Hii imetokea leo Shule ya Sekondari Ifuunda Tech iliyoko mkoani Iringa majira ya saa nane mchana baada ya wanafunzi kuvunja baadhi ya samani za shule ikiwemo vioo na kuiba kengele na kuificha kusikojulikana.
Chanzo cha fujo hizo inasemekana ni walimu kuwachapa viboko zaidi ya 15 kwa wanafunzi waliochelewa kufika parade. Inasemekana maji yalikatika hivyo wanafunzi kulazimika kufuata maji mbali kidogo na shuleni hivyo kuwafanya wachelewe parade.
Hiyo ndio sababu kuu iliyowafanya waibe kengele na kufanya uharibifu na uongozi wa shule kwa kushirikiana na afisa elimu kuifunga shule hiyo na wanafunzi walipewa nusu saa wawe wameondoka eneo la shule vinginevyo polisi waliokuwa wamesheheni silaha na gari za washawasha wangewashugulikia.
Chanzo cha fujo hizo inasemekana ni walimu kuwachapa viboko zaidi ya 15 kwa wanafunzi waliochelewa kufika parade. Inasemekana maji yalikatika hivyo wanafunzi kulazimika kufuata maji mbali kidogo na shuleni hivyo kuwafanya wachelewe parade.
Hiyo ndio sababu kuu iliyowafanya waibe kengele na kufanya uharibifu na uongozi wa shule kwa kushirikiana na afisa elimu kuifunga shule hiyo na wanafunzi walipewa nusu saa wawe wameondoka eneo la shule vinginevyo polisi waliokuwa wamesheheni silaha na gari za washawasha wangewashugulikia.