Huyu mtu ananifaa kweli au niachane nae

Huyu mtu ananifaa kweli au niachane nae

niwe mkweli mimi nilikuwa kama chris wako, nilikuwa muasherati na hata baada ya ndoa nikawa mzinzi sana. hapo ulipo jua kuwa unazini na adhabu yake ni moto wa milele, ukifa sasaivi unaenda motoni moja kwa moja, shida ni kwamba haujui utakufa lini, leo, usiku huu, kesho au lini, umejiandaaje? unabahatisha maisha uishi kwa bahati nasibu kwamba nikiishi basi nisipoishi basi wakati Mungu amekupa uzima ambao ni opportunity ya kupanga na kuchagua?

kuna siku Mungu alinifunulia hicho nilichokiandika hapo juu, nikaogopa sana, nikapiga magoti nikatubu dhambi zangu, nikajiunga na wokovu na kuwa mwokovu hadi kesho na kuendelea, sitaacha wokovu. ndio maana nakuandikieni hata ninyi, sio kwamba nahukumu bali nawashauri muache michezo hiyo. pamoja na dhambi hizo za uasherani, Mungu anakuona, ila ameandaa njia ya wokovu kwa Yesu Kristo, alimwaga Damu ili ukitubu akusamehe uzinzi wake wote, ila kama hautatubu utabaki na dhambi zako na ukifa ni motoni moja kwa moja. mwogope Mungu, Yusufu alisema nimtendeje Mungu dhambi kubwa namna hii? dhambi ya sirini uzinzi ambao hata angefanya asingejulikana ila akajua Mungu anamwona amtendeje Mungu anayemuona kila kitu dhambi ya uzinzi ile? kwanini umsaliti Mungu anayekuona tangu unavua ngua hadi uchafu wote, dharau gani hizo kwa Mungu aliyekukataza usifanye hayo na wewe bado unafanya tena kwa makusudi? tumaini lako ni nini hapo ulipo?

TITO 2:11 inatuaburu kuukataa ubaya natamaa za dunia,na tuach euovu, INASEMA: Maana neema ya Mungu iwaokoayo wanadamu wote imefunuliwa; 12 nayo yatufundisha kukataa ubaya na tamaa za kidunia; tupate kuishi kwa kiasi, na haki, na utauwa, katika ulimwengu huu wa sasa; 13tukilitazamia tumaini lenye baraka na mafunuo ya utukufu wa Kristo Yesu, Mungu mkuu na Mwokozi wetu; 14ambaye alijitoa nafsi yake kwa ajili yetu, ili atukomboe na maasi yote, na kujisafishia watu wawe milki yake mwenyewe, wale walio na juhudi katika matendo mema.

Amua leo, okoka, ama la hukumu ipo juu yako. UFUNUO 14:13 INASEMA: Nikasikia sauti kutoka mbinguni ikisema, Andika, Heri wafu wafao katika Bwana tangu sasa. Naam, asema Roho, wapate kupumzika baada ya taabu zao; kwa kuwa matendo yao yafuatana nao.

usidanganywe na mapadre na wachungaji wanaosema ukifa wataiombea maiti yako nayo itasamehewa dhambi. Mungu amekupa nafasi ya kutengeneza mambo yako ungali hai, ukifa ndio deadline yako ya kutubu, hapo juu Biblia inasema ukifa utaenda na matendo yako. sehemu zingine anasema baada ya kufa ni hukumu. baada ya kufa sio kutubu, unatubu vipi sasa wakati maisha yako ya hapa duniani yameisha? na kama nafasi hiyo ingekuwepo Mungu asingesema tusifanye dhambi kwasababu angejua hata tungefanya siku tunakufa ndugu zetu huwa wanahuzunika sana lazima tu wangetutubia dhambi badala yetu. lakini sio hivyo, hata waombe na kufukiza uvumba namna gani huwezi kusamehewa baada ya kifo, nafasi yako ya kutengeneza na Mungu imekoma, matendo yako utaenda nayo, utahukumiwa nayo. hapa ndipo penye hekima na busara ya watakatifu, wewe unayetaka kuwa mtakatifu pambana kuyakimbia makanisa ya aina hiyo yanayofundisha watu kuwa watawazika vizuri kwa kuwaombea, hayo ya katoliki na mengine, ni uongo wa shetani, ndio maana mmeshikwa masikio mnaogopa mapadre na wachungaji kama nini kwasababu mnaogopa nani atawazika, kwani mkiliwa na mamba au simba nani atawazika? mkiungua moto au kupotea na ndege hewani nani atawazika? akili zenu zimeenda wapi ndugu zangu. Mwogopeni Mungu, tubuni mkaiamini Injili ya kweli, nanyi mtapata kipawa cha Roho Mtakatifu awaongoze muishi maisha matakatifu ili mkaurithi uzima wa milele, ama la hukumu ya Mungu ipo juu yenu. Heshima na utukufu kwa Mwanakondoo wa Mungu, Kwa Jina la Yesu!

Nilikuwa huko mkuu walokole wakanitenda sasa sitaki mwanaume wa kujifanya mlokolee nataka mwanaume mcha Mungu
 
Kwa haraka haraka umejawa tamaa ya fedha ewe mwanamke acha Chris akupelekee moto alale mbele safari hii na yeye siyo boya amerudi kajipanga..
 
Hivi ndoa ya serikali nikitaka kufunga inaweza kuwa ya siri yaani nijue mimi na mtu wangu bila mashahidi wenginee… maana kwa kazi yake kwasasa bado muda
Hakuna cha ndoa ya siri; iwe ya Kiserikali au ya Kidini. Kabla ya ndoa kufungwa (serikalini na kidini) lazima tangazo liwekwe (Marriage ban) ubaoni kwa kipindi fulani na kanisani na misikitini lazima matangazo yafanywe mara kadhaa. Siku ya arusi, arusi lazima ifungwe mahali pa wazi na mtu yo yote anaruhusiwa kuhudhuria bila kuhitaji mwaliko wo wote. Ni kwenye ukumbi wa kusherehekea tu ndiyo unaweza kumkataza mtu kuingia kama hujamualika. Lakini kanisani, msikitini au kwenye ofisi ya serikali panapofungishwa ndoa mtu yo yote anaruhusiwa kuhudhuria. Hivyo basi, hakuna ndoa ya siri.
 
Nilikuwa huko mkuu walokole wakanitenda sasa sitaki mwanaume wa kujifanya mlokolee nataka mwanaume mcha Mungu
bahati mbaya, hakuna mwanaume mcha Mungu nje ya walokole. inaonekana kwa bahati mbaya ulikutana tu na mnafiki mmoja aliyekua hajaokoka ila ameingia kwa walokole ili kutafuta kitu, wapo wengi pia, utawatambua kwa matunda yao, ndio maana inaonekana mlikuwa kwenye ulokole na bado mkawa na mahusiano ya uasherati, kama mlifanya uzinzi mkiwa kwenye wokovu nyote hamkuwa walokole, mlikuwa wanafiki tu. kwasababu ulishasogezwa eneo unaloweza kumjua Mungu ilikuwa nafasi yako muhimu sana kuutafuta uso wa Mungu hadi uupate na umwombe akupe mwenza mwema kulingana na wewe ulivyo.

nakuhakikishia, kama unaenda kwa macho ya kibinadamu hivyo, nakuombea kwa Mungu usilete ushuhuda mwingine hapa wa kupopolewa za uso. hakuna mtu aliyewahi kuijua njia ya kweli akaiacha na kuitukana akafuata njia nyingine ya upotevuni akafanikiwa, HAJAWAHI KUWEPO. mark my words.

