Azizi Mussa
JF-Expert Member
- May 9, 2012
- 9,172
- 7,429
Idara ya Usalama wa Taifa (TISS) ni miongoni mwa Taasisi nyeti kabisa nchini kutokana na umuhimu wa majukumu yake.
Umuhimu wake unakuja kutokana na sabababu kwamba; nchi yeyote ile ni lazma iwe na maadui wa ndani na nje na ili nchi hiyo ipate kustawi, basi ni lazma maadui hao wadhibitiwe.
Baadhi ya maadui wanao hujumu nchi (wawe wa ndani au nje) wanaweza kufanya shughuli zao kwa siri sana lakini kwa ufanisi mkubwa na mazingira na mitandao wanayotumia kufanya uhalifu inaweza kuwa yenye utata na usiri mkubwa kiasi kwamba Jeshi la polisi kulingana na muundo wake haliwezi kugundua njama hizo bila kupata msaada wa vyombo vingine.
Kadhalika viongozi wa nchi huhitajika kufanya maamuzi wakiwa na taarifa za kutosha hivyo ni lazma wawe na njia inayoweza kuwapa taarifa juu ya mambo kadhaa ili wafanye maamuzi "With informed mind".
Pamoja na kuwepo kwa Taasisi hii inayoogopwa na wengi, kumekuwa na matukio mengi ambayo ni hatari kwa usalama wa nchi kama vile Ujangili wa Tembo, Usafirishaji wa wanyama Hai nje ya Nchi,Ulipuaji wa mabomu ya kuua, Kuongezeka kwa ufisadi,Ufichaji wa fedha nje ya nchi,Uingizaji wa fedha chafu kwenye mzunguko,Rushwa kwenye mambo nyeti ya kitaifa na mambo mengine mengi ambayo kwa pamoja yanahatarisha usalama wa nchi yetu.
Kwa mujibu wa sheria iliyounda taasisi hii (TISS) ,yaani ; "TANZANIA INTELLIGENCE AND SECURITY SERVICE ACT 1996", Unakuta taasisi hii haipaswi kulaumiwa kwa kile kinachotokea nchini. Hii ni kwa sababu; kwa mujibu wa sheria hii,Taasisi hii imepewa majukumu ya kukusanya taarifa, kuzichambua, na kisha kushauri.
Wanaoshauriwa wanakuwa ni viongozi wa siasa wanaotokana na vyama vya siasa (Rais na Mawaziri) ambao licha ya kuwa viongozi wa kitaifa ; pia wanakuwa wamebeba ajenda zao za kisiasa,ajenda za vyama vyao na dhamira zao binafsi (ambazo zaweza kuwa za afya kwa taifa au hatari kwa Taifa). Kwa hiyo basi; Chombo hiki kinapokuwa kimemaliza majukumu tajwa hapo juu kwa kuishia na "kushauri"Kinakuwa kimemaliza majukumu yake kisheria (Bila kujali kama ushauri wake utafuatwa au laa) na hakipaswi kulaumiwa kwa kuwa sheria hairuhusu kufanya zaidi ya hapo.
Katika mazingira kama haya (ya kuipa TISS) Mamlaka kidogo namna hii, kimsingi kuna mambo mengi yanaweza kuhatarisha usalama wa nchi na huku kukiwa hakuna maelekezo ya kutosha ya kisheria kwamba nani afanye nini.Kwa mfano; Milipuko ya mabomu kwenye mkutano wa CHADEMA Arusha; Upo uwezekano kwamba TISS Walijua, pengine wakashauri, na ushauri wao ukapuuzwa.(kama ambavyo naamini walikuwa wanajua kuhusu suala la kusafirishwa kwa Twiga hai lakini bado Twiga walisafirishwa). Kimsingi kama suala la Arusha lilikuwa ni tukio la kisiasa kama baadhi ya watu wanavyo sema,na ikiwa watekelezaji ni CCM; TISS, Kushauri ingekuwa ni sawa na kumshawishi boss wao asitekeleze kile anachodhani anatakiwa kutekeleza. Kwa hakika katika mazingira haya, inawezekana kabisa kwamba chombo hiki kinatekeleza majukumu yake lakini pamoja na hivyo matukio ya kuhatarisha usalama yanatokea kutokana na udhaifu wa kisheria.
Kwa kuendelea na sheria hii (1996) bado vyama vya siasa,Viongozi wa kisiasa, na baadhi ya watu wanaweza kuwa na nguvu kuliko TISS; Yaani TISS, inaweza kukusanya taarifa,kuzichambua na kuwashauri ila wakakataa ushauri na kutenda kinyume na kuvuruga usalama wa nchi.Katika mazingira haya upo uwezekano siku moja nchi ikaelekea tusiko kutegemea kwa kuwa si lazma kila mwanasiasa awe na nia ya dhati ya kuipeleka nchi mbele kwa kuwa viongozi wa kisiasa hupatikana kwa bahati nasibu kutoka katika jamii (jamii yenye watu wema na wabaya).
