Ibada za kutakasa ardhi/makazi

Ibada za kutakasa ardhi/makazi

Mshana Mungu akubariki sana. Umekuwa kiungo kizuri cha kuzijaza nafsi za watu juu ya ufahamu wa miili yao na Roho zao.

Tunajua kabisa mfumo wa utawala wa ulimwengu huu umewekwa kiasi kwamba anayemuwahi mwenzie rohoni ndiye anayekula nyama.

Mwili ni silaha ya tusaidia kutawala mazingira yetu, Lakini utawala halisi ni rohoni.
Kwa wale wanaoiamini biblia ukisoma Mwanzo 1. Soma yote Mungu anamuumba Adamu na Eva na anawabariki na kuwapa amri ya kuijaza nchi na kiitiisha wakati hawana miili ila ni Roho

Sura ya pili Mwanzo wanapewa miili wakati assignment ya kuzaa na kutiisha Imeshatolewa. Inamaana mwili ni silaha tuu ya kutimiza kazi. Ni sawa unapoajiliwa unapewa gari. Maana hiyo gari sio wewe. Na mwili sio wewe ni lugha ngumu kidogo Lakini ndiyo ukweli.

Mshana jr Mungu ukuongeze maarifa na uthubutu wa kuendelea kuufunua huu ulimwengu wa roho ili maarifa ijazwe kwetu na tusiangukie kwenye kundi la kupotea sababu ya kukosa maarifa.

MUNGU AKUBARIKI SANA MTUMISHI
 
Mungu ni nafsi tatu baba mwana na Roho mtakatifu.( ni kitu kimoja lakini vinafanya kaz tofauti) Yesu anaposema mimi na Baba tu mmoja. Baba yake ni nani? Kama mariam alichukua mimba kwa uwezo wa Roho. Roho ni nani na Baba ni nani? Hawa wote ni kitu kimoja sema vinafanya kaz tofauti. Mfano mimi nikiwa nyumban ni mama nikiwa na mume wangu ni mkewe na nikiwa kazini ni mwalimu. Hapo huwez sema ni watu watatu tofauti bali mtu mmoja lakin nina wadhifa tofauti. Roho inaweza kureproduce kasome biblia vizuri mathew 1: 18-25. Hii inaenda kwa imani. Na hatutafsir biblia kimwil cz andiko linaua wakati unasoma omba Mungu( Roho mtakatifu) akufundishe

Mkuu nielewe vizuri. Mungu ni roho ambaye kwake roho za viumbe vyote zinatoka. (He is God of all souls). Kama unaamini kuwa mti una roho, basi hiyo roho ya huo mti imetoka kwake. Hivyo anauwezo wote, hakuna kinachomshinda. Ndo maana ukisoma Biblia kitabu cha Mwanzo, baada ya uumbaji wa Mwanadamu, Biblia inasema Binadamu wa kwanza walikuwa pure. They were born divine. Baada ya kuanza kuona dunia inapendeza wakavutiwa na mazuri ya dunia kiwango cha divine kikaanza kupungua. Ndivyo ilivyo hata leo. Mtoto yeyote anayezaliwa he/she is born divine ila sasa anapokuwa na kuachakupalilia ile divine power iliyoko ndani yake iendelee kuwa pure kama ilivyowekwa, hapo ndipo ule utakatifu unapungua. Kuhusu fundisho la Yesu aliposema kuwa " Mimi na Baba yangu tu wamoja" ana maana kubwa sana. nitaeleza kwa jinsi mimi ninavyolielewa neno hili.

Kama nilivyosema tokea mwanzo kuwa Yesu alizaliwa kama wewe na mimi. Lakini alipokuwa alikuwa na nia ya kumtafuta Mungu na Yesu alianza kumtafuta Mungu akiwa na miaka 12 (katika kipindi hiki Yesu hakuokeneka machoni Mwa watu) alikuwa milimani akifunga na kuomba ili Mungu ajidhihilishe kwake. Alikuja kuonekana tena akiwa na miaka 30. (hiyo miaka 18 ndiyo aliyokuwa nyikani akimtafuta Mungu). Alivyotoka huko ndo kaanza kuwafundisha watu wamjue Mungu na kwakuwa alikutana na Mungu roho yake ilirudia utakatifu iliokuwa nao tokea mwanzo. Ndo maana aliweza kufanya kitu chochote ndo maana kila kitu kilimtii. kwa sababu utatatifu wa roho yake ulikuwa sawa na wa roho kuu. (The Supreme Soul) yaani Mungu Mwenyewe. Na maneno yake kuwa "aliye niona mimi amemuona baba" ndo yanapodhihirishwa. Kwa sababu utafatifu na utukufu wa Mungu ulikuwa tayari ndani na juu yake. Usingeweza kuwatenganisha. Hata leo ukimtafuta Mungu kwa dhati utampata nawe utakuwa kama Yesu. Lakini siyo kwa namna watu wanavyomtafuta Mungu kwa sasa hapo hapo wanafikiria kutafuta pesa, wanafikiria familia, wanafikiri wapenzi wao na wazazi wao. Hivyo vyote ni vifungo ambavyo vitaturudisha nyuma.