pia, ninyi mnaookoka, msirudishwe nyuma na watu wanafiki au wadhaifu waliopo kwenye kundi la walokole. jueni kuwa ulokole ni imani tu iliyopo kwenye madhehebu fulani, ni imani ya kuokoka ndio maana tunaitwa walokole, na ni imani nzuri kwasababu inakuelekeza kwenye imani ile ile waliyokuwa nayo mitume kwenye kanisa la kwanza, misingi ni ileile. hii ina maana kwamba faida yako wewe ni kuwepo sehemu inayosimamia ile misingi ili ikusaidie umwone Mungu misingi mingine ya kuabudu maria na wafu au mood haiwezi kukufanya umwone Mungu, ukiisimamia ile misingi ya walokole, lazima utamwona Mungu, ukiokoka na hauisimamii ile misingi, wewe hautakuja kumwona Mungu na ni sawa tu na wanafiki wa duniani. misingi yenyewe ni Kumkiri Yesu kwa kinywa na kuamini, kujazwa na kutembea na Roho Mtakatifu na kuendelea kupalilia au kutomkwaza Roho ili awepo, akiondoka pambana arudi, kujiunga na watu wenye imani moja na wewe kwasababu Biblia inasema hatuwezi kuchangamana na watu wasioamini kwa jinsi isivyo sawasawa hakuna urafiki kati ya nuru na giza, kuhudhuria ibada kwasababu walipo wawili watatu wamekusanyika kwa jina langu Mungu yupo na kufanya mapendi ya Mungu kwa uongozi wa Roho. huyo ndio mlokole. ukiishi kwenye ulokole huna Roho, wewe unasindikiza. ndo hao wanafiki wanaumiza watu mioyo. na hawawezi kukosekana na hata wakiwepo haimaanishi wokovu ni imani au kundi baya, ni huyo binafsi yake amepoteza muda kuwepo kwenye kundi lenye misingi ya Kimungu ila yeye amefuata misingi isiyo ya Mungu.

pia, wapo watu wanaokoka na bado wachanga, hao ni kama watoto wachanga, wengine wametoka kwenye umalaya hivyo hadi kuja kukombolewa kamili inachukua muda anaweza kuendelea kupambana na ile dhambi ya uzinzi, wengine wauaji na wakatili ile ukatili anapambana nayo na inaweza kujirudia ikamshinda akawa katili, wengine wezi anaweza kuiba tena n.k, hadi pale atakapofundishwa vya kutosha kwa maana ya kunywesha maziwa kama mtoto akamjua Mungu na kusimama mwenyewe, katika utoto anaweza kutenda dhambi na hiyo haimaanishi ulokole ni mbaya. ni sawa na mtoto wako akijisaidia hovyo huwezi kusema sio mtoto wako, kuna siku atakua tu.

kwahiyo msitukane au msitegemee mnapookoka mnaenda kukutana na malaika, noo, mnaenda kukutana na kundi la watu waliokuwa wenye dhambi za kutisha kama ulivyo wewe ila wameamua kumpokea Yesu na wanapambana kuzikimbia dhambi pamoja na wewe, kuna wakati wanalemewa na kusimama tena, cha muhimu wameamua kumfuata Yesu, na huwa inafika wakati wanashinda na kuimarika mazima. kwenye ulokole kuna wazinzi waliokuwa wamekubuhu, wadhurumaji, wauaji, majambazi, wauza unga, wavuta madawa, kila kitu kipo ila wameamua kuokoka. wangekuwa walikuwa watakatifu basi wasingekuwa na umuhimu wa kuokoka.

ukimwacha Yesu hujamkomoa mtu, umejikomoa wewe na future yako ya milele na hautafanikiwa nje ya Yesu kwa hicho unachokitafuta.
 
Mabinti tunapitia mambo magumu sana sema hamuelewi mnatupa lawama… imagine umetulia na mtu unaamini atakuoa upo nae peke yake mara ghafla kabadilika

Ni vile tu sisi tunaolewa hatuoi so hatuwezi kupanga ndoa
Ukiona mwanaume kakuacha ujue si mjinga kakuona ufuhi kuwa mke wake, sisi wanaume tuna kawaida moja tunapokuwa kwenye mahusiano tunajua huyu ni mwanamke wakupita au wakuishi nae? Kulikana na wewe utavyokuwa unabehave
 
bahati mbaya, hakuna mwanaume mcha Mungu nje ya walokole. inaonekana kwa bahati mbaya ulikutana tu na mnafiki mmoja aliyekua hajaokoka ila ameingia kwa walokole ili kutafuta kitu, wapo wengi pia, utawatambua kwa matunda yao, ndio maana inaonekana mlikuwa kwenye ulokole na bado mkawa na mahusiano ya uasherati, kama mlifanya uzinzi mkiwa kwenye wokovu nyote hamkuwa walokole, mlikuwa wanafiki tu. kwasababu ulishasogezwa eneo unaloweza kumjua Mungu ilikuwa nafasi yako muhimu sana kuutafuta uso wa Mungu hadi uupate na umwombe akupe mwenza mwema kulingana na wewe ulivyo.