Katika mazingira haya mfanyabiashara mmoja wa madawa ya kulevywa anaweza kugombea ubunge, baada ya kupata ubunge akapewa uwaziri mkuu (by chance), baada ya kupewa uwaziri mkuu akawa anatumia nafasi yake serikalini na kinga za kiungozi kufanya mambo yenye manufaa kwake lakini hatari kwa taifa,TISS wakamshauri lakini akakataa.
Kimsingi taasisi hii ya Usalama wa Taifa sasa inatakiwa kupewa mamlaka zaidi na kuruhusiwa kuzuia matukio yoyote yanayoonekana kuwa ni tishio kwa usalama wanchi bila kujali mfanyaji ni nani(Wawe na nguvu ya juu kabisa katika masuala yanayoweza kuhatarisha usalama).Inatakiwa tuwe na dira,misingi na maadili ya taifa ambayo ni lazma yafatwe na kila mtu (kuanzia Rais na wengine wote) na mamlaka ya kuhakikisha kwamba misingi hiyo inafuatwa wapewe TISS. Hii itawasaidia kuwa na mmlaka kamili ya kutekeleza majukumu yao kama lilivyo jina la Taasisi yenyewe. Baada ya kukipa mamlaka hayo chombo hiki, mambo kama vile kuficha fedha nje, umafia kwenye siasa na mambo mengine kama mitandao ya madawa ya kulevya yanaweza kudhoofishwa sana hata kama yanafanywa na vigogo wazito.
Swali la kizushi:
Kama msajili wa vyama vya siasa anasema ikibainika kuwa waliolipua bomu Arusha ni CHADEMA atakifuta CHAMA, Lakini kama ikibainika ni CCM; Kwa kuwa ni chama tawala atakishauri. Je! ushauri wa Tendwa unaweza kuwa na nguvu kuliko wa TISS, na hivyo kuwa ni lazma ukubalike? Ikiwa sio, Je ikibainika ni CCM, halafu akawa shauri na wakakataa, TISS wakawashauri wakakataa, ni nani wakuwadhibiti? Je! Hali itakayofuata baada ya hapo itakuwa ya afya kwa nchi yetu kweli?
Umuhimu wake unakuja kutokana na sabababu kwamba; nchi yeyote ile ni lazma iwe na maadui wa ndani na nje na ili nchi hiyo ipate kustawi, basi ni lazma maadui hao wadhibitiwe.
Baadhi ya maadui wanao hujumu nchi (wawe wa ndani au nje) wanaweza kufanya shughuli zao kwa siri sana lakini kwa ufanisi mkubwa na mazingira na mitandao wanayotumia kufanya uhalifu inaweza kuwa yenye utata na usiri mkubwa kiasi kwamba Jeshi la polisi kulingana na muundo wake haliwezi kugundua njama hizo bila kupata msaada wa vyombo vingine.
Kadhalika viongozi wa nchi huhitajika kufanya maamuzi wakiwa na taarifa za kutosha hivyo ni lazma wawe na njia inayoweza kuwapa taarifa juu ya mambo kadhaa ili wafanye maamuzi "With informed mind".
Pamoja na kuwepo kwa Taasisi hii inayoogopwa na wengi, kumekuwa na matukio mengi ambayo ni hatari kwa usalama wa nchi kama vile Ujangili wa Tembo, Usafirishaji wa wanyama Hai nje ya Nchi,Ulipuaji wa mabomu ya kuua, Kuongezeka kwa ufisadi,Ufichaji wa fedha nje ya nchi,Uingizaji wa fedha chafu kwenye mzunguko,Rushwa kwenye mambo nyeti ya kitaifa na mambo mengine mengi ambayo kwa pamoja yanahatarisha usalama wa nchi yetu.
Kwa mujibu wa sheria iliyounda taasisi hii (TISS) ,yaani ; "TANZANIA INTELLIGENCE AND SECURITY SERVICE ACT 1996", Unakuta taasisi hii haipaswi kulaumiwa kwa kile kinachotokea nchini. Hii ni kwa sababu; kwa mujibu wa sheria hii,Taasisi hii imepewa majukumu ya kukusanya taarifa, kuzichambua, na kisha kushauri.
