unajua namna ambavyo Kova anataka jamii iamini ni kua Muro ni sehemu ya kundi la wahalifu ambae anatumia Pingu katika matendo yakutishia watu, na ndio maana siku ya pili akaibuka na wadau fulani hivi akiwahusisha na matukio kadhaa ya kitapeli hapa mjini, na akahitimisha kwa kusema kua wale jamaa ukiwapa dhamana wanaweza kuitapeli hata dhamana yenyewe.....nguvumali (old or new?), kwani kazi ya pingu ni nini hadi mtu aulizie mahakamani? Kweli tunahitaji mahakama kuuliza kazi ya pingu ni nini?
bingo!!!!!!!!!!! I like you Kimweri.. ndio maana nimesema kwenye ule ukurasa mwingine hakuna jaji wala mahakama inayoweza kumfunga Muro kwa "kosa" la kukutwa na pingu ambazo zilikuwa ndani ya gari (wapi???)! Vinginevyo, itafungua mlango wa watu kufungwa wakikutwa na kamba, mnyororo n.k!
hili swala naamini likifikishwa mahakamani kuna mengi yaliofichika yatakua wazi, upo upande utaumbuka na utatafuta pakufichia sura zao. nasema haya kwa maana kuna mtafaruku katika kila hatua, hali ambayo inamuacha mtanzania wakawaida asiwe na maoni binafsi yaliyo huru....bado natamani kumuona Jerry Muro akiulizwa swali la matumizi ya pingu yake mahakamani .... maana Kova ameshindwa kumuhoji hilo swali kama Jerry mwenyewe alivyonukuliwa.
sasa baaada ya sakata hili na UMMA kueleweshwa juu ya matumizi ya PINGU bila shaka duka linalouza pingu lijiandae kupokea maombi mengi ya kuhitaji bidhaa hiyo.
Taanzania Tanzaniaaa nilukupenda nchi yangu!!!
Mkjj, unasahau kwamba serikali yetu inapinga shughuli za ukahaba??... hatuchelewi kukuta kwamba sababu kubwa zinazowapelekea 'watawala' wetu kupinga manunuzi ya pingu hizo ni matumizi yake yasiyotarajiwa kwenye mambo ya ukahaba. Wamegundua hivi karibuni ununuzi wa pingu umeshamiri na uchunguzi wao umewajuza kuwa pingu hizi zinatumika kwenye S & M (ngono machachari), jambo ambalo ni kinyume na sheria zetu.
HUYU KOVA KASEMA PINGU NI ILLEGAL,swali la msingi MTU AKIKUTWA NA GONGO(which is deemed illegal) huwa anaulizwa risiti ya kununulia gongo hiyo?au huwa anakamatwa kwa kumiliki,kunywa gongo?
Hili ni suala dogo sana kushughulikiwa kisheria kwani utaratibu uko wazi ila kutokana na upeo mdogo na ushabiki hasa wa taasisi kama jeshi la polisi yote haya yanatokea na kuudhiii...
Ninaamini chanzo cha umasikini wetu ni ukosefu wa watu makini katika nafasi za uongozi hasa upeo wa kuchambua na kuona mbele wala sio mbali..
Tutaliia rasilimali tulizonazo lakini ukosefu wa rasilimali watu katika kutumikia umma ni KIKWAZOOO KIKUBWAA..Hatuhitaji madini, mafuta wala ardhi yenye rutuba, TWAHITAJI RASILIMALI WATU.
Hivi hawa viongozi wetu wanashindwa nini kabla ya kuongea kuhakikisha kuwa wemepima wanachoongea? Ngumu kweli kwa sasa kujua kuwa mtu amekosea kwa makusudi au hajui aongeacho
Nilalapo usingizi wa mangamungamu napata majinamizi juu yako weee!
Niamkaponi ni uchungu kwangu mama wa kambo weeee!
.Sisemi kwa maana ya kuwatukana lakini kutokana na uzoefu wangu katika mambo ya afya ya akili (mental health) naweza kusema pasipo shaka kabisa kuwa kuna watu wanahitaji kupimwa na kupatiwa matibabu ya haraka kwani wana matatizo katika uwezo wao wa kutumia chembechembe za ubongo kufikiri na kujenga hoja.
Nother greater thinker!! - - - mental health again man, should we wonder who "rules" this country?HUYU KOVA KASEMA PINGU NI ILLEGAL,swali la msingi MTU AKIKUTWA NA GONGO(which is deemed illegal) huwa anaulizwa risiti ya kununulia gongo hiyo?au huwa anakamatwa kwa kumiliki,kunywa gongo?
macho nimefunguka Waberoya, naninaamini sakata la muro litaibua mengi mazuri aidha kisheria ama kijamii, maaana nimeanza kujua matumizi mwanana wa pingu katika mahaba, hii imenipa hamasa ya mimi kuitafuta ili nikidhi haja....Hilo duka wamemuuzia pingu Muro tu au? haiwezekani wakaleta stock ya pingu moja jamani ebu fungueni macho !!!!!
!!
kinachonishangaza Nyambala ni kuwa wanakasirishwa sana na kukutwa pingu ndani ya gari kuliko bunduki!! NIlikuwa najiuliza mara ya mwisho kusikia majambazi yamevamia mitaa na pingu au wamepora benki kwa kutumia pingu ilikuwa lini?
unajua namna ambavyo Kova anataka jamii iamini ni kua Muro ni sehemu ya kundi la wahalifu ambae anatumia Pingu katika matendo yakutishia watu, na ndio maana siku ya pili akaibuka na wadau fulani hivi akiwahusisha na matukio kadhaa ya kitapeli hapa mjini, na akahitimisha kwa kusema kua wale jamaa ukiwapa dhamana wanaweza kuitapeli hata dhamana yenyewe.....
ninachotaka kusema ni kua kama atathubutu kumpeleka Muro mahakamani anaweza akafile swala la kukutwa na Pingu kama dhana yakutishia raia ili apate kitu kidogo , sasa silazima kumuhoji lakini kama moja ya vithibitisho vya Jerry kuhusika na aina hiyo ya Uhalifu hakuna namna ila ni kumuhoji kwanini anamiliki hiyo PINGU, na hapo ndipo hoja yangu imelalia.
This is only the tip of the iceberg I am afraid.
Sheria zetu za ajabu nyingine hazijabadilishwa tangu zikokotolewe na muingereza kutoka India 1948.