nakuhakikishia, kama unaenda kwa macho ya kibinadamu hivyo, nakuombea kwa Mungu usilete ushuhuda mwingine hapa wa kupopolewa za uso. hakuna mtu aliyewahi kuijua njia ya kweli akaiacha na kuitukana akafuata njia nyingine ya upotevuni akafanikiwa, HAJAWAHI KUWEPO. mark my words.

pia, ninyi mnaookoka, msirudishwe nyuma na watu wanafiki au wadhaifu waliopo kwenye kundi la walokole. jueni kuwa ulokole ni imani tu iliyopo kwenye madhehebu fulani, ni imani ya kuokoka ndio maana tunaitwa walokole, na ni imani nzuri kwasababu inakuelekeza kwenye imani ile ile waliyokuwa nayo mitume kwenye kanisa la kwanza, misingi ni ileile. hii ina maana kwamba faida yako wewe ni kuwepo sehemu inayosimamia ile misingi ili ikusaidie umwone Mungu misingi mingine ya kuabudu maria na wafu au mood haiwezi kukufanya umwone Mungu, ukiisimamia ile misingi ya walokole, lazima utamwona Mungu, ukiokoka na hauisimamii ile misingi, wewe hautakuja kumwona Mungu na ni sawa tu na wanafiki wa duniani. misingi yenyewe ni Kumkiri Yesu kwa kinywa na kuamini, kujazwa na kutembea na Roho Mtakatifu na kuendelea kupalilia au kutomkwaza Roho ili awepo, akiondoka pambana arudi, kujiunga na watu wenye imani moja na wewe kwasababu Biblia inasema hatuwezi kuchangamana na watu wasioamini kwa jinsi isivyo sawasawa hakuna urafiki kati ya nuru na giza, kuhudhuria ibada kwasababu walipo wawili watatu wamekusanyika kwa jina langu Mungu yupo na kufanya mapendi ya Mungu kwa uongozi wa Roho. huyo ndio mlokole. ukiishi kwenye ulokole huna Roho, wewe unasindikiza. ndo hao wanafiki wanaumiza watu mioyo. na hawawezi kukosekana na hata wakiwepo haimaanishi wokovu ni imani au kundi baya, ni huyo binafsi yake amepoteza muda kuwepo kwenye kundi lenye misingi ya Kimungu ila yeye amefuata misingi isiyo ya Mungu.

pia, wapo watu wanaokoka na bado wachanga, hao ni kama watoto wachanga, wengine wametoka kwenye umalaya hivyo hadi kuja kukombolewa kamili inachukua muda anaweza kuendelea kupambana na ile dhambi ya uzinzi, wengine wauaji na wakatili ile ukatili anapambana nayo na inaweza kujirudia ikamshinda akawa katili, wengine wezi anaweza kuiba tena n.k, hadi pale atakapofundishwa vya kutosha kwa maana ya kunywesha maziwa kama mtoto akamjua Mungu na kusimama mwenyewe, katika utoto anaweza kutenda dhambi na hiyo haimaanishi ulokole ni mbaya. ni sawa na mtoto wako akijisaidia hovyo huwezi kusema sio mtoto wako, kuna siku atakua tu.

kwahiyo msitukane au msitegemee mnapookoka mnaenda kukutana na malaika, noo, mnaenda kukutana na kundi la watu waliokuwa wenye dhambi za kutisha kama ulivyo wewe ila wameamua kumpokea Yesu na wanapambana kuzikimbia dhambi pamoja na wewe, kuna wakati wanalemewa na kusimama tena, cha muhimu wameamua kumfuata Yesu, na huwa inafika wakati wanashinda na kuimarika mazima. kwenye ulokole kuna wazinzi waliokuwa wamekubuhu, wadhurumaji, wauaji, majambazi, wauza unga, wavuta madawa, kila kitu kipo ila wameamua kuokoka. wangekuwa walikuwa watakatifu basi wasingekuwa na umuhimu wa kuokoka.

ukimwacha Yesu hujamkomoa mtu, umejikomoa wewe na future yako ya milele na hautafanikiwa nje ya Yesu kwa hicho unachokitafuta.