Wanaoshauriwa wanakuwa ni viongozi wa siasa wanaotokana na vyama vya siasa (Rais na Mawaziri) ambao licha ya kuwa viongozi wa kitaifa ; pia wanakuwa wamebeba ajenda zao za kisiasa,ajenda za vyama vyao na dhamira zao binafsi (ambazo zaweza kuwa za afya kwa taifa au hatari kwa Taifa). Kwa hiyo basi; Chombo hiki kinapokuwa kimemaliza majukumu tajwa hapo juu kwa kuishia na "kushauri"Kinakuwa kimemaliza majukumu yake kisheria (Bila kujali kama ushauri wake utafuatwa au laa) na hakipaswi kulaumiwa kwa kuwa sheria hairuhusu kufanya zaidi ya hapo.
Katika mazingira kama haya (ya kuipa TISS) Mamlaka kidogo namna hii, kimsingi kuna mambo mengi yanaweza kuhatarisha usalama wa nchi na huku kukiwa hakuna maelekezo ya kutosha ya kisheria kwamba nani afanye nini.Kwa mfano; Milipuko ya mabomu kwenye mkutano wa CHADEMA Arusha; Upo uwezekano kwamba TISS Walijua, pengine wakashauri, na ushauri wao ukapuuzwa.(kama ambavyo naamini walikuwa wanajua kuhusu suala la kusafirishwa kwa Twiga hai lakini bado Twiga walisafirishwa). Kimsingi kama suala la Arusha lilikuwa ni tukio la kisiasa kama baadhi ya watu wanavyo sema,na ikiwa watekelezaji ni CCM; TISS, Kushauri ingekuwa ni sawa na kumshawishi boss wao asitekeleze kile anachodhani anatakiwa kutekeleza. Kwa hakika katika mazingira haya, inawezekana kabisa kwamba chombo hiki kinatekeleza majukumu yake lakini pamoja na hivyo matukio ya kuhatarisha usalama yanatokea kutokana na udhaifu wa kisheria.
Kwa kuendelea na sheria hii (1996) bado vyama vya siasa,Viongozi wa kisiasa, na baadhi ya watu wanaweza kuwa na nguvu kuliko TISS; Yaani TISS, inaweza kukusanya taarifa,kuzichambua na kuwashauri ila wakakataa ushauri na kutenda kinyume na kuvuruga usalama wa nchi.Katika mazingira haya upo uwezekano siku moja nchi ikaelekea tusiko kutegemea kwa kuwa si lazma kila mwanasiasa awe na nia ya dhati ya kuipeleka nchi mbele kwa kuwa viongozi wa kisiasa hupatikana kwa bahati nasibu kutoka katika jamii (jamii yenye watu wema na wabaya).
Katika mazingira haya mfanyabiashara mmoja wa madawa ya kulevywa anaweza kugombea ubunge, baada ya kupata ubunge akapewa uwaziri mkuu (by chance), baada ya kupewa uwaziri mkuu akawa anatumia nafasi yake serikalini na kinga za kiungozi kufanya mambo yenye manufaa kwake lakini hatari kwa taifa,TISS wakamshauri lakini akakataa.
Kimsingi taasisi hii ya Usalama wa Taifa sasa inatakiwa kupewa mamlaka zaidi na kuruhusiwa kuzuia matukio yoyote yanayoonekana kuwa ni tishio kwa usalama wanchi bila kujali mfanyaji ni nani(Wawe na nguvu ya juu kabisa katika masuala yanayoweza kuhatarisha usalama).Inatakiwa tuwe na dira,misingi na maadili ya taifa ambayo ni lazma yafatwe na kila mtu (kuanzia Rais na wengine wote) na mamlaka ya kuhakikisha kwamba misingi hiyo inafuatwa wapewe TISS. Hii itawasaidia kuwa na mmlaka kamili ya kutekeleza majukumu yao kama lilivyo jina la Taasisi yenyewe. Baada ya kukipa mamlaka hayo chombo hiki, mambo kama vile kuficha fedha nje, umafia kwenye siasa na mambo mengine kama mitandao ya madawa ya kulevya yanaweza kudhoofishwa sana hata kama yanafanywa na vigogo wazito.
Swali la kizushi:
Kama msajili wa vyama vya siasa anasema ikibainika kuwa waliolipua bomu Arusha ni CHADEMA atakifuta CHAMA, Lakini kama ikibainika ni CCM; Kwa kuwa ni chama tawala atakishauri. Je! ushauri wa Tendwa unaweza kuwa na nguvu kuliko wa TISS, na hivyo kuwa ni lazma ukubalike? Ikiwa sio, Je ikibainika ni CCM, halafu akawa shauri na wakakataa, TISS wakawashauri wakakataa, ni nani wakuwadhibiti? Je! Hali itakayofuata baada ya hapo itakuwa ya afya kwa nchi yetu kweli?