Huu ndiyo utamu wa CCM...

Huu ndiyo utamu wa CCM...

Hii ndo ilimfanya Chris Lukosi aone kuwa Tanzania imeendelea sana ndo maana akarudi CCM. Kweli ukiwa na akili za KiCCM ni kama umelaniwa
 
Naona kwenye huu uzi Magamba hawajitokezi..
 
Nilikuwa nashangaa sana kwanini lukosi ajitoe ufaham kiasi kile? Kumbe nae ukoo wa panya!!
 
Duh kweli hata ukiishiwa nguvu za kiume utaisingizia CCM.
 
Siku kukitokea moto hivi wataomba msaada wa vijiji vinavyozunguka kusaidia kuuzima? Hawajui umuhimu wa Corporate Social Responsibility
Dakika chache zilizo pita nilikuwa kwenye kikao cha watu walio kosa Vibali vya kuchana Mbao za SAO HILL,Aisee!!! watu wananung'unika na kukata tamaa kabisa na CCM ambayo ndiyo inamiliki majimbo yote mawili ya Wilaya Mufindi,kikao hiki kimehudhuriwa na watu wapatao 900 ukitutoa sisi tulio jipenyeza hali ilikuwa mbaya bwana wana dai CCM haina shukrani na Haijui dhamani yao.

Ni hivi baada ya kuvisubiri Vibali hivi kwa muda mrefu sana , Subira yao haikuvuta heri kwani wameambulia patupu.

Wakati wa mchakato wa kuomba vibali watu hawa walitakiwa na Manager wa shamba kuonesha viwanda vyao vya kupasulia mbao hivyo watu waliingia Benki na kukopa na walinunua mashine za kuchania mbao na hivyo maombi yao yalipokelewa.

Maajabu ni kwamba wanakijiji na wakaazi wa hapa wilaya ya Mufindi wengi wamekosa vibali na badala yake wamepewa watu ambao hata ramani ya wilaya hii hawaijui MFANO RITHONE Pia wafanya biashara wakubwa ndio wamekumbukwa,na Viongozi wa Serekali kama LUKUVI,MAKINDA na NAPE.

Kinacho chekesha zaidi kuna Watu walio fariki miaka mingi iliyo pita nao waliomba vibali na kupata,Kinacho wakera wapiga kura hawa ni jinsi wao wanavyo kosa kibali japo kila mwaka wanaomba lakini marehemu wanapewa na viongozi wa serekali kama Wakuu wa Wilaya,mikoa,OCDs,RPCs, na wengine wengi Mbona hawana viwanda na wamepewa vibali?

Mtu kama Chris Lukosi hana kiwanda sehemu yoyote hapa Wilayani lakini eti ana kibali,watu wanataka kujua iweje mtu kama Kangesa,AKYOO,MAKAMBAKU na Rithone wanaomba vibali kila mwaka na wanapata wakati wengine wanaomba zaidi ya mara 1000 na hajawahi kupata hata siku moja! hivi ni haki kweli watu hawa wameapa lazima kieleweke.

Hali ni mbaya kwa kweli na wameazimia kufungua kesi Mahakama kuu kuomba kusimamishwa kwa uvunaji wa mbao mpaka taratibu zilizo tumika kugawa vibali viainishwe.

Kuna mzee mmoja anasema kuwa baba yake alinyang'anywa shamba na kupanda miti na walikuwa wakiiangalia miti hiyo tangu zamani tena kwa lazima bila kupewa chochote lakini eti leo ananyimwa kibali japo ameomba kwa zaidi ya mara 317 inauma sana!

My take:- CCM kuweni na shukrani maisha bora ndiyo haya!
 
Mtani wangu Lukosi bana...... Kumbe ni Kifisadi hiki, Ex-Police ni Fisadi.
 
hivi haya mapovu yanayomtoka lukosi humu jf unadhani ni bure ? Ccm wako tayari kuwapa vibali wachina kuliko wazalendo ! Tuungane kumtokomeza huyu shetani .
 
Mtani wangu Lukosi bana...... Kumbe ni Kifisadi hiki, Ex-Police ni Fisadi.

mkuu , kumbe siku zote hujajua tu , kama una akili timamu na una hofu ya mungu huwezi kuwa mwanaccm , ukimuona wa hivyo ujue si bure .
 
Andaeni kura zenu, vibali hivyo ni vya miaka miwili tu.
 
Mlichokosea ni kutaka kwenda mahakamani. Nani aliwadanganya kuwa haki kama hizo zinapatikana mahakamani Tz hii...

Wanyalu na nyie mmezidi kuwa wapole, ngoja wawaonyeshe...
 
kama kuna dhambi isiyo weza kusamehewa na vizazi vijavyo ni kupigia kura MaCCM, au chama cha kifisadi, au wauza sembe, ua masogange....
 
Kumbe Chris Lukosi ni fisadi,ndiyo maana anakifagilia sana chama cha mafisadi(ccm) humu ndani

unadhani kilichompeleka CCM nini,kule kuna fursa za wizi,ulaghai,zuluma....
na ndio maana toka hili bandiko liwekwe hapa hajaruka jf
 
Mlichokosea ni kutaka kwenda mahakamani. Nani aliwadanganya kuwa haki kama hizo zinapatikana mahakamani Tz hii...

Wanyalu na nyie mmezidi kuwa wapole, ngoja wawaonyeshe...

Wanaipenda CCM kama nini cjui!!! Ona matokeo ya chaguzi zilizofanyika 16/06/2013:

Kata ya Mbalamaziwa wilaya ya Mufindi: CCM kura 1420; CDM kura 184

Kata ya Ng'ang'awe wilaya ya Kilolo: CCM kura 686; CDM kura 217.

Sasa wanalalamika nini kina Lukuvi kuchukua vibali???
 
Hivi nyie watu zimo mukichwa kweli?

Yaani niache kupiga box huku niende Mufindi kupasua mbao?

Naona sasa tumechokana
 
Back
Top Bottom