Hata Yesu mwenyewe amesemema ukitaka kunifuata renounce kila ulichonacho. Vunja hizo bondage ulizofungwa kwazo utamuona Mungu.
Acha maigizo yanayoendelea sasa hivi makanisani eti mchungaji anasema anafanya miujiza na wengine kujitangaza kuwa mitume na Manabii.
 
Mshana Mungu akubariki sana. Umekuwa kiungo kizuri cha kuzijaza nafsi za watu juu ya ufahamu wa miili yao na Roho zao.

Tunajua kabisa mfumo wa utawala wa ulimwengu huu umewekwa kiasi kwamba anayemuwahi mwenzie rohoni ndiye anayekula nyama.

Mwili ni silaha ya tusaidia kutawala mazingira yetu, Lakini utawala halisi ni rohoni.
Kwa wale wanaoiamini biblia ukisoma Mwanzo 1. Soma yote Mungu anamuumba Adamu na Eva na anawabariki na kuwapa amri ya kuijaza nchi na kiitiisha wakati hawana miili ila ni Roho

Sura ya pili Mwanzo wanapewa miili wakati assignment ya kuzaa na kutiisha Imeshatolewa. Inamaana mwili ni silaha tuu ya kutimiza kazi. Ni sawa unapoajiliwa unapewa gari. Maana hiyo gari sio wewe. Na mwili sio wewe ni lugha ngumu kidogo Lakini ndiyo ukweli.

Mshana jr Mungu ukuongeze maarifa na uthubutu wa kuendelea kuufunua huu ulimwengu wa roho ili maarifa ijazwe kwetu na tusiangukie kwenye kundi la kupotea sababu ya kukosa maarifa.

MUNGU AKUBARIKI SANA MTUMISHI
Nakushukuru mno obseva kwa kunitia nguvu
 
Very nice topic mshana...mfano mashamba tunayokodi kwa kilimo mengi yamefungwa kutokana na matambiko au mila za huko nyuma,ukifanya kitubio kwa niaba yao na kufungua vifungo utashangazwa na mazao yatokayo hapo...kuna vitu ukivijua raha sana
 
Kuna somo moja aliwahi kufundisha Mwl Christopher Mwakasege linafanana na mada hii.ni kweli unaweza ingia ktk mji fulani ukitazama hali ya uchumi wa watu na watu wenyewe ukatumia akili vzr utagundua MUNGU wa kwanza kukalibishwa ktk eneo hilo ni MUNGU yupi,kuna maeneo yamechimbiwa wanyama na kumwaga damu mpaka ardhi inashangaa,na vitu vinakua vinajionyesha kwa watu,hali ya afya zao na vipato vyao,ardhi inalimwa lakini haiwapatii mavuno ya kutosha,na watu wenye kupiga makafala ndo unawakuta wenye uwezo ktk maeneo hayo,late say ni kijiji fulani,unakuta watu watatu au wawili ndo wenye magari ya kusafilisha abiria to town per day,ndo wenye mashine za kusaga nafaka na nyumba nzuri,wengine wote wamechoka,inakua inaonyesha ni MUNGU yupi ametamalaki hapo,MUNGU wa kishetani au MUNGU aloziumba mbingu na nchi,sasa hapo ili kuwatoa watu ktk hali hiyo panatakiwa toba ya hali ya juu mbele za MUNGU ili aiponye ardhi hiyo na kuweka usawa wa kimaisha na watu wote wawe na amani.mada hii nimeipenda,bless you Mshana jr
 
Very nice topic mshana...mfano mashamba tunayokodi kwa kilimo mengi yamefungwa kutokana na matambiko au mila za huko nyuma,ukifanya kitubio kwa niaba yao na kufungua vifungo utashangazwa na mazao yatokayo hapo...kuna vitu ukivijua raha sana
Kuna ulimwengu unaoendesha hii dunia kwa namna ya pekee kabisa. . . . unajikuta tu baraka zinamiminika
 
Kwema kaka majukumu yamenikaba koo lakini tupo pamoja kila nipatapo wasaa lazma nichungulie jukwaani mshana katupia ujuzi gani.
Kazi na dawa vizuri sana lazima kubalance mambo usipotee sana lakini
 
Yesu amezaliwa kwa uwezo wa Roho Mtakatifu. Na Roho mtakatifu ni Mungu. Mariam aliku bikira na ndio maana joseph aliposikia mariam ana mimba alitaka kumuacha kwa siri sababu mimba haikua yake lakin aliambiwa usimuache mkeo sababu amebeba mimba kwa uwezo wa Roho. Rudi kusoma ktk mathayo. 1: 28-25 halafu urekebishe hapo juu. Kitu kingine mtoto akiwa tumbon damu inakua ni ya baba na si ya mama. Kwahiyo damu ya mariam haikuingia kwa Yesu. Kwahiyo Yesu anadamu ya Mungu Roho mtakatifu. Damu yake tunasema haina hila wala mawaa. Ndio maana tunaitumia hata ktk kujitakasa sisi na kuitakasa ardhi. Bwana Yesu asifiwee. Wote tuseme Amen
Amina Amina Ubarikiwe kwa jina la Bwana wetu Yesu Kristo mfufuka alie hai kwa ufafanuzi huo
 
Amen Amen
1454256802019.jpg
 
Back
Top Bottom