I seems to be boring

Mrs Mtaba

Senior Member
Joined
Jan 21, 2009
Posts
104
Reaction score
6
Hello my dears Wana JF,
Napenda kuelimika katika hili swala, na hisi kuwa huwa na bore hubby kutokana sijui ni mazoea au sijui cha kuongea naye! Nifanye nini ili nisiwe na mbore, maana mimi nadhani nimkimya sana inaweza kupita masaa manne hatujaongea kitu, na sipendi kuongea pumba nikaonekana wa kuja. Msaada tafadhalini wandugu
 
mmmh?

Mausioano yenu ya aina gani? Unaogopa kuongea pumba?
Huyo anatakiwa kuwa mshkaji wako, unachoogopa nini?
Hebu changamka....
 
Pole ndugu yangu.Umeolewa na bado unamwogopa Mr wako?
Jiachie, hata kama ni pumba basi atakurekebisha na polepole utakuwa sawa tu.Ukijifanya bubu, anaweza akakutana na mafundi wa kuongea akakuona wewe si mali kitu!
 
E bana e, mbona wamama wengi inaonekana mmekaa na mawazo ya ki-utumwa-utumwa dizaini.?

Mi nakushauri be yourself and enjoy the self in you. Huna haja kumuogopa mtu, au ku-try harder kumfurahisha mtu. Kama mlioana kwa kupendana, alipaswa kujua ulivyo na unachopenda, sio swala la wewe tu kuhangaikia kukidhi viwango vyake daima.
 
Pole ndugu yangu.Umeolewa na bado unamwogopa Mr wako?
Jiachie, hata kama ni pumba basi atakurekebisha na polepole utakuwa sawa tu.Ukijifanya bubu, anaweza akakutana na mafundi wa kuongea akakuona wewe si mali kitu!
Nashukuru dada (samahani kama wewe ni kaka), ni kweli najikuta nakaa kimya kutoka na respond zake (sometimes hukaa kimya hanijibu au anaweza kunipa short answer ya kunikatisha tamaa kabisa). So kuepusha maumivu hujikuta nakaa kimya. Pengine niulize je kuna mahali (may be website) mtu huweza kupata tips how to talk to your man, how to respond to him etc.
 

Bila samahani ndugu yangu... mimi ni mdada.
Kabla ya kukupa mbinu za kuvunja ukimya wako naomba nikuulize:Kwani toka mnachumbiana hadi mnaoana mlikuwaje?Ulikuwa mkimya hivyohivyo?
 
Bila samahani ndugu yangu... mimi ni mdada.
Kabla ya kukupa mbinu za kuvunja ukimya wako naomba nikuulize:Kwani toka mnachumbiana hadi mnaoana mlikuwaje?Ulikuwa mkimya hivyohivyo?
samahani ntakujibu swali lako kwenye PM please.
 
karibu sana.

mh...

Mrs Mtaba, uyo bwana ni mzungu au mwafrika mwenzetu? huenda labda ndo tabia yake ilivo, na tabia haina dawa?

Au mtafutie kakinywaji atachangamka, kisha muulize kisa na maana, au mvizie kwenye mambo yetu yaleeeee...umueleze wasiwasi/hofu yako kwake

Asante
 
Nilishajaribu yote hayo, tena akiwa amelewa ndo balaa zaidi you can get disappointed to the maximum ya kuchuna ngozi! Ni mtu wa tz kabisa.
 
Mrs. Mtaba

Unamiss vitu vingi kweli, jiachie mama huyo ni mumeo ndo anayejua weakness na strength zako hivyo usijaribu kuwa na mawazo ya pumba au nafaka.
Anakupenda atakuambia tu kuwa hiki sawa hiki siyo.. Mumeo anapenda vitu gani uwe unamfanyia au kuviongelea pengine hata stori za hapa na pale kuondoka kimya cha mshindo.
 
Hasemi nini anachopenda nimfanyie, nikimuuliza anazuga nakukaa kimya!
 
Hasemi nini anachopenda nimfanyie, nikimuuliza anazuga nakukaa kimya!

Du!..umenishangaza kweli? mlifikiaje mpaka hapo mkaoana? Au sijakuelewa vizuri, ni boifrendi au mume mpaka umenichanganya?
So mawasiliano yenu ni duni kwenye hiyo ndoa? Na unafahamu mawasiliano mazuri ni kitu muhimu kama siyo kizuri kwenye ndoa/mahusiano!..

Mfanyie suprises tofauti tofauti uone anafurahi vipi kati ya hivyo!..Huyo mumeo anahitaji mtu mchangamfu na mwenye uthubutu wa hali ya juu asione ndoa ni mazoea..
 

Asante dadangu...ntajaribu pengine unipe hizo suprises nijaribu!
 

Hicho kimya kina maana. Kma sio chuji ni kwamba anamawazo na wewe unamyeyusha... we pita na upande wa khanga wakati bado mbichi umetoka kuoga. ataongea tu hata kama ana mawazo. vidume hapo umetufikisha...
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…