Huyu baba mkwe simwelewi anataka Nini?

Huyu baba mkwe simwelewi anataka Nini?

Kulingana na maelezo ya Uzi wako, bila kukuficha ni kwamba umeonyesha tamaa ya mali za Jamaa na unalazimisha kuwa legal ili uwe sehemu ya mali hizo.

Unaonekana unalazimisha kufunga ndoa uli uwe sehemu ya umiliki Wa mali hizo. Utu uzima ni dawa Mzee kashakusoma kuwa unatumia nguvu nyingi kulazimisha ndoa, ula huyo zumbukuku wako hajatambua coz umemuweka kwapani.

Na kwa jinsi unavyoandika kwa baba mkwe inaonekana una matatizo sana ya kinidhamu ila ujitambui. Ova ova ovaa gonga like wadau twende zetu asituchoshe huyu gold digger.
 
Mwenzenu naomba ushauri huyu baba mkwe simwelew kabisa

Iko hivi
Nimeanza kuishi na huyu mwanaume mwaka Jana baada ya kukamilisha process zote ikabaki kufunga ndoa tu

Ilipofikia mda wa kufunga ndoa baba mkwe akaja nyumbani kwa wazazi wangu pamoja na wazee wengine 2, akaomba nije niishi na mwanae uchumi wake haujakaa vizur anategemea kilimo ivyo anaomba mwaka huu tufunge....
Nilikubali kwa sababu alizozitoa kwamba mwanae kahamishwa kikaz so anaomba ahame na mkewe ambae Ni Mimi
Ok imefika mwaka huu Mimi na mwenzangu tukaanza kujiandaa pamoja na kusave pesa tukiamin mwaka huu tutafunga ndoa..

Mwez wa 6 mwenzangu akaenda Kijijini kumwambia mzee nataka nifunge ndoa mwaka huu,,. Baba mkwe akadai anataka afanye sherehe ivyo tumpe muda kidogo atatupa jibu
Juz tena mwenzangu kaenda kijijin kaita kikao Cha baadhi ya ndugu zake pamoja na wazazi wake akamwambia mzee vp nataka nifunge ndoa
Baba akadai sijajipanga vzuri tufanye mwaka kesho kwa Sasa Sina hela, mwenzangu akamwambia baba Mimi pesa ninayo we kama unataka unifanyie sherehe andaaa tu mi nitakuwezesha
Baba kakataa et umenifanyia makubwa Sana leo na ndoa ufunge kwa pesa yako hapana hela yako kafanyie vitu vingine Mimi najipanga mtafunga mwakakesho
Kabembelezwa Sana na baadhi ya ndugu kakataa kabisa anadai tusubir...

Tumejadilian na mwenzangu kwamba tufunge tu sisi bila kufanya sherehe then Kama yeye anataka sherehe atatufanyia mwaka kesho.,,,,, Bado tumemwambia hataki anadai Kama mmeamua hivyo fanyen ila msinishirikishe Mimi
Mi nachotaka mtulie mtafunga mwaka kesho

Waungwana naomben ushaur tufanyeje? kumbuka nimeanza kuishi na huyu mwanaume mwaka Jana bila ndoa kadai mwaka huu ,,
Mwaka umefika hataki tena anadai mwaka kesho ... nifanyeje??
Anataka ajue kama ilichezea usichana wako na huzai ndiyo basi tena atasamehe ata mahari..
 
Ukisikia shangazi anakwambia huyu mtoto Masikio hayafanani na familia kama mwanaume unahitaji jiongeza....KUNA KITU HUWI MWAZI NA BABA MKWE HATAKI MPOTEZA MWANAYE...ukweli mchungu
 
Ili Jambo wote tumejadili kwa pamoja Wala sio Mimi nalalamika hata mwenzangu sababu nimwajiliwa ivyo Kuna vingi anakosa ,, mfano hata hela ya likizo anapewa kidogo vitu ni vingi istoshe sio Mimi ninaemkazinia mkuu
Yaani uoe kwa sababu ya hela za likizo?samahani naungana na huyo Mzee,kuna kitu tumekiona ila huyo jamaa yako bado amepofushwa na mapenzi
 
Wenzako wana mwaka wa 16 na watoto 3 hawajafunga ndoa na maisha yanasonga wewe unalalamikia vimiaka viwili? Fikiria maisha sio ndoa, huenda hapo upo katka usahili na huenda ukafeli kwa unavyoonekana mlalamishi mlalamishi wa vitu vidogo vinavyofaa kuvutiwa subira.
 
