Huyu binti ananifanya nikonde

Huyu binti ananifanya nikonde

i wish ningekuwa mimi maaana nimeongeza weight sana kipindi hiki nataman kupungua bila kufanya mazoezi
 
Pole sana...

Nyie wate ni sitaki nataka... Ila mnapendana... Kama unampenda tafuta namna ya kumtuliza... Do what a man gat to do... Kupenda siyo vibaya ila penda huku ukitumia akili pia...

Follow your heart but take your brain with you... Moyo ukishapenda ni vigumu kushaurika...


Cc: mahondaw
 
Ndugu zangu awali ya yote napenda kumshukuru Mungu kwa kuniweka salama siku ya leo japo hapa nilipo pressure ipo juu kweli kwasababu ya binti ambaye kwa dhati ya moyo wangu niweke wazi napenda sana awe mama watoto wangu kwa muda ambao yeye atakuwa tayari mimi nipo tayari muda wowote.

Kilicho nisukuma kuandika uzi huu ni hali ngumu na mawazo anayonipa huyu binti sio uwongo ananidengulia sana, ni mwanamke niliye dumu naye kwenye uhusiano kwa kipindi kisichopungua miezi mitatu lakini nimetokea kumpenda mpaka nimefikia hatua ya kutaka kuoana naye na akanikubalia. Lakini kwa siku za karibuni zisizozidi wiki mbili amekuwa mtu asiyeeleweka kwa maana ya kwamba anatuma sms ananiambia tuachane kwa mda kwanza alafu tuendelea baadaye hivyo hivyo nalia lia mpaka anabadilisha mawazo. Lakini hiyo tabia ilijirudia kwa mara tatu na mara ya nne nikapiga moyo konde japo naumia moyo nijamjibu kuwa asiwe na tatizo nimekubali kuachana nae kama anavyohitaji.

Lakini leo asubuhi akatuna sms kwamba hakumaanisha bali ni utani tu na mimi nikamwambia HAPANA acha iwe kama ulivyohitaji mwanzo, akajibu POA.

Lakini ndugu zangu niwe muwazi ili mnishauri vyema huyu binti nampenda sana sana ila niliamua tu kutikisa kiberiti na mimi. Je kuna uwezekano ananipenda au ashaniona kilaza na kunifanya mdoli?

Tafadhali nahitaji ushauri wenu.
Huyo demu anatikisa kiberitii tuu mimi ilishawahi kunitokea hivyo kwa msichana mmoja hiv ilikua hivyo hivyo kama baadae nikamwambia sawa tuachane na tena nikamwambia sitaki hata masiliano naye.

Lakini cha kushangaza baada ya siku moja tuu aliniambia alikua ananitega ili anione kama nampenda na toka hapo hajawahi kurudia tena huo mchezo coz alikiona cha moto.

Hapo mkuu wew fanya kama unamkazia vile atakuja mwenyewe kukuomba msamaha tena na machoziii.
 
Wewe fuata moyo wako, usitusikilize sisi. Sometimes ni muhimu uji sacrifice kwa unayempenda!
 
umeonja walau?? Nakushauri tu usipende kumuonyesha mwanamke kwamba unampenda saana atakufanya Ngiri
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom