Huyu Traffic hajipendi, aache Sifa!!

Huyu Traffic hajipendi, aache Sifa!!

Njia ya Mtwara kuna askari alidondoka toka juu ya mti. Tusubiri na nyoka nao waanze kuwamulika katika hivyo vichaka ndipo wataacha.
 
Kama umelazimishiwa kosa usilipe hiyo fine waambie wakupeleke mahakamani.
muda huwa watu wanaangalia muda wa kuzungushana na askari mara mahakamani ..... sasa haya mamilion sijui wanayafanyia nini? maana wao wanakaba sometimes uchague kosa lolote kati ya watakayokupangia...... ili tu wakutoze fedha
 
hadhari ya kamera kwa wenye SMARTPHONEs
nenda Google play store: pakua SPEED CAMERA, install kisha fanya settings kwa ku-connect na google map.

ukianza safari; hakikisha una bundle na uweke DATA ON; weka simu yako karibu na upeo wa macho yako mf. dashboard au gear lever/gear stick. we ruhusu mguu ucheze na accelerator pedal upendavyo huku jicho likitua 'kimakengeza' kwa smartphone yako.
*ukiweza kufanya settings vizuri waweza kuwa una-oversee uwepo wa kamera njia unayotarajia kupita
*ukiikaribia kamera, smartphone yako itatoa alarm/alert kuashiria upunguze endapo utakuwa una-cruse over 50km/h
*jenga mazoea ya kukimbia <48km/h kabla hujafikia kibao cha 50km maana hawa watani wa madreva wana tabia ya kujificha na kupiga picha hata kabla hujakanyaga eneo la tukio.
*changamoto kubwa ni charge ya simu yako. kama ukiwa na chaja ya kiberiti (madereva mnajua) au power bank itakusaidia
[HASHTAG]#Samahani[/HASHTAG] kwa 'Kiswanglish' aghalabu sipendi itokee ila leo nimejikita kuinakishi rejesta mujarabu kwa madereva wa rika la 15-30
asante
 
mkuu kama umebahatika kupita Kilwa road unaenda mkuranga huko hawa jamaa ndivyo wanavyofanya. Wanajificha kwenye vichaka au wanakaa kilimani wanakupiga tochi halafu wanawasiliana na wale walioko pale mzani mkuranga ukifika hapo unakuta wameshakuandikia na risiti ukibisha wanakwambia turudi mahali uone kwenye kamera Tanzania kuna maajabu.
 
Back
Top Bottom