Dakika chache zilizo pita nilikuwa kwenye kikao cha watu walio kosa Vibali vya kuchana Mbao za SAO HILL,Aisee!!! watu wananung'unika na kukata tamaa kabisa na CCM ambayo ndiyo inamiliki majimbo yote mawili ya Wilaya Mufindi,kikao hiki kimehudhuriwa na watu wapatao 900 ukitutoa sisi tulio jipenyeza hali ilikuwa mbaya bwana wana dai CCM haina shukrani na Haijui dhamani yao.
Ni hivi baada ya kuvisubiri Vibali hivi kwa muda mrefu sana , Subira yao haikuvuta heri kwani wameambulia patupu.
Wakati wa mchakato wa kuomba vibali watu hawa walitakiwa na Manager wa shamba kuonesha viwanda vyao vya kupasulia mbao hivyo watu waliingia Benki na kukopa na walinunua mashine za kuchania mbao na hivyo maombi yao yalipokelewa.
Maajabu ni kwamba wanakijiji na wakaazi wa hapa wilaya ya Mufindi wengi wamekosa vibali na badala yake wamepewa watu ambao hata ramani ya wilaya hii hawaijui MFANO RITHONE Pia wafanya biashara wakubwa ndio wamekumbukwa,na Viongozi wa Serekali kama LUKUVI,MAKINDA na NAPE.
Kinacho chekesha zaidi kuna Watu walio fariki miaka mingi iliyo pita nao waliomba vibali na kupata,Kinacho wakera wapiga kura hawa ni jinsi wao wanavyo kosa kibali japo kila mwaka wanaomba lakini marehemu wanapewa na viongozi wa serekali kama Wakuu wa Wilaya,mikoa,OCDs,RPCs, na wengine wengi Mbona hawana viwanda na wamepewa vibali?
Mtu kama Chris Lukosi hana kiwanda sehemu yoyote hapa Wilayani lakini eti ana kibali,watu wanataka kujua iweje mtu kama Kangesa,AKYOO,MAKAMBAKU na Rithone wanaomba vibali kila mwaka na wanapata wakati wengine wanaomba zaidi ya mara 1000 na hajawahi kupata hata siku moja! hivi ni haki kweli watu hawa wameapa lazima kieleweke.
Hali ni mbaya kwa kweli na wameazimia kufungua kesi Mahakama kuu kuomba kusimamishwa kwa uvunaji wa mbao mpaka taratibu zilizo tumika kugawa vibali viainishwe.
Kuna mzee mmoja anasema kuwa baba yake alinyang'anywa shamba na kupanda miti na walikuwa wakiiangalia miti hiyo tangu zamani tena kwa lazima bila kupewa chochote lakini eti leo ananyimwa kibali japo ameomba kwa zaidi ya mara 317 inauma sana!
My take:- CCM kuweni na shukrani maisha bora ndiyo haya!