Andre-Pierre
JF-Expert Member
- Nov 4, 2019
- 336
- 1,236
“Naibu Waziri Mkuu”
Ali Hassan Mwinyi akiwa Rais wa JMT, alilazimika kuteua Waziri Mkuu kutoka bara baada ya kuchukua madaraka kutoka kwa Mwl. J.K Nyerere.
Katiba ilielekeza ikiwa Rais atatoka Zanzibar Waziri Mkuu atatoka Tanganyika na ndiye atakayekuwa Makamu wa Kwanza wa Rais wa Muungano.
Joseph Sinde Warioba, ambaye alikuwa Mwanasheria Mkuu wakati wa Mwl. J.K Nyerere, aliteuliwa kuwa waziri mkuu na makamu wa kwanza wa Rais.
Dkt. Salim Ahmed Salim aliteuliwa kuwa Naibu Waziri Mkuu, 5.11.1985 hadi 19.09.1989 wakati huo akiwa Waziri wa Ulinzi.
Waziri Mkuu akiwa Jaji Joseph Sinde Warioba na Makamu wa kwanza wa Rais. Warioba amekuwa Waziri Mkuu 5.11.1985 hadi 9.11.1990
Dk. Salim Ahmed Salim aliondoka baada ya kuchaguliwa kuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Nchi Huru za Kiafrika (O.A.U) alipohudumu 1989-2001
Mzee Ali Hassan Mwinyi aliulizwa swali hilo, kwa nini umeanzisha cheo ambacho hakipo katika Katiba ya JMT?
Mzee Ali Hassan Mwinyi akajibu, Katiba ya JMT haijasema (Naibu Waziri Mkuu) awepo, na haijakataza asiwepo.
Ali Hassan Mwinyi alikuwa na Mawaziri Wakuu na Makamu wa kwanza wa Rais: Joseph Warioba, John Malecela, na Cleopa Msuya.
katika kipindi hicho Marais wa Zanzibar na makamu wa pili wa Rais walikuwa ni; Sheikh Idiris Abdul Wakil, na Dkt. Salmin Amour.
Leo 30.08.2023 Rais Samia Suluhu Hassan kamteua Dotto Biteko kuwa Naibu waziri mkuu. Mjadala unaibuka.
Ukimuuliza Rais Samia Suluhu Hassan hili swali, atakuelekeza uelekee ukatazame Ibara ya 36 ya katiba ya JMT.
Bado mjadala utakuwa ule wa mwaka 1985. Katiba ya JMT haijasema (naibu waziri mkuu) awepo, na haijakataza asiwepo.
Utata unakuja kwa sababu hatuna “Enumerated powers doctrine” kwenye mfumo wa Katiba yetu.
Kama baadhi ya nchi, kama kitu katika Katiba hakijaelezwa kwamba kiwepo maana yake kimekatazwa!
Kuna kanuni ya kisheria inaitwa (legal maxim). “Kila kitu ambacho hakijakatazwa kinaruhusiwa” ni kanuni ya kikatiba
Ni dhana, hatua yoyote inaweza kuchukuliwa na mtu binafsi au chombo isipokuwa kama kuna sheria dhidi yake
Tunarudi mezani, ndiyo maana tunasema tunaitaka katiba mpya kwa haraka. Rais amepewa madaraka makubwa sana
Katika nchi yenye utawala wa kidemokrasia, Rais amepewa madaraka kama tawala za kijeshi, kiimla, kifalme na kisultan
Ibara ya 36 inapaswa kumfunga Rais na kumpoka mamlaka ya kuanzisha na kufuta nafasi za madaraka katika utumishi.
Ingawa wakosoaji wanatumia Ibara ya 36(2) kwamba Rais anatakiwa kuteua watu hao kushika nafasi zilizotajwa katika katiba.
Rejea ‘hansard’ za Bunge, 24.06.2011, Augustine Mrema, alikuwa analalamika bungeni hajapewa mafao ya Naibu Waziri Mkuu.
“Mheshimiwa Mwenyekiti... ukiacha kazi utapewa asilimia 80 ya mafao yako ya mshahara wako, nipeni basi hata asilimia 20 tu.”
“Mnasema hiki cheo changu hakikuwa kwenye Katiba, Rais ndiye anaanzisha cheo. Hata Mawaziri wetu wanaanzishwa kwa decree ya Rais.”
Naibu Waziri Mkuu ni cheo hakipo kikatiba. Alipodai mafao ya cheo hicho aliambiwa aoneshe kifungu cha sheria kinachompa uhalali wa kulipwa ameondoka bila kulipwa.
Augustine Mrema aliteuliwa kuwa waziri wa mambo ya ndani katikati ya kipindi cha uwaziri mkuu wa John Samuel Malecela.
Mrema akiwa waziri wa mambo ya ndani alikuwa anafanya maamuzi mengi kinyume na sheria. Malalamiko yakaendelea kuwepo.
Hiyo ilisababisha Mrema apewe naibu waziri Jaji Edward Anthony Mweisumo kutoka Mororogoro ili kuzuia serikali kuingia katika migogoro ya kisheria.
Kulitokea malalamiko mawaziri wenzake Mrema anaingilia majukumu yao. Kuzima malalamiko Rais Mwinyi akamteua kuwa Naibu Waziri Mkuu.
Kulikuwa na malumbano makali sana kati ya Mary Chipsi Chipungahelo na Augustine Lyatonga Mrema. Ndiyo mwanzo wa Mrema kuteuliwa kuwa Naibu Waziri Mkuu.
Kwa sababu tulikuwa na Rais aliyekuwa anaendesha mambo kiswahili ndio maana aliweka vyeo kama hivyo, mambo ya Kiswahili.
Ni matumizi mabaya ya fedha za umma. Unakuwa na Waziri Mkuu ambaye ofisi yake ina wizara kadhaa halafu unaunda cheo cha “Naibu Waziri Mkuu”.
MMM, Martin Maranja Masese
Ali Hassan Mwinyi akiwa Rais wa JMT, alilazimika kuteua Waziri Mkuu kutoka bara baada ya kuchukua madaraka kutoka kwa Mwl. J.K Nyerere.
Katiba ilielekeza ikiwa Rais atatoka Zanzibar Waziri Mkuu atatoka Tanganyika na ndiye atakayekuwa Makamu wa Kwanza wa Rais wa Muungano.
Joseph Sinde Warioba, ambaye alikuwa Mwanasheria Mkuu wakati wa Mwl. J.K Nyerere, aliteuliwa kuwa waziri mkuu na makamu wa kwanza wa Rais.
Dkt. Salim Ahmed Salim aliteuliwa kuwa Naibu Waziri Mkuu, 5.11.1985 hadi 19.09.1989 wakati huo akiwa Waziri wa Ulinzi.
Waziri Mkuu akiwa Jaji Joseph Sinde Warioba na Makamu wa kwanza wa Rais. Warioba amekuwa Waziri Mkuu 5.11.1985 hadi 9.11.1990
Dk. Salim Ahmed Salim aliondoka baada ya kuchaguliwa kuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Nchi Huru za Kiafrika (O.A.U) alipohudumu 1989-2001
Mzee Ali Hassan Mwinyi aliulizwa swali hilo, kwa nini umeanzisha cheo ambacho hakipo katika Katiba ya JMT?
Mzee Ali Hassan Mwinyi akajibu, Katiba ya JMT haijasema (Naibu Waziri Mkuu) awepo, na haijakataza asiwepo.
Ali Hassan Mwinyi alikuwa na Mawaziri Wakuu na Makamu wa kwanza wa Rais: Joseph Warioba, John Malecela, na Cleopa Msuya.
katika kipindi hicho Marais wa Zanzibar na makamu wa pili wa Rais walikuwa ni; Sheikh Idiris Abdul Wakil, na Dkt. Salmin Amour.
