ICC naanza kuwaona ni wazembe

ICC naanza kuwaona ni wazembe

Salary Slip

Platinum Member
Joined
Apr 3, 2012
Posts
52,144
Reaction score
162,541
Nilikuwa na imani sana na hii mahakama, ila kwa sasa naanza kupoteza matumaini kuwa huenda nayo inaingilliwa .

Tangu watuhumiwa wa mauji ya Oktoba 29 wafunguliwe kesi, inakuwaje mahakama hii iko kimya mpaka leo huku ikionekana kukutana na watu ambao ni wateule wa mtuhumiwa mkuu?

Kukutana sio kosa, ila huu ukimya unaanza kutupa mashaka.

Au wanasubiri uchunguzi wa tume ya Samia?

Kama wanasubiri huo uchunguzi, hawa watu kweli wako serious?

Anyway, mnaojjua hii mahakama inavyofanya kazi hebu tusaidiane labda kuna mambo sisi wengine hatuyajui kuhusu utendaji kazi wa hii mahakama.
 
Nilikuwa na imani sana na hii mahakama, ila kwa sasa naanza kupoteza matumaini kuwa huenda nayo inaingilliwa .

Tangu watuhumiwa wa mauji ya Oktoba 29 wafunguliwe kesi, inakuwaje mahakama hii iko kimya mpaka leo huku ikionekana kukutana na watu ambao ni wateule wa mtuhumiwa mkiuu?

Au wanasubiri uchunguzi wa tume ya Samia?

Kama wanasubiri huo uchunguzi, hawa watu kweli wako serious?

Anyway, mnaojjua hii mahakama inavyofanya kazi hebu tusaidiane labda kuna mambo sisi wengine hatuyajui kuhusu utendaji kazi wa hii mahakama.
Mkuu,

Umesoma kitabu gani, chapisho gani kubusu ICC inavyofanya kazi?

Naona kama Watanzania wengi wanakwenda kwa assumptions sana bila kutazama facts.
 
Icc hawajawah kuweka hadharani mfumo wao wa ufanyaji kazi,kuna muda kesi inakua silent mpaka miaka 3 then wanaibuka na kumwajibisha mshtakiwa...
Vuta subra tutajua ukweli muda ukifika
 
Icc hawajawah kuweka hadharani mfumo wao wa ufanyaji kazi,kuna muda kesi inakua silent mpaka miaka 3 then wanaibuka na kumwajibisha mshtakiwa...
Vuta subra tutajua ukweli muda ukifika
Una mfano wa kesi iliochukua miaka 3 kuanza kusikilizwa?
 
Kesi za ICC huchukua muda mrefu sana kuanza, pia ICC sasa hivi inapumulia mashine kutokana na kuandamwa na kuwekewa vikwazo na utawala wa Trump baada ya kutoa waranti ya kukamatwa Netanyahu.
 
Tunelekea mwezi wa 5 huu sasa wako kimya, Je, huoni kuna shida hapa?
Hujajibu swali langu.

Shida kwa muktadha gani?

Unaelewa ICC inavyofanya kazi? Unaelewa mandate yake? Unaelewa guidelines zake? Unaelewa role ya geopolitics? Unaelewa process zake zikoje? Unaelewa muda zinazochukua?

Au una assume tu kuwa itakuwa hivi na vile kutokana na unavyofikiri wewe tu? Kwamba kesi ya ICC ni sawa na kwenda kituo cha Polisi kuchukua RB kufungua kesi Kisutu?

Nimekuuliza umesoma nini kuhusu ICC inavyofanya kazi?

Hujanijibu.
 
Nilikuwa na imani sana na hii mahakama, ila kwa sasa naanza kupoteza matumaini kuwa huenda nayo inaingilliwa .

Tangu watuhumiwa wa mauji ya Oktoba 29 wafunguliwe kesi, inakuwaje mahakama hii iko kimya mpaka leo huku ikionekana kukutana na watu ambao ni wateule wa mtuhumiwa mkuu?

Kukutana sio kosa, ila huu ukimya unaanza kutupa mashaka.

Au wanasubiri uchunguzi wa tume ya Samia?

Kama wanasubiri huo uchunguzi, hawa watu kweli wako serious?

Anyway, mnaojjua hii mahakama inavyofanya kazi hebu tusaidiane labda kuna mambo sisi wengine hatuyajui kuhusu utendaji kazi wa hii mahakama.
Endeleeni kuimba 'Mungu Wabariki Wazungu '
 
Mkuu, ICC huchukua miaka kadhaa kuanza kesi. Mfano ni kesi ya machafuko ya baada ya uchaguzi wa 2008 nchini Kenya, Ilichukua zaidi ya miaka 5 hadi kuanza kusikilizwa.
 
Una mfano wa kesi iliochukua miaka 3 kuanza kusikilizwa?
Rodrigo Duterte , dikteta na muuaji wa Philippines, kakamtwa mwaka 2025 mwezi March kwa makosa aliyofanya kati ya 2011 na 2019 .


Uhuru Kenyatta na William Ruto walipanda kizimbani 2011 kwa makosa yaliyotokea baada ya vurugu za uchaguzi 2007-2008


Hivyo , muda bado upo na siku itafika nyang'au la Kizimkazi lipata haki yake.
 
Back
Top Bottom