ya sukari ilipo sasa..hizo hizo amri amri..Sijawahi kuona amri ya mkuu wa majeshi inakuwa compromised...huyu jamaa ahesabu siku zake tu
Tatizo la wanahabari wa kibongo wengi hawajui uwandishi hivyo Mungu anawajua ndio aliwakaushiaMangu is not a good person, Ana tabia ya upendeleo hata akiwa kazin, mwaka 2013 akiwa RPC, mwanza Kuna askari aliua raia kwa makusudi, lakin sisi Kama wanahabari tulihitaji kujua msimamo wake kwa askari yule lakin alipiga kimya Ili kulinda jeshi lake, angeangalia upande wa pili wa haki za binadamu
Kwa ufahamu wangu mdogo
amri ya rais haihitaji kuwasilishwa kwa maandishi,,,utekelezaji wake huanza pale tu anapomaliza kuzungumza na wahusika wanatakiwa kuitekeleza mara moja ,hayo mengine hufuata baada ya kuanza utekelezaji
Ni vizuri kusimamia sharia...kuna kitu kinaitwa precedence...akimpandisha huyu cheo atakuja mwingine kesho na kudai kupandishwa cheo kwa vile naye katukanwa...ukikataa unakuwa hauko fair kwa taratibu za kazi...kwa uufupi ni kama ku redefine vigezo vya kupandishwa vyeo...je itakuwa sahihi? ha ha ha tutaanza kuona kila askari na recorder....
hahahhhha...Mzukaaaa umepanda mzukaaa umeshukaaaa..weraaa weraaaa
JF noma sana!
Unajua kilichomkuta Kamanda mmoja wa USA kwa kupishana Kauli na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama!
Tangazo la Raisi ni Amri hali hitaji taarifa ya Kimaandishi na hasa hili la majeshi ya Ulinzi na Usalama!
Huyu wa kwetu kapandishwa cheo kwasababu ya......! Tanzania raha sanaAmiri Jeshi Mkuu kwa mujibu wa sheria na kanuni za majeshi yote, anayo mamlaka ya kumpandisha cheo askari yoyote kwa sababu atakayooba inamstahiki mtu yule kupandishwa cheo. Wanajeshi, Askari Magereza na Pilisi hupandishwa vyeo kutokana na kufanya jambo lolote lililotukuka katika kesho au kwa nchi. Philbert alipanda mpaka kuwa captain baada ya kuvunja rekodi ya dunia. Bondia Nassoro Michael alipanda cheo baada ya kutwaa medali Jumuiya ya Madola. Hata nchi nyingine utaratibu huo pia unatumika. Chris Katongo wa Zambia alipandishwa cheo baada ya kuiongoza Chipolopolo kuchukua ubingwa wa AFCON.nk, nk
Amir maana yake ni kamanda.kuna kamanda wa kawaida na kamanda mkuu so kwa upeo wangu yupo sahihi kusema amiri jeshi mkuu.Kiswahili sanifu ni AMIRI JESHI usiweke tena neno MKUU kwasababu neno AMRI ni neno la kiaraabu likimaanisha neno MKUU, kwa hiyo ukisema AMIRI JESHO MKUU ni sawa na kusema BARABARA YA MOROGORO ROAD
Kuna polisi alipandishwa cheo pia baada ya mwandishi Daudi Mwangosi kupoteza uhai. Nimesahau jina lake lkn Dr. Slaa alikuwa analitaja saaaaanaKwan yule jamaa aliyewadhibiti majambazi pale Ubungo kipindi kile, alienda mafunzon ndiyo akapandishwa cheo? SMH!