Huu ufa kwenye hii ndoa unazibika?

Huu ufa kwenye hii ndoa unazibika?

Kuna wanawake kama wanakuamini sana ukiwasaliti hata akisema amekusamehe bado roho itaendelea kumuuma daima milele amina. Kuna ndoa fulani ambapo mke na mume wote ni rafiki zangu, mke classmate, mume roomate wa chuo, mke alikuwa anamuamini sana mume wake kiasi aliwahi kuniambia hata angeambiwa mwamba ameonekana anatoka guest house na demu, asingeamini. Siku alipofuma msg mumewe amemtumia ela mchepuke atoe mimba, ni mwaka wa tano ila things have never been the same again.
Wanaishi wote, wana kazi nzuri wote, mke anatimiza majukumu yote, wanatengeneza miradi wanasomesha watoto, yani wote wako vizuri sana kila moja ana take home si chini ya 4mls, lakini ni kama wanaishi kwa mazoea. Mume kajaribu sana weeka mambo sawa lakini wapi. Mke anasem yuko sawa na kamsamehe lakini mtu anayewajua anaona tu wanaigiza.
Very painful.
Sitaki tena haya masuala ya ndoa. Sitaki tena hata kuyasikia
 
Ili usaidiwe hebu funguka chanzo kilichopelekea kutetereka kwa ndoa yako sio kutuletea maelezo nusunusu tena ya kumlaumu mke wako ili uonekane malaika.
 
Furaha haipo tena wakuu nimedaiwa talaka na mke wangu usiku wa kuamkia leo, mimi mke bado namuhitaji. Chanzo cha yote(tatizo) ni mimi haihusiani na usaliti na tulishakaa vikao na familia tukayamaliza lkn mara zote toka hapo haijawahi kuisha wiki bila kununiana furaha siku 3 nne zillizobaki ni sintofahamu pamoja na kuwa anatimiza majukumu yake yote kama mke.

Usiku wa kuamkia leo baada ya kuniomba talaka yake alimpigia mama yake simu by 7 kasoro usiku kumueleza kuwa hana furaha tena! mama alikuwa na hamu ya kujua nini tatizo lkn binti alisisitiza siioni ndoa yangu tena na kukata simu ila kabla ya kukata alimuahidi kesho ntakuambia kila kitu.

Kwa hili sikuwa na namna sababu nilisharuhusu simu kupigwa japo baada ya kupiga simu nilimuomba usizungumze chochote na mama yako kuhusu hili wewe utajua namna ya kuongea ili kutuliza hali na ameniitikia kwa kunielewa, lkn sijui kichwani anawaza nini!

Nilimuahidi mimi pia nitazungumza na mama yake, jambo jingine nimemuomba nimuache peke yake kwanza nisafiri ili angalau upatikane muda wa utulivu kwanza lkn sio kumpa talaka.

Wanaume mafala mnateseka sana, kaa kimya akidai talaka mwambie aende kuanza procedures za mahakamani Kabisa.
 
Shida hasa ilikuwa pombe kiasi sikuwa nazingatia familia na hapo alikuwa mkoa mwingine kikazi hii ilileta shida kiasi hta nikashindwa kuheshimu amana zake sababu kunq wakati alipata eneo shamba nimnunulie na alinitumia milioni moja lkn sikuitimiza hii ahadi na ulitokea mzozo wa kudai talaka pia lkn tulikaa na familia tukamaliza hili kwa kuahidi kumrejeshea kiasi chake.Wakati huo mimi ni misheni town tu yy ni mujiriwa familia ikashauri itabidi ukaungane na mwenzio pmj nilikubalina na wazo hili nikajichukulia hakiba yangu kwanza nikamlipa kiasi chake nikabaki km na m hv ukiondoa maswala ya nauli na mahitaj mengine nikabakiwa km na laki 7 hivi so toka nimefika huku ni mwezi wa 4 sasa vtu havijaenda vile inavyotakiwa au ilivyopngwa.
Wiki iliyopita Kuna kiasi chake km 200000 hiv niliichukua na kumuahidi ntamrejeshea jna lkn sikutimiza hii ahadi, mara ghafla naona usiku vilio nauliza nini tatzo majibu ndio km hayo
Huu ugomvi kuhusu pesa ya mwanamke haupoi kabisa hasa kama ndio humsuport kwenye mambo yake
 
Hata sisi tusiokujua unatudanganya mambo uliyomfanyia mkeo? Acha ndoa ivunjike tu, Hakuna shida.
 
Pole sana kiongozi, hii taasisi ni ngumu mno na ku-survive inahitaji uvumilivu na upendo mwingi pia. Kama mke anasisitiza apewe talaka yake bila kutoa sababu hapo sababu itakuwa ni kuna mwamba mwingine ameanza kum-drive crazy kwahiyo wewe chakufanya hapo ni kumpa anachotaka
Kabisa! Ukigoma atakumaliza hili aende ulipo Moyo wake.Mwanamke akisema amekuchoka akutaki ...msikilize na mkubalie...Usije uka restishwa into peace
 
Ukweli ni kwamba kuishi na mwanamke muajiliwa wakati mume huna hela ni changamoto. Mkuu najua inauma sana, ila muache aende tafuta wa saizi yako uishi nae. Huyo ameshajazwa sumu na wafanyazi wenzake hapo hakuna tena mapenzi.
 
