nendiwekilasa
Member
- Nov 14, 2012
- 10
- 19
- Thread starter
- #61
Mara nyingi huwa tunakimbilia kutupa lawama kwa wapenzi wetu kupoteza hamu ya kuwa na sisi bila kujichunguza na sisi kwa upande wetu tumefanya nini mpaka hali imefikia huko.
Kutoka nje ya ndoa na kutembea na watu hovyo si suluhu ya kusolve tatizo lako la ndoa, badala yake utaishia kupata magonjwa, kufumaniwa na pengine hata kunasa na hatma yake kuja kufia mbali! Jambo la kujiuliza ni Una ushahidi gani kuwa mwenzio hupata tiba nje ya ndoa? Kwa nini usitafute sababu halisi ya tatizo na kutatua ili mrudi kama zamani kuliko kukimbilia kugawa? Ukiendelea kugawa utagawa mpaka lini? Unajisikiaje kuwa msaliti ndani ya ndoa yako mwenyewe?
Sikia, kaa chini, angalia mwenendo wako na mapungufu yako. Kisha mwite mumeo mkae myasuluhishe. Unaweza kutafuta wamama watu wazima wenye akili zao wakakufundisha namna ya kumrudisha mwanaume aliyefikia hatua hiyo. Unaweza kuwapm na akina Kaunga, nyumba kubwa, Kongosho, nivea, FP , snowhite, gfsonwin, FP na wengineo mpeane kitchen party ya ukubwani! Si jambo jema kuchukua hatua unazozifikiria.
Kila la kheri,
HorziPawa.
thanx kwa ushauri wako, yani unajua nimechanganyikiwa live..