Nicholas
JF-Expert Member
- Mar 7, 2006
- 25,260
- 7,195
Huyu dogo CCM wanalaziisha sana coverage yao.Huyu mchambuzi ana hoja za msingi sana lakini kwakuwa anakwenda kinyume na matarajio ya UKAWA kipindi hichi cha uchaguzi basi anaonekana mpumbavu na lofa. Aliyokuwa anasimamia juu ya mgombea mwenye maadili CCM ndio hayo hayo anayosisitiza mpaka UKAWA.Tuwe wakweli tuache kumshambulia Polepole, nakumbuka kabla ya Lowassa kuja UKAWA wapenzi wa CHADEMA pamoja na viongozi wao waandamizi walikuwa wakimshambulia sana Lowassa, rekodi zipo kwenye mitandao.Baada ya kukatwa huyo na kuhamia kwa wasakatonge basi wafuasi wa CHADEMA na UKAWA kwa ujumla wamejitoa akili na kusifia walichokuwa wakikipinga... Huu ni upumbavu.Tubadilike tufanye siasa zenye mashiko tuweze kumpata kiongozi atakayeweza kutupeleka kwenye nchi ya ahadi.Mimi kura yangu simpi kiongozi aliyeuza na kuifilisi ranchi ya Kitengule na kupeleka mradi wa maji Geita kwa sababu ana maslahi na madini kupitia kampuni dhalimu za madini, huku akiacha sehemu kubwa ya kanda ya Ziwa ikiwa haina maji.Majibu Ya Julius Mtatiro