Wanaume mafala mnateseka sana, kaa kimya akidai talaka mwambie aende kuanza procedures za mahakamani Kabisa.
Sio rahisi kihivyo wanawake wengine ni mgodi unaotembea. Unakuta mwanamke ni mchapakazi, anakupa heshima ya mume, hana makorokoro ya kando, mzuri na mtamu, hana tabia ya kuomba pesa hovyo anasolve mambo yake. Halafu wewe unakuwa mlevi pesa yake ya malengo unapigia liquor. Akikuambia anataka kusepa lazima kichwa kiwake moto
 
Furaha haipo tena wakuu nimedaiwa talaka na mke wangu usiku wa kuamkia leo, mimi mke bado namuhitaji
Kama mwanamke siyo mjamzito au hajanifumania na mchepuko mwingine sisi wanaume huwa tunampa anachokitaka ikiwa tuu anachotaka ni "anaomba talaka au anaomba tuachane" na hatuulizagi sababu wala kuonyesha kumng'ang'ania japo kuwa hatumwambii aondoke wala hatusitishi huduma tuna muacha aondoke mwenyewe na asipo ondoka tunafanya kama hakuna kilichotokea maisha yanaendelea

Ila kama ni mjamzito na tunajua kabisa mimba ni yangu hata aombe talaka au aseme tuachane, atukane au alete vimbwanga ndani huwa tunapuuzia hapati chochote maana tunajua siyo yeye ni homoni zinampelekesha japo wakati mwingine huwa tunajua wanafanya makusudi kwa kigezo cha mimba na tunaamua kunyamaza tuu.

Sasa ndugu yangu hapo pima maana wewe ndiye unaye ishi nae na kila mtu ana style ya kuishi na mwezake. Wangu alikua hana mimba ila yupo kama huyo japo alikua anapanga na nguo kabisa kwenye mabegi nikawa na mjibu "sawa" naacha hela ya matumizi alafu naendelea na mishe zangu, jioni narudi usiku sana na mkuta kapika chakula na maji ya kuoga kaniandalia na anacheki tamthilia ananisubiria nikifika ananiuliza nimetoka wapi" na mjibu kazini , akihoji sana na mwambia simple ulinambia unaondoka hivyo nikaona hakuna sababu ya kuwahi nyumbani bora niendelee na mishe zangu anaishia kunambia wewe endelea na malayer zako na penzi ananipa usiku kucha akizani ananikomoa. Ndivyo navyo ishi nae mpaka wa leo hii.

Alipokuwa na mimba kesi zikaongezeka nikawa sieleweki mpaka anafika muda mwingine ananiomba msamaha na jibu sawa japo mara moja moja na mtoa out na vizawadi na tulia zangu.. yani si mind kitu mpaka ananiambiaga wewe ni pasua kichwa na mjibu kama wewe ulivyo mkata kichwa anacheka life linasonga mbele


Sijawahi mtamkia aondoke ila na jibu "sawa" na haondoki zaidi anazidisha upendo. Kuishi na hawa viumbe muda mwingine unatakiwa uwe mwanaume umejizima data na usichukulie kila kitu serious utaumia yani chukulia vitu simple simple japo mara moja moja una kaza ili asikuzoe
 
Ukweli ni kwamba kuishi na mwanamke muajiliwa wakati mume huna hela ni changamoto. Mkuu najua inauma sana, ila muache aende tafuta wa saizi yako uishi nae. Huyo ameshajazwa sumu na wafanyazi wenzake hapo hakuna tena mapenzi.
Kijana ndio anazingua anaenda tofauti na malengo
 
Furaha haipo tena wakuu nimedaiwa talaka na mke wangu usiku wa kuamkia leo, mimi mke bado namuhitaji. Chanzo cha yote(tatizo) ni mimi haihusiani na usaliti na tulishakaa vikao na familia tukayamaliza lkn mara zote toka hapo haijawahi kuisha wiki bila kununiana furaha siku 3 nne zillizobaki ni sintofahamu pamoja na kuwa anatimiza majukumu yake yote kama mke.

Usiku wa kuamkia leo baada ya kuniomba talaka yake alimpigia mama yake simu by 7 kasoro usiku kumueleza kuwa hana furaha tena! mama alikuwa na hamu ya kujua nini tatizo lkn binti alisisitiza siioni ndoa yangu tena na kukata simu ila kabla ya kukata alimuahidi kesho ntakuambia kila kitu.

Kwa hili sikuwa na namna sababu nilisharuhusu simu kupigwa japo baada ya kupiga simu nilimuomba usizungumze chochote na mama yako kuhusu hili wewe utajua namna ya kuongea ili kutuliza hali na ameniitikia kwa kunielewa, lkn sijui kichwani anawaza nini!

Nilimuahidi mimi pia nitazungumza na mama yake, jambo jingine nimemuomba nimuache peke yake kwanza nisafiri ili angalau upatikane muda wa utulivu kwanza lkn sio kumpa talaka.
Labda sasa mna mali nyingi

Btw, hivi kama mwanamke anaiihitaji talaka kwa hamu hawezi itoa yeye?
 
Sio rahisi kihivyo wanawake wengine ni mgodi unaotembea. Unakuta mwanamke ni mchapakazi, anakupa heshima ya mume, hana makorokoro ya kando, mzuri na mtamu, hana tabia ya kuomba pesa hovyo anasolve mambo yake. Halafu wewe unakuwa mlevi pesa yake ya malengo unapigia liquor. Akikuambia anataka kusepa lazima kichwa kiwake moto

Kuna makosa umefanya then, mbona hujayasema ? Hakuna mwanamke anayetaka talaka asiye na mwanaume, elewa Hilo Kijana, narudia elewa Hilo Kijana, Hakuna mwanamke anayetaka kuondoka kwa mwanaume ili aende kutafuta mwanaume!

Endelea kulazimisha, utaondoka hapo kwa usaliti, eti mtamu? Pumbavu kabisa
 
Back
Top Bottom