Hukumu ya Kesi ya Uchaguzi Biharamulo

Hukumu ya Kesi ya Uchaguzi Biharamulo

Don't comment unless u are well informed. Mkuu wala hakuna mkoa wa CHATO kamanda. Biharamulo haiko mkoa huo na haijawahi kuwa mkoa mwingine zaidi ya KAGERA tangu Yesu apae kwenda Mbinguni. Chato iko mkoa mpya wa Geita na zamani ilikuwa tarafa ndani ya wilaya ya Biharamulo. Na lilikuwa jimbo mwaka 1995 lilipotajwa kuwa JIMBO LA BIHARAMULO MASHARIKI. Ni kujaribu kurekebishana ili kuweka kumbukumbu sawa.

UPDATES: Hukumu bado inasomwa na nimepata taarifa hii kutoka kwa jamaa angu ambaye yuko ndani ya mahakama, alitoka tu kunijuza na amerudi, simu kazima tena na anasema jamaa anasoma hukumu taratibu sana na anapangua baadhi ya hoja!!!!!!

Mtajuzwa tu wakuu!!!!!

well noted mkuu
 
Huu sasa ni msala. Inakuwaje hakuna mwanaJF hata mmoja anajua matokeo ya hiyo hukumu mpaka sasa? Nashindwa kuamini.

Tiba
 
nadhani matokeo kama kweli yatakuwepo ni bora kuyasikilizia kwa zitto kwenye twitter/facebook
 
Unauliza au unapotosha??
Threads zipo nyingi humu JF, hii achana nayo!!

Wilaya ya Chato ipo mkoa mpya wa Geita.
Mkoa wa Kagera = Bukoba, Muleba, Karagwe, Ngara, Kyerwa (mpya) na Biharamulo

i stand to be corrected mkuu
 
Jamani jamani kuweni na subira!! Hukumu jaji ndo anaingia chemba, hukumu itakuwa tiyari kufikia saa nne!!

(duh! Bora tupeane moyo2)
 
CONFIRMED: Kama jamaa yangu alokuwa mahakamani hakunidanganya basi kanambia kuwa hukumu imetolewa na upande wa mashataka "CCM" wameshindwa na hivyo Mh. Dr Mbassah (CHADEMA) anaendelea kuwa mbunge wa Biharamulo. Nasema kuwa " kama hajanidanganya" kwa kuwa ni rafiki yangu na ni mtani wangu pia, nimeongea naye kwa simu na nimesikia watu wanashangilia. Naomba kama matokeo ya hukumu yatakuwa tofauti basi nisilaumiwe kwani that was the only informer of mine. Nadhani nimeeleweka!!! THITHIEMU CHALI!!!!! Bila shaka Mukasa (CCM) atapaswa kulipa gharama za kesi ( kama ni kweli)
 
Back
Top Bottom