Deadbody
JF-Expert Member
- May 30, 2015
- 4,292
- 6,693
HUU NDIO MUUNDO WA KIJESHI KWA MAJESHI YOTE DUNIANI
Katika ulimwengu wa Kijeshi kuna mfanano mkubwa sana ambao watu wengi hasa 'Raia Wema' hawafahamu.
Labda tu niseme tu wazi kuwa mimi nimekulia jeshini maisha yangu yote yaliyopita mpaka hivi sasa navyoandika sio miaka mingi sana iliyopita ndio nikajitoa katika makambi ya jeshi hivyo naandika haya nikiwa najua nidhamu ya jeshi na kila aina ya maisha ya wanajeshi.
Nimekulia Kikosi 603 KJ Airwing(Miaka 19) na Nikahamia 511 KJ Gongo la mboto Ambapo nimekaa kambini mpaka mwaka 2015,baada ya hapo nikatoka rasmi kambini nihamia mtaani kwa Temba UKONGA nilipoanzisha maisha yangu binafsi.Thread hii naiandika nikiwa KWA TEMBA ukonga.
Labda tu niweke wazi kuwa mpaka hapo nilipofikia sijasema lolote kama mimi nimeishi huko kama Mwanajeshi.Sijawahi kuwa mwanajeshi wa jeshi la wananchi Tanzania na naandika haya nikiwa kama raia mwema tu mwenye moyo wa kizalendo na ambaye nalipenda sana jeshi letu JWTZ.
TWENDE MOJA KWA MOJA KWENYE MADA HUSIKA:
Katika muundo wa Jeshi(Hii ni kwa dunia nzima) askari wa Jeshi wamegawanywa makundi makundi kama ifuatavyo
1.FireTeam
Hii ndio kikosi kidogo zaidi katika muundo wa jeshi kikiongozwa na KOPLO(corpoal).
Kikosi hiki ni cha askari 3-4 tu.
-Koplo ambaye anaongoza kikosi hiv anakuwa na V mbili
2.Section
Hiki ni kikosi cha wanajeshi wapatao 8-12 na wanaongozwa na SAJENTI(sergeant)
-Sajenti ambaye anaongoa kikosi hiki ana V tatu tu.
3.Platoon
Hiki ni kikosi kinachoongozwa na LUTENI(lieutenant).
-Kikosi hiki kina wanajeshi wapatao 15-30
-LUTEN ana nyota mbili
4.Company(Tanzania tunaita kombania)
Hiki ni kikosi kinachoongozwa na CAMPTAIN au major
-Kiongozi wa kikosi hiki ana nyota 3(Captain) au ngao ya nchi(Major)
-Kikosi hiki kina wanajeshi 80-150
5.Battalion(Infantry )
Kikosi hiki kinaongozwa na LUTENI KANALI()
-Hiki kinahusisha wanajeshi 300-800
-Luteni kanali ananyota moja na ngao ya nchi
6.BRIGADE
KKikos hiki kinaongozwa na Kanali au Brigedia.
-Hiki kinahusishwa wanajeshi 2000-5000
-Kanali ana ngao ya nchi na nyota mbili,brigedia ana ngao ya nchi na nyota tatu(Huu mfumo Tanzania tumechana nao)
7.Division
Hiki kikosi huongozwa na Maj Jeneral na hujumuisha wanajeshi 10000-15000
-Katika jeshi la uingereza maj gen ana mkasi na nyota moja ila ni tofauti na Kwetu ambapo ana mkasi na nyota mbili na ngao
(Hii ni kwa Tanzania )
8.Corps
-Hiki hujumuiya wanajeshi 20000-40000 na Huongozwa na LUTENI JENERAL
-Katika jeshi la Uingereza Lt Gen ana mkasi,ngao na nyota moja ila kwetu sisi ni tofauti toka 2015 september
9.Field Army
-Hii hujumuisha wanajeshi 80000+ na huongozwa na General
-Tanzania Gen ana nyota 4,mkasi na ngao.
10.Army group
-Kikosi hiki huongoza na Field marshal
-Ambacho huusisha Army group kuanzia mbili na kuendelea
-nchi yetu haina Field marshal hivyo majukumu yake yapo chini ya General
11.Theater (Warfare)
Hiki kikosi huongoza na mkuu wa nchi ambato hujumuisha askari (4+Army group) yanii Army groups 4 na kuendelea
Sengwile Makamanda