My dear mimi nilichumbiwa kabisaa na Kijana tunasali kanisa tofauti uchumba ulitangazwa kanisani mpk kikao cha kwanza cha harusi kilifanyika kilichotokea uchumba ukavunjwa yule jamaa kumbe alimtia mwanamke mwinginee mimbaa kipindi tunatangaza uchumba mwanamke alikuwa na mimbaa ya miezi 8… huyo kijana alikana kabisa kwamba hajampa mimba jambo liliposhikiliwa sawasawa jamaa akakubali kuwa ni kweli mimba yake

Hivi imagine hiyo aibu aliyonitiaa kwa ndugu, majirani na marafiki…

Kwa kifupi ndugu mimi nimezaliwa huko nimekulia huko ila kwa sasa sitaki kusikia habari za wanaume wa lokoleee hakuna kitu ni walaghai tu
 
My dear mimi nilichumbiwa kabisaa na Kijana tunasali kanisa tofauti uchumba ulitangazwa kanisani mpk kikao cha kwanza cha harusi kilifanyika kilichotokea uchumba ukavunjwa yule jamaa kumbe alimtia mwanamke mwinginee mimbaa kipindi tunatangaza uchumba mwanamke alikuwa na mimbaa ya miezi 8… huyo kijana alikana kabisa kwamba hajampa mimba jambo liliposhikiliwa sawasawa jamaa akakubali kuwa ni kweli mimba yake

Hivi imagine hiyo aibu aliyonitiaa kwa ndugu, majirani na marafiki…

Kwa kifupi ndugu mimi nimezaliwa huko nimekulia huko ila kwa sasa sitaki kusikia habari za wanaume wa lokoleee hakuna kitu ni walaghai tu
ndio maana nimesema wewe na yeye wote mlikuwa wazinzi tu na hamkuokoka, ila mlikuwa wana dini. ungeokoka ungejua kuwa Mungu alikuepusha na mtu mbaya hivyo ungeshukuru, na walokole mtu akifanya hivyo huwa wanaweka wazi ila kwengine huko ndoa ingeendelea na ungeingia kwenye moto huo. wapi kuzuri sasa?
 
ndio maana nimesema wewe na yeye wote mlikuwa wazinzi tu na hamkuokoka, ila mlikuwa wana dini. ungeokoka ungejua kuwa Mungu alikuepusha na mtu mbaya hivyo ungeshukuru, na walokole mtu akifanya hivyo huwa wanaweka wazi ila kwengine huko ndoa ingeendelea na ungeingia kwenye moto huo. wapi kuzuri sasa?

Wewe hatukuwai kuzini na huyo kaka kwasababu alikuja yupo serious na mimi nilikuwa na 21 yr so sikuwah hata jihusisha na uhusiano… huyo kaka tuliachana swafi bila uzinifu sema ndio alieniumiza kihisia na siwezi tena amini kijana mlokole
 
Huyu kijana tulidate kama miezi 2 tu nikamuacha tumwite chris,, sababu nilikuwa na mpnz wangu ambae alikuwa nnje ya nchi kwa wakati huo… Sikupanga kumcheat ni ile tu sikuwa na uhakika na huyo mpnz wangu wa nnje ya nchi maana hatukuwai kuonana live ilikuwa ni mahusiano ya mtandaoni

Kwa kipindi hicho sikuwa na mahusiano yoyote zaidi ya huyo mwanaume wa nnje ya nchi…. Kama unavojua mwanamke na mwanaume wakikaa pamoja sumaku huvutana

Kwa kipindi hiko sikuwa nampenda yoyote kati yao maana sikuzingatia… ukaribu na chris tukajikuta nimempa tunda, hilo jambo nilijutia sana kwasababu sikuwa nikimpenda halafu jamaa sijui ndio akazama kwangu, akaanza kuwa msumbufu mpk kukeraa, nikamdanganya nina ujauzito wake ili tu nile pesa ake kweli kaka akajitoa sana kwa harakaharaka ndani ya hiyo miezi 2 nilishatumia zaidi ya laki 9 (alinitengenezea bima, account ya benk kila mwezi anaweka laki 2 hii ilikuwa kwaajili ya maandalizi ya kujifungua alisema niwe natunza nilipokea miezi2 tu).

