Huu ni ukweli kuhusu samaki aitwaye chunusi

Huu ni ukweli kuhusu samaki aitwaye chunusi

Mvuvi maarufu na mtaalamu wa mambo ya bahari na mito, bwana Hmood Nassor Hamdoun anaeleza dhana moja ndegefu inaoaminika na wengi hasa wa mwambao mwa pwani kwamba baharini kuna jini liitwalo Chunusi.

Akitumia picha tanzu bwana Hmood anasema, katika picha anaitwa chunusi ila kwa jina lingine anaitwa "electric eel". Anafanana na kambale. Anatoa umeme wa aina ya tuli (static electricity) hadi vilt 850v.

Kiwango hicho cha umeme kinatosha vizuri kuua binaadamu na damu kuganda ndio maana utasikia wanasema jini chunusi ananyonya damu.

Ni vigumu kumvua kutokana na maumbile yake na umeme autoao. Wengi hawajawahi kumuona ndiyo maana inabaki kuwa tu ni jini wa kwenye maji.

La Voice ni muafrica wa kwanza kugundua kuwa chunusi sio jini bali ni electric eel.


FB_IMG_1579083591024.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app

Source: fb ya Yericko Nyerere
 
Kuna tofauti gani kati ya electric cat fish apatikanaye ziwa Tanganganyika pamoja na mto Nile na huyo electric eel?

Maana huyo samaki umeme niliyemtaja ni samaki anayevuliwa kwa njia ya kawaida, anachunwa ngozi yake ambayo ni sumu kabla hajaandaliwa kwa kitoweo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hata aseme nini lakini tunajua kuwa Chunusi yupo na huyo samaki yupo pia. Niliwahi kumvua pale Salender bridge na nikamkimbia. Kama sio mzee mmoja aliyekuwepo pale akamuua kwanza nadhani hata ule mshipi ningelimuachia.
Kifo cha chunusi ni kuwa; Lazima akuzamishe kwenye tope jingi na kukukausha kabisa kabisa. Kweli huyo samaki (Mkunga) ni mbaya sana ila hakuzamishi
 
Hata aseme nini lakini tunajua kuwa Chunusi yupo na huyo samaki yupo pia. Niliwahi kumvua pale Salender bridge na nikamkimbia. Kama sio mzee mmoja aliyekuwepo pale akamuua kwanza nadhani hata ule mshipi ningelimuachia.
Kifo cha chunusi ni kuwa; Lazima akuzamishe kwenye tope jingi na kukukausha kabisa kabisa. Kweli huyo samaki (Mkunga) ni mbaya sana ila hakuzamishi
Huyo pichani sio mkunga. Mkunga Hana umeme ila wanang'ata Kama nyoka
 
Kawaida chunusi anazamisha mtu majini na kumkwamisha huko huko,haibuki juu.
Ila kuna wataalumu wa hayo mambobwakiingozwa na Mshana Jr wanaelekea Arusha katika ziwa Duluti kufanya utafiti wa kina.
 
Huyo pichani sio mkunga. Mkunga Hana umeme ila wanang'ata Kama nyoka
Kwa hiyo weye unataka kuungana na mleta hoja kuwa chunusi ni samaki?? Leta picha ya chunusi tukuarifu sehemu mbali mbali alipokaa huyo chunusi. Mpaka huko bara bado unaamini ati ni samaki?? Si wangeshavuliwa wengi?? Kwa nini awe mmoja mmoja tu?
 
Watu wa ziwa ~Tanganyika mukuje hapa maana mimi niliponea kuuawa na samaki umeme sababu afande wa Bulombola jkt alimgundua kabla sijamgusa. Kwa kiingereza ni electric eels. Wanatoa umeme kiboko ila huyu kwenye picha ni mrefu kuliko niliyetaka kumkamata. Ana madoa meupe ila yeye mweusi. Aliua samaki wote tuliovua wajkawa mishkajki baada ya kukaribiana nao. The funny thing is mtego haukutoboka..
 
Uongo! Samaki wenye umeme huku Kigoma tunawaita nyika.. wanavuliwa sana na tunawala Kama kawa. Ila huyo Chunusi ni majini ya majini..Nishashuhudia watu wengi wanakufa ajili ya chunusi kwenye bwawa tulilokua tunaogelea enzi za utoto.
Tena anaweza kukukausha Damu Wirelessly na ukafa.
 
Watu wa ziwa ~Tanganyika mukuje hapa maana mimi niliponea kuuawa na samaki umeme sababu afande wa Bulombola jkt alimgundua kabla sijamgusa. Kwa kiingereza ni electric eels. Wanatoa umeme kiboko ila huyu kwenye picha ni mrefu kuliko niliyetaka kumkamata. Ana madoa meupe ila yeye mweusi. Aliua samaki wote tuliovua wajkawa mishkajki baada ya kukaribiana nao. The funny thing is mtego haukutoboka..
Mbona tunawala kawaida tu
 
Uongo! Samaki wenye umeme huku Kigoma tunawaita nyika.. wanavuliwa sana na tunawala Kama kawa. Ila huyo Chunusi ni majini ya majini..Nishashuhudia watu wengi wanakufa ajili ya chunusi kwenye bwawa tulilokua tunaogelea enzi za utoto.
Tena anaweza kukukausha Damu Wirelessly na ukafa.
Wenzako wamefanya tafiti na wakakubalika duniani.

Wewe unaleta ngano eti ulikuwa unaogelea kwenye bwawa.

Aisee hizo elimu zenu sijui ndio tuziite memkwa.!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom