Huu ni ulimbukeni au utoto?

Huu ni ulimbukeni au utoto?

Kuna watu wanafedhehesha sana, tena wengine wakiwa ni watu wazima waliofika miaka 40 au zaidi huku wakiwa wanaandika hovyo wakati wa kutuma ujumbe hasa WhatsApp au hata sms za kawaida.

Mtu mzima unamtumia mwanaume mwenzako sms eti inasema "oi, xafi, vepee, xhwari nk! Hivi watu huwa hamuoni kama ni upuuzi huo? Tena mnatuma hata kwa mtu mwenye heshima zake, si atajihisi umemuona ni wa aina yako? Hivi sijui ni kwanini kuna watu hawajishtukii hata ukipotezea jumbe zao!

Kwa kweli kama bado unaandika kipumbavu hivyo ni bora ukaacha tu, na wale mnaokereka na watu wa aina hiyo ni vema mkapotezea mawasiliano yao kama hamuwezi kuwapa cha mbavu ili wajue wewe sio mpuuzi kama wao.

Wewe uliyoyaandika unaona upo sahihi katika dhima halisi ya kimantiki katika lugha hii adhimu ya kiswahili?"ni vyema mkapotezea mawasiliano yao"
Unafahamu kua hilo neno "kupotezea" ulivyolitumia humu sio maana yake katika kamusi ya TUKI?
Sitetei ulichozungumza ila kama.unataka kuelimisha umma nawe uwe sehemu ya mapokeo chanya.
Lakini tambua lugha inakua na wazungu wanasema "not every non sense is a non sense".
Lugha inatambua Rejesta kama sehemu ya nakshi katika lugha yoyote duniani..
Ni mawazo tu
 
Back
Top Bottom