Hussein Bashe anatoa wapi jeuri aliyonayo?

Hussein Bashe anatoa wapi jeuri aliyonayo?

Bashe na Mkuu wa nchi.

Hawa ndio wanachama wa CCM wanao simamia kile wanachoamini ni MASILAHI ya WANANCHI (sio chama)

Hawaongozwi na UNAFIKI...
 
Huyu Bashe bado haamini kwamba yale mapesa yote aliyokuwa anasafirisha kuwapa wanachama wa CCM sehemu mbalimbali TZ kuhakikisha jamaa anateuliwa na CCM kuwa mgombea wa Urais kwamba eti hayakufanikisha. Inauma sana haswa inapotokea kuwa aliyeteuliwa na CCM hakutumia pesa yoyote!!!! Hata siku moja Bashe hawezi kukubaliana na yule ambaye hakutumia pesa lakini akambwaga yule jamaa aliyekuwa anajaza gari mapesa na kulindwa na wana usalama wa taifa na TAKUKURU ambao nao walipewa mgao. Hata hivyo inauma kweli hata ingekuwa mimi ningeumia na ningempinga huyu jamaa kwa nguvu zote.

Ila kwa sasa hivi akili za wabunge wote wa ccm (wa kuchaguliwa, viti maalum na wale wa kuteuliwa) pamoja na mawaziri wao hawamfikii Bashe.
 
Tena ulitakiwa ushukuru kwakua na mbunge kama Bashe,,ni mtu ambaye hayumbishwi tena ana msimamo,,nadhani ni yeye tu pale kijani ndie mwenye akili,,wengine wote maliangiri

Acha kuwatusi wazee wewe.
 
Huyu Bashe bado haamini kwamba yale mapesa yote aliyokuwa anasafirisha kuwapa wanachama wa CCM sehemu mbalimbali TZ kuhakikisha jamaa anateuliwa na CCM kuwa mgombea wa Urais kwamba eti hayakufanikisha. Inauma sana haswa inapotokea kuwa aliyeteuliwa na CCM hakutumia pesa yoyote!!!! Hata siku moja Bashe hawezi kukubaliana na yule ambaye hakutumia pesa lakini akambwaga yule jamaa aliyekuwa anajaza gari mapesa na kulindwa na wana usalama wa taifa na TAKUKURU ambao nao walipewa mgao. Hata hivyo inauma kweli hata ingekuwa mimi ningeumia na ningempinga huyu jamaa kwa nguvu zote.
Uelewa wako ni mdogo sana! Huu ujinga upeleke facebook
 
  • Thanks
Reactions: SDG
Hussein Bashe Kayanda alipambana peke yake hadi akafikia hatua ya kuuza ng'ombe wake na hakuishia hapo.Alikuwa akiwapikia wali wapiga kula wake kila siku huku CCM wamejikausha kama hawapo.Mwisho wa siku akaamua kujitoa muhanga na kwenda kuoga katikati ya makutano ya barabara pale Round about ya Nzega ili mambo yaende sawa.So sishangai kumuona akiwa na msimano binafsi japo sijui kwa nini haogopi.Au Kinana anam....?
 
Mwenye jibu atupie hapa tafadhali.

View attachment 533308

Matawi yote aliyoyazindua yeye hayana alama yoyote ya CCM bali ni TEAM BASHE...




Kwa kuwa ni rahisi zaidi katika serikali hii mtu kupotea kuliko fedha ya serikali kupotea,na kwa kuwa atakayekula fedha ya serikali itatokea katika tundu lolote la mwili wake,ni bora mumpoteze tu huyo Bashe kuliko kuendelea kuiyumbisha serikali yetu tukufu yenye dhamira ya kweli ya kumkomboa mnyonge wa Taifa hili.
 
Huyu Bashe bado haamini kwamba yale mapesa yote aliyokuwa anasafirisha kuwapa wanachama wa CCM sehemu mbalimbali TZ kuhakikisha jamaa anateuliwa na CCM kuwa mgombea wa Urais kwamba eti hayakufanikisha. Inauma sana haswa inapotokea kuwa aliyeteuliwa na CCM hakutumia pesa yoyote!!!! Hata siku moja Bashe hawezi kukubaliana na yule ambaye hakutumia pesa lakini akambwaga yule jamaa aliyekuwa anajaza gari mapesa na kulindwa na wana usalama wa taifa na TAKUKURU ambao nao walipewa mgao. Hata hivyo inauma kweli hata ingekuwa mimi ningeumia na ningempinga huyu jamaa kwa nguvu zote.
Bashe ndo mbunge pekee aliyebaki ccm ninayemkubali kwa 100% mwingine alishatangulia mbele ya haki hayati Philikunjombe
 
Anajua hata akitoka CCM akaenda chama kingine cha siasa bado ataendelea kuwa mbunge kutokana na heshima aliyojijengea
true.

2020 CCM hawatamrudisha Bashe bungeni, kwa hiyo ajipange kugombea kupitia opposition platform.
kama atahisi wapiga kura wake jimboni kwake ni misukule ya CCM na kuna uwezekano wa kutomchagua kupitia upinzani, sisi wa jimbo la huku Busokelo (Mbeya) tunamhitaji fasta na tutamrudisha bungeni kupitia UKAWA ili rais atakayechaguliwa kupitia UKAWA ampe uwaziri kijana achape kazi.

watu wa Busokelo hatutakagi ujinga sisi!!
 
Bashe atakuwa anaungwa mkono na watu wenye itikadi ya vyama tofauti na wale wasiokuwa na itikadi ya Chama chochote zaidi ya CCM.
Fanya facibility study kwa wabunge woooote wa ccm utagundua bashe ndo mbunge pekee aliyepo ccm anayekubalika vyama vyooote, hata atoke Leo ccm, ubunge kwake hauna shaka, ni muwazi anaongea kitu kilichopo si mnafiki ambayo ndio nguzo kuu uwapo ccm, mi ni shabiki wa cuf lkn akisimama bashe kugombea na cuf yangu bashe anachukua kura yangu mchana kweupeeee....
 
Bashe ni jasiri wa kuamini na kusimamia msimamo anao amini tatizo ccm utamaduni huu kwenu ni mgeni hivyo mmekuwa kasuku wa kuiga sauti ya mwenyekiti zama za kauli mbiu ya zidumu fikra za mwenyekiti zama hizo kwenye kizazi cha akina Bashe na Nape hazina maana tena kila mmoja ana fikra huru hata ww mtoa mada kuwa na fikra huru
 
Kuna msukuma na silinde.Huwa siwaelewi wanaongeaga nini bungeni
Msukuma MGANGA wa kienyeji na silinde mjenz wa mashinabya ccm, usirudie kumfananisha Bashe na majitu ya hovyo hovyo, kiongozi utakuwa unakosea sana....
 
Namkubali sana huyo jamaa......ngoja tu azidishe kiburi namuombea mema tu
 
Bashe ni jasiri wa kuamini na kusimamia msimamo anao amini tatizo ccm utamaduni huu kwenu ni mgeni hivyo mmekuwa kasuku wa kuiga sauti ya mwenyekiti zama za kauli mbiu ya zidumu fikra za mwenyekiti zama hizo kwenye kizazi cha akina Bashe na Nape hazina maana tena kila mmoja ana fikra huru hata ww mtoa mada kuwa na fikra huru

Mtoa mada?Sawa Kayanda.
 
Back
Top Bottom