Huyu ndiye mume wangu

Sky Eclat

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2012
Posts
58,636
Reaction score
220,353
Ni m-Tanzania, hajawahi kunipiga, Hulipia huduma zote ndani kuanzia umeme, maji na gesi. Jumamosi anakwenda sokoni asubuhi, Ana kumbuka mpaka pilipili na ndimu. Anajua kupika hivyo hata nikichelewa sina wasiwasi kuwa atakuwa na njaa.

Nguo zake anafua na kupiga pasi mwenyewe. Ni msafi na anapenda vitu vikae katika mpangilio. Hajali hata kukiwa na wageni anaosha vyombo vyote baada ya kula.

Siku za likizo kwenda kusalimu ndugu na jamaa nauli ni juu yake kwa familia nzima.

Lakini ana upande wa pili pia. Maua yote si mawaridi.
 
Hongera kwa kupata huyo mume ila msaidie kufua nguo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sasa wewe unamdhalilisha Aspirin, bora usingemtaja.

Kwenda sokoni mwenyewe, kupika mwenyewe, kuosha vyombo na kujifulia nguo, sasa wewe kazi yako ni nini?
 
Mme wako ni BASHA.
 
Nasubiri upande wa pili wa Asprini.
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…