Ulukolokwitanga
JF-Expert Member
- Sep 18, 2010
- 8,396
- 7,968
Mrembo nimemfuatilia kwa muda mrefu sana hatimaye kaamua kunipa tunda, cha kushangaza baada ya kula tunda mrembo kaniuliza "una mpango gani na mimi? Nami nikamuuliza unataka mpango gani toka kwangu hakunijibu. Toka siku hiyo anakuwa haeleweki eleweki kuwa anataka nini? Tunda ananinyima. Nimemuuliza kama anataka Vitz hasemi kitu, nimlipie kodi ya nyumba? Ameniboa. Nimejikuta natinga kwenye hili jukwaa kwa mara ya kwanza ili wadada wazoefu na mahusiano mnisaidie kujua huyu mrembo anataka mpango gani toka kwangu? Ila ushauri kwa wadada ni kuwa go straight to the point unataka nini badala ya kujizungusha kama traffic anayetaka rushwa ila anashindwa kusema straight anatumia vitisho. Kama anataka ndoa si aseme, na ndoa gani inatangazwa kabla hamjajuana vizuri, tunda mara moja...