Robert Heriel Mtibeli
JF-Expert Member
- Mar 24, 2018
- 21,340
- 51,900
Kwema Wakuu!
Sijui anatumia uchawi gani.
Sijui anatumia mbinu gani za kimedani.
Lakini huyu jamaa kwa sasa hakuna mwanasiasa yoyote ambaye anamsogelea kwa umaarufu hata kwa kilometa mia moja.
Kama ni riadha za siasa tunasema Makonda angeshatangazwa ndiye Mshindi kwa sababu tangu aingie kwenye riadha amewaweka wenzake wote pembeni na sio tuu pembeni bali mbali huko.
Jana kwenye Malumbano ya Hoja, ITV Makonda mbele.
Sokoni huko Makonda.
Bodaboda nao Makonda.
Kwenye Daladala Makonda.
Kwani Makonda kafanyaje?
Nilipofuatilia zaidi wengi wa washangiliaji wake wanasema kuwa Makonda ndiye Mtetezi wao, Makonda ndiye Magufuli wao.
Kwamba kwa nchi hii Watanzania waliowengi wanamchukulia Magufuli ndiye Masihi na sasa mrithi wake ni Makonda. Hayo ni mawazo na mtazamo wa watanzania hasa wa hali ya chini ambao ni zaidi ya asilimia 80 hivi.
Sio Chadema, sio ccm, sio Act hakuna mwanasiasa mashuhuri na mwenye ushawishi kwa Tanzania kumzidi Makonda. Hii inamaanisha nini? Kama hali itaendelea hivi basi Watu wataanza kumpenda na upendo siku zote uko na nguvu kuliko Mauti.
Ingawaje mimi sio mfuasi wa siasa za Makonda lakini nikiri kwa ukweli kuwa yeye ndiye amebeba kwa sasa siasa za nchi yetu. Jina lake likiwa kubwa na lenye kuandikwa na kusemwa na waliowengi.
Wasalamu
Sijui anatumia uchawi gani.
Sijui anatumia mbinu gani za kimedani.
Lakini huyu jamaa kwa sasa hakuna mwanasiasa yoyote ambaye anamsogelea kwa umaarufu hata kwa kilometa mia moja.
Kama ni riadha za siasa tunasema Makonda angeshatangazwa ndiye Mshindi kwa sababu tangu aingie kwenye riadha amewaweka wenzake wote pembeni na sio tuu pembeni bali mbali huko.
Jana kwenye Malumbano ya Hoja, ITV Makonda mbele.
Sokoni huko Makonda.
Bodaboda nao Makonda.
Kwenye Daladala Makonda.
Kwani Makonda kafanyaje?
Nilipofuatilia zaidi wengi wa washangiliaji wake wanasema kuwa Makonda ndiye Mtetezi wao, Makonda ndiye Magufuli wao.
Kwamba kwa nchi hii Watanzania waliowengi wanamchukulia Magufuli ndiye Masihi na sasa mrithi wake ni Makonda. Hayo ni mawazo na mtazamo wa watanzania hasa wa hali ya chini ambao ni zaidi ya asilimia 80 hivi.
Sio Chadema, sio ccm, sio Act hakuna mwanasiasa mashuhuri na mwenye ushawishi kwa Tanzania kumzidi Makonda. Hii inamaanisha nini? Kama hali itaendelea hivi basi Watu wataanza kumpenda na upendo siku zote uko na nguvu kuliko Mauti.
Ingawaje mimi sio mfuasi wa siasa za Makonda lakini nikiri kwa ukweli kuwa yeye ndiye amebeba kwa sasa siasa za nchi yetu. Jina lake likiwa kubwa na lenye kuandikwa na kusemwa na waliowengi.
Wasalamu