Wewe na Nyani Ngabu sijui mnatetea nini?! Kwamba haya mateso na mauaji kwa wapinzani ni haki yao na wasipige kelele kuitaka Tz bora na ya ki democracy ??!! Au mnamtetea huyu bhuana dhidi ya wapinzani wake kwa sababu hastahili kupingwa kwa hoja yoyote ?! WaTz wote wakishakuwa na mawazo kama yenu, hiyo Tz ya kesho itakuwaje kwa wajukuu zenu?!
Tuwe na uongozi unaoweza kuelezwa mapungufu yaliopo!! Yawe ya kutengenezwa au ya asili, tukiwa na miungu watu malengo ya taifa, kuwa na nchi bora na ya mfano Africa hayawezi kutimia .
Na mabaya yaliotokea awamu ya 1,2,3 na 4 hayatakiwi kuendelezwa kwa kigezo cha Mbona na huko nyuma yalitokea!!!! Natamani tungekuwa na nchi huru kwa watu wote watawala na watawaliwa. Siyo hii ya kumkosoa bwana mkubwa ni tiketi ya kuzimu
Zamani tukizinyooshea kidole mataifa yaliokuwa yakinyanyasa raia wao, leo tunaweza kumkosoa nani hapa Africa?! Kwani mitihani iliwashinda kina Gbagbo, Jahme, Nkurunzinza nk ndiyo yaliotushinda Zanzibar na hata huku bara.