Mwenzenu naomba ushauri huyu baba mkwe simwelew kabisa

Iko hivi
Nimeanza kuishi na huyu mwanaume mwaka Jana baada ya kukamilisha process zote ikabaki kufunga ndoa tu

Ilipofikia mda wa kufunga ndoa baba mkwe akaja nyumbani kwa wazazi wangu pamoja na wazee wengine 2, akaomba nije niishi na mwanae uchumi wake haujakaa vizur anategemea kilimo ivyo anaomba mwaka huu tufunge....
Nilikubali kwa sababu alizozitoa kwamba mwanae kahamishwa kikaz so anaomba ahame na mkewe ambae Ni Mimi
Ok imefika mwaka huu Mimi na mwenzangu tukaanza kujiandaa pamoja na kusave pesa tukiamin mwaka huu tutafunga ndoa..

Mwez wa 6 mwenzangu akaenda Kijijini kumwambia mzee nataka nifunge ndoa mwaka huu,,. Baba mkwe akadai anataka afanye sherehe ivyo tumpe muda kidogo atatupa jibu
Juz tena mwenzangu kaenda kijijin kaita kikao Cha baadhi ya ndugu zake pamoja na wazazi wake akamwambia mzee vp nataka nifunge ndoa
Baba akadai sijajipanga vzuri tufanye mwaka kesho kwa Sasa Sina hela, mwenzangu akamwambia baba Mimi pesa ninayo we kama unataka unifanyie sherehe andaaa tu mi nitakuwezesha
Baba kakataa et umenifanyia makubwa Sana leo na ndoa ufunge kwa pesa yako hapana hela yako kafanyie vitu vingine Mimi najipanga mtafunga mwakakesho
Kabembelezwa Sana na baadhi ya ndugu kakataa kabisa anadai tusubir...

Tumejadilian na mwenzangu kwamba tufunge tu sisi bila kufanya sherehe then Kama yeye anataka sherehe atatufanyia mwaka kesho.,,,,, Bado tumemwambia hataki anadai Kama mmeamua hivyo fanyen ila msinishirikishe Mimi
Mi nachotaka mtulie mtafunga mwaka kesho

Waungwana naomben ushaur tufanyeje? kumbuka nimeanza kuishi na huyu mwanaume mwaka Jana bila ndoa kadai mwaka huu ,,
Mwaka umefika hataki tena anadai mwaka kesho ... nifanyeje??
Mahali umeshatolewa?,hebu nijibu hili tuendelee kushauriana vizuri
 
Hapo either baba mkwe hampendi mwali kwasababu zake mwenyewe au mwali hana sifa za kuwa mke lakini mzee hataki kufunguka.
Hii lugha sio nzuri kwa baba mkwe wako....

Samahani ila kuna tatizo mahali.
 
Yawezekana kabisa huyo baba mkwe amegundua mambo au vijitabia fulani Fulani ambavyo hapendezwi navyo, kwa hiyo anakuchunguza zaidi ili kujiridhisha na kuona kama umebadilika au hapana. Kitu cha msingi ni wewe mwanamke kwanza kujitathmini una kasoro au mapungufu gani ambayo yanamtia hofu/wasiwasi baba mkwe? Msiwe na papara wala jazba ktk kumshawishi baba mkwe ili akubaliane na uamuzi wenu, muwe na busara ktk kumshawishi, akiridhika moyoni mwake anaweza akabadili msimamo wake.

Pia kumbuka, ndoa siyo cheti bali ni upendo wa dhati kabisa kutoka moyoni mwa wanandoa, pamoja na kuwepo kwa mahusiano mema baina ya wanandoa wenyewe pamoja na ndugu zao wa karibu wa pande zote mbili za wanandoa, wazazi wakiwa wa kwanza.
 
Katika pitapita zangu zote, sijawahi kukutana na dhahma ya aina hii zaidi ya kinyume chake. Na nikienkuwaza zaidi nitajikuta nakutukania mkweo hata unione sina adabu, na nikiruhusu kufikiria zaidi nitajikuta nina kutukania mkeo na baba yake kwa neno ambalo litakuwa ni kukuudhi zaidi.
 
Ulikosea kukubali kuishi na huyo mwanaume bila ndoa.
 
Makosa ya wengine hayawezi kufanya kosa hilo lisiwe kosa.
Wenzako wana mwaka wa 16 na watoto 3 hawajafunga ndoa na maisha yanasonga wewe unalalamikia vimiaka viwili? Fikiria maisha sio ndoa, huenda hapo upo katka usahili na huenda ukafeli kwa unavyoonekana mlalamishi mlalamishi wa vitu vidogo vinavyofaa kuvutiwa subira.
 
Ilitakiwa aandikeje?
Hilo kwake analiona pungufu kwa baba mkwe wake kitu ambacho ni kweli kwa wengi hilo ni pungufu.

Ila kuna namna ya kuliwasilisha hata kwa watu wasiokujua. Sitaki kuongeza neno mwishowe nionekane nami sina heshima.
 
Back
Top Bottom