Leo 30.08.2023 Rais Samia Suluhu Hassan kamteua Dotto Biteko kuwa Naibu waziri mkuu. Mjadala unaibuka.
Ukimuuliza Rais Samia Suluhu Hassan hili swali, atakuelekeza uelekee ukatazame Ibara ya 36 ya katiba ya JMT.
Bado mjadala utakuwa ule wa mwaka 1985. Katiba ya JMT haijasema (naibu waziri mkuu) awepo, na haijakataza asiwepo.
Utata unakuja kwa sababu hatuna “Enumerated powers doctrine” kwenye mfumo wa Katiba yetu.
Kama baadhi ya nchi, kama kitu katika Katiba hakijaelezwa kwamba kiwepo maana yake kimekatazwa!
Kuna kanuni ya kisheria inaitwa (legal maxim). “Kila kitu ambacho hakijakatazwa kinaruhusiwa” ni kanuni ya kikatiba
Ni dhana, hatua yoyote inaweza kuchukuliwa na mtu binafsi au chombo isipokuwa kama kuna sheria dhidi yake
Tunarudi mezani, ndiyo maana tunasema tunaitaka katiba mpya kwa haraka. Rais amepewa madaraka makubwa sana
Katika nchi yenye utawala wa kidemokrasia, Rais amepewa madaraka kama tawala za kijeshi, kiimla, kifalme na kisultan
Ibara ya 36 inapaswa kumfunga Rais na kumpoka mamlaka ya kuanzisha na kufuta nafasi za madaraka katika utumishi.
Ingawa wakosoaji wanatumia Ibara ya 36(2) kwamba Rais anatakiwa kuteua watu hao kushika nafasi zilizotajwa katika katiba.
Rejea ‘hansard’ za Bunge, 24.06.2011, Augustine Mrema, alikuwa analalamika bungeni hajapewa mafao ya Naibu Waziri Mkuu.
“Mheshimiwa Mwenyekiti... ukiacha kazi utapewa asilimia 80 ya mafao yako ya mshahara wako, nipeni basi hata asilimia 20 tu.”
“Mnasema hiki cheo changu hakikuwa kwenye Katiba, Rais ndiye anaanzisha cheo. Hata Mawaziri wetu wanaanzishwa kwa decree ya Rais.”
Naibu Waziri Mkuu ni cheo hakipo kikatiba. Alipodai mafao ya cheo hicho aliambiwa aoneshe kifungu cha sheria kinachompa uhalali wa kulipwa ameondoka bila kulipwa.
Augustine Mrema aliteuliwa kuwa waziri wa mambo ya ndani katikati ya kipindi cha uwaziri mkuu wa John Samuel Malecela.
Mrema akiwa waziri wa mambo ya ndani alikuwa anafanya maamuzi mengi kinyume na sheria. Malalamiko yakaendelea kuwepo.
Hiyo ilisababisha Mrema apewe naibu waziri Jaji Edward Anthony Mweisumo kutoka Mororogoro ili kuzuia serikali kuingia katika migogoro ya kisheria.
Kulitokea malalamiko mawaziri wenzake Mrema anaingilia majukumu yao. Kuzima malalamiko Rais Mwinyi akamteua kuwa Naibu Waziri Mkuu.
Kulikuwa na malumbano makali sana kati ya Mary Chipsi Chipungahelo na Augustine Lyatonga Mrema. Ndiyo mwanzo wa Mrema kuteuliwa kuwa Naibu Waziri Mkuu.
Kwa sababu tulikuwa na Rais aliyekuwa anaendesha mambo kiswahili ndio maana aliweka vyeo kama hivyo, mambo ya Kiswahili.
Ni matumizi mabaya ya fedha za umma. Unakuwa na Waziri Mkuu ambaye ofisi yake ina wizara kadhaa halafu unaunda cheo cha “Naibu Waziri Mkuu”.
MMM, Martin Maranja Masese