Baada ya miezi 2 nikamwambia mimba imetoka jamaa alilaumu sana akisema nimetoa ila mimi nilikazana imetoka basi bhn nia ilikuwa ni kumuacha ili nibaki na mwanaume wangu wa siku zote maana alionesha malengo japo hatukuwai kuonana… nilifanikiwa kumuacha yule kaka (chris) japo alikuwa king’ang’anizi.

Mpnz wangu wa nnje alirudi tukaonana na mipango ikaendelea na alikuwa akinipenda sana but kama mnavojua mipango si matumizi yule kaka sipo nae tena (siwezi kuelezea kilichotokea maana nitafungua code ila hatuna mahusiano kabisa kabisa) ila hatukuachana kwasababu za usaliti au uongo ni sababu za kimungu tu.

Kwa sasa nimerudi kwa chris japo mguu pande kwasababu sijamuamini kiivo… kuna jambo alimwambia rafiki yake kwamba mimi alinifumania jambo ambalo sio kweli na nimeshangaa ni kwanini amemwambia rafiki ake hivyo kwamba alinipigia simu usiku akasikia sauti ya mwanaume anauliza naongea na nani( jamaani wananchi ilo jambo ametunga si kweli).

Sasa nimewaza huyu jamaa sio kwamba karudi kulipa kisasi kwangu nilivyomuacha
Mimi nilimuacha kwasababu ana akili za kitoto mfano akipiga simu upokee hapo hapo kama hupokei atapiga hata mara 20 mpk nikawa naogopa ukipikea sasa zinaanza lawama hii hali ya kulaumiwa kila siku nikaichoka yaani tuna miezi 2 ila kama miaka ndio ikapelekea nimuache.

Kilichonirudisha kwake ni kwakuwa sina mtu ninaemuelewa kwa sasa then nimeona kama yeye ananipenda japo mimi still nasuasua.

Ila sasa hivi amekuwa bahili hata vocha ni kusumbuana… anachosema mimi sieleweki kigeugeu ili aniamini anataka tuzae mtoto

Wakuu ushauri kuhusu huyu mtu nifanyaje?
Kama waolewaji wenyewe ndo hawa, naomba nitangaze rasmi kujiunga team kataa ndoa.

I hope Chris hatowaangusha singo mazaz kwa kuwaongezea mwanachama mmoja soon.

dronedrake naomba utaratibu wa kadi ya chama.

##kataandoa##
##ndoaniwizi##
##ndoaniutapeli##
##ndoaniujambaz########
 
Nilikuwa huko mkuu walokole wakanitenda sasa sitaki mwanaume wa kujifanya mlokolee nataka mwanaume mcha Mungu
😁😁😁we kila angle umekutana na balaa tu, Hadi walokole wamekunyoosha?
 
Nimeuliza Kama karudi kwangu kulipa kisasi ama…
Tulikulana mara moja tu… amesema amechoka mahusiano ya kupeana hela halafu namnyima uchi ndio kawa bahili

Mambo ya mimba ni kwa kuwa alisema aniamini tena naweza kumgeuka ili aniamini anipe mimbaa
Yaani miezi yote hiyo na hela zote hizo halafu nikulale mara moja!?

Hii aidha ni chai, au huyo Chris ni hanith aliyechangamka
 
Huyu kijana tulidate kama miezi 2 tu nikamuacha tumwite chris,, sababu nilikuwa na mpnz wangu ambae alikuwa nnje ya nchi kwa wakati huo… Sikupanga kumcheat ni ile tu sikuwa na uhakika na huyo mpnz wangu wa nnje ya nchi maana hatukuwai kuonana live ilikuwa ni mahusiano ya mtandaoni

Kwa kipindi hicho sikuwa na mahusiano yoyote zaidi ya huyo mwanaume wa nnje ya nchi…. Kama unavojua mwanamke na mwanaume wakikaa pamoja sumaku huvutana

Kwa kipindi hiko sikuwa nampenda yoyote kati yao maana sikuzingatia… ukaribu na chris tukajikuta nimempa tunda, hilo jambo nilijutia sana kwasababu sikuwa nikimpenda halafu jamaa sijui ndio akazama kwangu, akaanza kuwa msumbufu mpk kukeraa, nikamdanganya nina ujauzito wake ili tu nile pesa ake kweli kaka akajitoa sana kwa harakaharaka ndani ya hiyo miezi 2 nilishatumia zaidi ya laki 9 (alinitengenezea bima, account ya benk kila mwezi anaweka laki 2 hii ilikuwa kwaajili ya maandalizi ya kujifungua alisema niwe natunza nilipokea miezi2 tu).

Baada ya miezi 2 nikamwambia mimba imetoka jamaa alilaumu sana akisema nimetoa ila mimi nilikazana imetoka basi bhn nia ilikuwa ni kumuacha ili nibaki na mwanaume wangu wa siku zote maana alionesha malengo japo hatukuwai kuonana… nilifanikiwa kumuacha yule kaka (chris) japo alikuwa king’ang’anizi.

Mpnz wangu wa nnje alirudi tukaonana na mipango ikaendelea na alikuwa akinipenda sana but kama mnavojua mipango si matumizi yule kaka sipo nae tena (siwezi kuelezea kilichotokea maana nitafungua code ila hatuna mahusiano kabisa kabisa) ila hatukuachana kwasababu za usaliti au uongo ni sababu za kimungu tu.

Kwa sasa nimerudi kwa chris japo mguu pande kwasababu sijamuamini kiivo… kuna jambo alimwambia rafiki yake kwamba mimi alinifumania jambo ambalo sio kweli na nimeshangaa ni kwanini amemwambia rafiki ake hivyo kwamba alinipigia simu usiku akasikia sauti ya mwanaume anauliza naongea na nani( jamaani wananchi ilo jambo ametunga si kweli).

Sasa nimewaza huyu jamaa sio kwamba karudi kulipa kisasi kwangu nilivyomuacha
Mimi nilimuacha kwasababu ana akili za kitoto mfano akipiga simu upokee hapo hapo kama hupokei atapiga hata mara 20 mpk nikawa naogopa ukipikea sasa zinaanza lawama hii hali ya kulaumiwa kila siku nikaichoka yaani tuna miezi 2 ila kama miaka ndio ikapelekea nimuache.

Kilichonirudisha kwake ni kwakuwa sina mtu ninaemuelewa kwa sasa then nimeona kama yeye ananipenda japo mimi still nasuasua.

Ila sasa hivi amekuwa bahili hata vocha ni kusumbuana… anachosema mimi sieleweki kigeugeu ili aniamini anataka tuzae mtoto

Wakuu ushauri kuhusu huyu mtu nifanyaje?
Wewe ni tapeli, unakulaje hela ya mwanaume kwa uongo? Mwizi mkubwa wewe, ndomaana watu wanasema wanawake wote ni mashetani, sijui mliongea Nini na shetani kule eden, chakufanya toa uchi kwa jamaa, akupigdakupige miti mpaka laki tisa yake irudi, dawa yenu msiojielewa kama nyie ni kupiga pumbu tu.
 
Wewe hatukuwai kuzini na huyo kaka kwasababu alikuja yupo serious na mimi nilikuwa na 21 yr so sikuwah hata jihusisha na uhusiano… huyo kaka tuliachana swafi bila uzinifu sema ndio alieniumiza kihisia na siwezi tena amini kijana mlokole
ok, basi tafuta walevi, wazinzi huko barabarani, na waganga wa kienyeji alafu utaleta mrejesho siku moja hapa. Mungu akusaidie.
 
ok, basi tafuta walevi, wazinzi huko barabarani, na waganga wa kienyeji alafu utaleta mrejesho siku moja hapa. Mungu akusaidie.

Kwani ndugu wasiokoka wote ni walevi, wazinzi ama ni waganga ndugu kuna wanaume wazuri sana na vyote ulivyotaja hawana mfano mzuri ni kornelio yeye alikuwa mtu wa aina gani??

Tatizo mnaojiita walokole wengi wenu ni wanafkii mnafikiri nyie mbingu ni ya kwenu peke enu

Hubiri injili ila sio kuwakashfu watu as if wasiookoka wote ni. Wachawi
 
Back
Top Bottom