Huyo mke sio wako...

Huyo mke sio wako...

mediaman

JF-Expert Member
Joined
Mar 20, 2011
Posts
451
Reaction score
688
Ulifunga ndoa Kanisani, mkasherehekea sana harusi. Baada ya siku chache ukaachana na mke wako, kisha ukaoa mke mwingine. Haukupita muda mrefu ukampa talaka. Kwakuwa hukuweza kuishi peke yako ukaoa tena kwa mara ya tatu mke mwingine.

Utafanyaje ukisikia sauti ya Yesu inakuambia "huyo mke uliye naye sasa sio mke wako..." Utakuwa tayari kumwacha na kumrudia yule mke wa kwanza? Au utapuuza tu sauti hiyo na kujitetea sana?

Siku hizi ndoa nyingi zinavunjika, na watu wanapeana talaka kama risiti.

Katika kitabu cha Yohana 4:16-18
Yesu alimwambia mwanamke msamaria "...nenda kamwite mumeo, uje naye hapa. Yule mwanamke akajibu, Sina mume. Yesu akamwambia, Umesema vema, Sina mume; kwa maana umekuwa na waume watano, naye uliye naye sasa siyo mume wako; hapo umesema kweli."

Naamini hata leo kuna watu wengi wanaoisikia sauti ya Yesu ikiwaambia: huyo mke/mume sio wako, lakini wanajifanya hawasikii.
 
Hee, Aliyeumba viungo vyote vya mwili wako ashindwe kuwa mshauri wa ndoa? Jina jingine la Yesu ni Mshauri wa Ajabu.

Nyie Wakristo mna shida sana. Huyo Mtoto wa Maryam ambaye nyie mnamwita Yesu ndie aliyeumba viuongo vya mwili wa wanadamu ? Endeleeni kupotosha Wakristo wenzenu.
 
Nyie Wakristo mna shida sana. Huyo Mtoto wa Maryam ambaye nyie mnamwita Yesu ndie aliyeumba viuongo vya mwili wa wanadamu ? Endeleeni kupotosha Wakristo wenzenu.
Biblia ina mistari/aya nyingi zinazothibitisha wazi kuwa Yesu ni Mungu
 
Huyo Yesu tangu uzaliwe umewahi kusikia sauti yake?

Acha hilo, Yesu hakuwahi kuoa.... anawezaje kuwa mshauri wa mambo ya ndoa!
Hakimu mbona anatoa huku kwani yeye aliwahi kuhumiwa ??? Daktari je, anawatibu watu wanapona inamaana akiwahi kuugua ugonjwa huo.
 
Back
Top Bottom