Yericko Nyerere
JF-Expert Member
- Dec 22, 2010
- 17,026
- 20,511
Zabuni ya Mradi wa ujenzi wa barabara ya mabasi yaendayo kasi jijini Dar ulipitia kwenye misukosuko ya urasimu wa hali ya juu baada ya wanachama na makada maarufu wa CCM kuteka mchakato mzima,
Mjumbe wa halmashauri kuu ya CCM na Katibu mkuu wa CCM ndugu Abdulahman Kinana ndie aliyeileta nchini Tanzania Kampuni ya Strabag ya Ukandarasi wa Ujenzi iliyoanzishwa na Muastria katika mji wa Villach na kuweka makao yake makuu mjini Vienna Austria ambapo kampuni hii ndiyo ilishinda zabuni hiyo
Kinana aliileta kampuni hii kutoka tawi la kampuni hiyo lililopo Ujerumani,
Kuileta kampuni hiyo nchini ni jambo jema, lakini hoja yangu ni namna Kinana anavyousababishia TRA kukosa mapato kutoka kwenye Kampuni hiyo ya uingizaji mitambo ya ujenzi nchini,
Taarifa za TRA mpaka jana zilikuwa zinaonyesha kuwa kampuni hiyo imeingiza mizigo/mitambo yenye thamani ya kodi ya shilingi za kitanzania 16 milioni tu kupitia kampuni ya Sharaf Shipping Company ambapo Taarifa zinaonyesha kuwa Kinana anamiliki hisa 7,500 kati ya 10,000 za kampuni hiyo inayoitwa Sharaf Shipping Company iliyosajiliwa Dar es Salaam tangu mwaka jana mwezi wa saba.
Kinyume chake taarifa na nyaraka za kiintelijensia kutoka ndani ya kampuni hiyo ya Strabag zinaonyesha kuwa kampuni ya Strabag imeilipa 8.56 bilioni kampuni ya wakala wa meli ya Sharaf Shipping Company kama malipo stahiki ya kodi ya uingizaji mitambo nchini tangu kampuni hiyo ilipoanza uingizaji wa mitambo ya ujenzi nchini 03-07-2012,
Kisha ikailipa tena 7.8 bilioni kama gharama za uwakala wa mitambo hiyo,
Wanabodi hayo ni machache tu lakini nitaweka hapa nyaraka za malipo ya Strabag kwa Sharaf Shipping Company na nyaraka za malipo ya Sharaf Shipping Company kwa TRA kama Mods watanipa kibali cha kuweka hapa,
Maafisa wa TRA wanasema linapofika suala la Sharaf Shipping Company hufanya kazi kwa maagizo ya katibu mkuu wa ccm,
Huyo ndie katibu mkuu wa chama tawala nchini Tanzania
Mjumbe wa halmashauri kuu ya CCM na Katibu mkuu wa CCM ndugu Abdulahman Kinana ndie aliyeileta nchini Tanzania Kampuni ya Strabag ya Ukandarasi wa Ujenzi iliyoanzishwa na Muastria katika mji wa Villach na kuweka makao yake makuu mjini Vienna Austria ambapo kampuni hii ndiyo ilishinda zabuni hiyo
Kinana aliileta kampuni hii kutoka tawi la kampuni hiyo lililopo Ujerumani,
Kuileta kampuni hiyo nchini ni jambo jema, lakini hoja yangu ni namna Kinana anavyousababishia TRA kukosa mapato kutoka kwenye Kampuni hiyo ya uingizaji mitambo ya ujenzi nchini,
Taarifa za TRA mpaka jana zilikuwa zinaonyesha kuwa kampuni hiyo imeingiza mizigo/mitambo yenye thamani ya kodi ya shilingi za kitanzania 16 milioni tu kupitia kampuni ya Sharaf Shipping Company ambapo Taarifa zinaonyesha kuwa Kinana anamiliki hisa 7,500 kati ya 10,000 za kampuni hiyo inayoitwa Sharaf Shipping Company iliyosajiliwa Dar es Salaam tangu mwaka jana mwezi wa saba.
Kinyume chake taarifa na nyaraka za kiintelijensia kutoka ndani ya kampuni hiyo ya Strabag zinaonyesha kuwa kampuni ya Strabag imeilipa 8.56 bilioni kampuni ya wakala wa meli ya Sharaf Shipping Company kama malipo stahiki ya kodi ya uingizaji mitambo nchini tangu kampuni hiyo ilipoanza uingizaji wa mitambo ya ujenzi nchini 03-07-2012,
Kisha ikailipa tena 7.8 bilioni kama gharama za uwakala wa mitambo hiyo,
Wanabodi hayo ni machache tu lakini nitaweka hapa nyaraka za malipo ya Strabag kwa Sharaf Shipping Company na nyaraka za malipo ya Sharaf Shipping Company kwa TRA kama Mods watanipa kibali cha kuweka hapa,
Maafisa wa TRA wanasema linapofika suala la Sharaf Shipping Company hufanya kazi kwa maagizo ya katibu mkuu wa ccm,
Huyo ndie katibu mkuu wa chama tawala nchini Tanzania